Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 11 January 2014

TUNAJIFUNZA NINI KWA HABARI YA LAZARO ALIYEFUFULIWA NA BWANA YESU


Mtumishi Gasper Madumla.
Karibu tuendelee kujifunza zaidi siku ya leo,ikiwa leo ni siku ya nne ya fundisho hili.
Tunajifunza mambo mengi sana kupitia habari ya Lazaro wa Bethania mwenyeji wa mji wa Mariumu,yule aliyefufuliwa na Bwana Yesu.Yapo mambo ambayo ni msaada kwetu,na kupitia hayo tutavuka,
Basi nakusalimu katika jina la Bwana Yesu;
Bwana Yesu asifiwe…
Karibu tuendelee...
Na hapa tunasoma;

NINA WASIWASI YANGA WANAUVAGAA MKENGE KWA PLUIJM

YANGA SC inasaka kocha Mkuu, baada ya kumfukuza Mholanzi Ernie Brandts mwishoni mwa mwaka na kuna uwezekano ikaangukia kwa Mholanzi mwingine, Johannes Franciscus ‘Hans’ van der Pluijm.
Habari za ndani kutoka Yanga zinasema, imemuita kwa mazungumzo, kocha huyo, aliyewahi kuifundisha Berekum Chelsea ya Ghana na anaweza kutua leo Dar es Salaam iwapo atafanikiwa kupata ndege.
Hakupata usafiri wa ndege kutoka Ghana kuja Dar es Salaam jana na ikaelezwa alikuwa anahaha kutafuta ndege ya kuunganisha na kama akifanikiwa basi atakuja nchini leo, ikishindana wakati wowote mapema wiki ijayo.


Pluijm anakuja kufanya mazungumzo na Yanga, baada ya uongozi wa klabu hiyo kuridhishwa na wasifu wake katika orodha ndefu ya walimu zaidi ya 30 walioomba kazi Jangwani.

MESSI ASHINDWA KUIBEBA BARCA LA LIGA


Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi akipiga kichwa katika mechi ya La Liga dhidi ya Atletico Madrid usiku huu iliyoisha kwa sare ya bila kufungana.

SHULE MASHUHURI YA ETON KUENDELEZA MICHEZO TANZANIA



Picha na Urban Pulse
Imeandikwa na Freddy Macha
Mradi wa majaribio ya mwezi mmoja ulioandaliwa na Waingereza kuendeleza shule sita wilaya za Arusha na Moshi unatazamiwa kuanza wiki hii, ilitangazwa London, mwishoni mwa juma. Wanafunzi Nicolas Zafiriou (18), Ali Lyon(19) na Tom Pearson (18) wakiwa na kocha wao Glen Pierce.

MAN UNITED YAZINDUKA, YAICHAPOA 2-0 SWANSEA CITY

KOCHA David Moyes amepumua kidogo baada ya Manchester United kushinda 2-0 dhidi ya Swansea City usiku huu Uwanja wa Old Trafford na kuepuka kipigo cha nne mfululizo na cha tatu Uwanja wa nyumbani.
Ushindi wa United leo katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya England umetokana na mabao ya Antonio Valencia dakika ya 47 na Dany Welebeck dakika ya 59
United sasa inatimiza pointi 37 baada ya kucheza mechi 21, ingawa inabaki nafasi ya saba kwenye msimamo.

La pili: Danny Welbeck akishangilia baada ya kufunga bao la pili

CHELSEA YAPANDA KILELENI ENGLAND BAADA YA KUIFUMUA 2-0 HULL CITY

MSHAMBULIAJI Eden Hazard 'amelipa' fadhila kwa kocha Jose Mourinho baada ya kuifungia Chelsea bao katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Hull City na kupanda kileleni mwa Ligi Kuu ya England jioni ya leo.
Huku ikiripotiwa kwamba tayari Paris St Germain wanamtaka kiungo huyo Mbelgiji wa Chelsea, Mourinho amesema wiki hii kwamba hatakubali hata ofa ya Pauni 100,000.
Alifunga bao lake dakika ya 57 kabla ya Fernando Torres kufunga la pili dakika tatu kuelekea mwishoni mwa mchezo. Chelsea imetimiza pointi 46 baada ya kucheza mechi 21 ikiwa juu ya Arsenal yenye pointi 45 na Manchester City pointi 44, ambazo zimecheza mechi 20.

Yuko sawa: Eden Hazard alifunga bao la kwanza Chelsea ikiilaza Hull City

KOCHA ALIYEMUIBUA VAN NISTERLOOY AJA KESHO KUFANYA MAZUNGUMZO NA YANGA

Na Prince Akbar, Dar es Salaam
KLABU ya Yanga SC imemualika kwa mazungumzo, kocha ‘babu’, Johannes Franciscus ‘Hans’ van der Pluijm, aliyewahi kuifundisha Berekum Chelsea ya Ghana, ambaye anaweza kutua Dar es Salaam kesho iwapo atafanikiwa kupata ndege.
Hakuna nafasi katika ndege za kutoka Ghana kuja Dar es Salaam na babu huyo anahaha kutafuta ndege ya kuunganisha na kama akifanikiwa basi atakuja nchini kesho, ikishindana wakati wowote mapema wiki ijayo.

Atakuwa kocha mpya wa Yanga? Hans van der Pluijm anatarajiwa kutua kesho kwa mazungumzo

YANGA YAWACHAPA WAZUNGU 3-0

Na Baraka Kizuguto, Antalya
YANGA imeanza vizuri katika kambi yake ya mafunzo nchini Uturuki baada ya kuifunga timu ya Ankara Sekerspor kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika pembeni kidogo ya eneo ililofikia katika mji wa Manavgat Antalya.
Kocha wa Young Africans aliwatumia wachezaji 18 jumla katika mchezo huo ambao wenyeji mara baada ya mchezo walimpongeza kwa timu yake kwa kucheza vizuri katika mchezo huo wa kirafiki.

Yanga iliyochapa Wazungu leo

UGANDA BINGWA NETIBOLI KOMBE LA MAPINDUZI 2014

Na Zaituni kibwana, Zanzibar
TIMU ya Taifa ya netiboli ya Uganda ikiwa chini ya nahodha wake, Peace Proscocia, leo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuifunga Tanzania Bara magoli 52-39.
Mchezo huo wa fainali umefanyika leo jioni jijini hapa kwenye Uwanja wa Gymkhana visiwani hapa.
Kikosi hicho cha kina dada wa Uganda kilianza vyema michuano hiyo baada ya kuanza kuwa mbele kuanzia robo ya kwanza ya mchezo huo kwa kumaliza wakia na magoli 11-9.

COASTAL UNION YAWALAZA WAARABU 2-0 OMAN


Coastal Union (wenye jezi nyekundu) wameanza ziara yao ya Oman leo kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Musannaa. Coastal ipo huko kwa ziara ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Friday 10 January 2014

YANGA DIMBANI KESHO DHIDI YA ANKARA SEKER SPOR.

Wakati mabingwa wa soka wa Tanzania Bara, Yanga kesho wanacheza mechi yao ya kwanza dhidi ya timu daraja la kwanza ya Ankara Seker Spor, uongozi wa timu hiyo leo utatangaza jina la kocha mkuu katika mkutano na waandishi wa habari.
Mechi hiyo itachezwa saa 9.00 za Tanzania kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Mashindano wa kimataifa wa Yanga, Seif “Magari” Ahmed amesema kuwa mazoezi ya jana yalifanyika asubuhi kutokana na jua kuwahi kuzama na hali ya hewa kubadilika.
Ahmed alisema kuwa wachezaji wanaendelea vizuri na mpaka sasa wamepania kufanya vyema katika mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua.


Alisema kuwa baada ya mechi hiyo, timu hiyo itaendelea na mazoezi kabla ya kucheza mechi nyingine mbili na timu za madaraja ya juu.

MSIBA MSIBA, MSIBA… KIONGOZI TASWA AAGA DUNIA

Na Dina Ismail, Dar es Salaam
MWEKA Hazina wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) na timu ya soka ya chama hicho, Sultan Sikilo amefariki dunia usiku huu katika hospitli ya Rufaa ya Muhimbili, Dar es Salaam.
Katibu wa TASWA, Amir Mhando ameiambia BIN ZUBEIRY usiku huu kwamba, Sikilo alifikishwa hospitali ya Muhimbili, ambako umauti uimfika akitokea hospitali ya Temeke, Dar es Salaam, Alhamisi wiki hii.

Pumzika kwa amani sahiba; Sultan Sikilo wa kwanza kulia

Hii ni kutoka Kenya jamaa amefufuka akiwa chumba cha kuhifadhia maiti


Hii ni kutoka kwa majirani zetu ambapo tunaambiwa Wananchi wa Kenya wameshangazwa na taarifa ya kuzinduka kwa mwanaume mmoja aliyedhaniwa kuwa amekufa ambapo alizinduka akiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali moja mjini Naivasha umbali wa kilomita tisini kutoka mji mkuu wa Kenya Nairobi.

NI MWAKA WA RAHA MSIMBAZ; ISIMBA YAFUZU FAINALI MAPINDUZI CUP.



Klabu ya Simba imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali ya kombe la Mapinduzi baada ya kuifunga URA ya Uganda mabao 2-0.

mabao ya Simba kwenye mchezo huo yamefungwa na beki Joseph Owino pamoja na kiungo Amri Kiemba huku kiungo Owen Kasule wa URA akilimwa kadi nyekundu kwa kumchezea madhambi Ramadhani Singano.

Simba sasa itacheza fainali siku ya Jumatatu na timu ya KCC pia toka nchini UGANDA iliyoitoa AZAM kwa mabao 3-2.





Hingera rasta; Wachezaji wa Simba wakimpongeza mwenzao, Amri Kiemba kushoto baada ya kufunga bao la pili  katika  Uwanja wa Amaan, Zanzibar.


Simba rahaa


Amri Kiemba akipambana na mabeki wa URA


Ramadhani Singano ''Messi' akifanya yake dhidi ya beki wa URA


Messi ni balaa


Beki wa Simba, Haruna Shamte akimdhibiti mshambuliaji wa URA


Beki wa URA akimdhibiti msambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe


Mfungaji wao bao la kwanza la Simba SC, Joseph Owino akiondoka na mpira


Awadh Juma wa Simba SC akipasua katikati ya wachezaji wa URA


Kiungo wa URA Milos Ilic akimtoka mchezaji wa Simba SC, Haroun Chanongo


Issa Rashid 'Baba Ubaya' wa Simba akigombea mpira na mchezaji wa URA


Katikati ni Amri Kiemba akiwa amesujudu baada ya kufunga bao la pili


Shabiki maarufu wa Simba SC, Abdulfatah Salim Saleh, mmiliki wa hoteli a Sapphire Court mjini Dar es Salaam kulia alikuwepo


Kikosi cha Simba SC leo


Makocha wa Simba SC kulia na wakisalimiana na makocha wa URA kabla ya mechi, Simba SC itamenyana na KCC ya Uganda pia katika fainali keshokutwa baada ya timu zote za Tanzania zilizoshiriki mashindano hayo kutolewa. 
NA  princezub@hotmail.com Mahmoud Zubeiry
www.tabasamuleo.blogspot.com

COASTAL UNION NDANI YA MUSCAT



Msafara wa Coastal Union baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Muscat, Oman jana kwa mwaliko wa klabu ya Fanja ya Oman. Coastal itakuwa huko Januari 23 kwa mazoezi na mechi za kujipima nguvu.

ROBERTO CARLOS USO KWA USO NA YANGA NCHINI UTURUKI, APIGA NAO PICHA.

Beki wa kushoto wa zamani wa Real Madrid na timu ya taifa ya Brazil Robert Carlos leo asubuhi amekutana na wachezaji na viongozi wa Yanga kabla ya mazoezi.
Carlos Kwa sasa ni kocha wa timu ya Sivasspor iliyopo Ligi Kuu nchini Uturuki, Yanga pamoja na Sivasspor zimeweka kambi kwenye hotel ya Sueno Beach zikijiandaa na mashindano mbali mbali yanazikabil,Yanga wakiwa wameweka kambi kujiandaa na raundi ya pili ya ligi kuu ya Vodacom wenzao Sivasspor wanajiandaa na mchezo kombe la chama cha soka nchini humo ambao utachezwa siku ya jumanne.

Roberto Carlos akiwa na wachezaji wa Yanga nchini Uturuki.

YANGA YAANZA MAZOEZI UTURUKI

AZAM FC YAVULIWA UBINGWA KOMBE LA MAPINDUZI, YAPIGWA 3-2 MBELE YA RAIS MWINYI AMAAN

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
NDOTO za Azam FC kubeba kwa mara ya tatu mfululizo Kombe la Mapinduzi, leo zimeyeyuka baada ya kufungwa mabao 3-2 na KCC ya Uganda katika Nusu Fainali ya michuano hiyo Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Shujaa wa timu ya Watunza Jiji la Kampala leo alikuwa ni William Wadri aliyefunga bao la tatu dakika ya 45 na ushei, akiunganisha krosi ya Habib Kavuma.
Kabla ya hapo, Tony Odur aliifungia bao la kusawazisha KCC na kuwa 2-2 dakika ya 51, akiunganisha pia krosi ya Habib Kavuma.

Kipre Tchetche akimtoka mchezaji wa KCC katika mchezo wa leo

Thursday 9 January 2014

Hii hapa ni ratiba ya movie kuanzia January 10 hadi January 11.


Moja ya movie mpya zitakazoanza kuonyeshwa wiki hii ni The family na hapa kuna trailer yake unaweza kuiangalia.

SIMBA SC NA AZAM KATIKA BONGE LA MTIHANI KOMBE LA MAPINDUZI LEO

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
TIMU mbili maarufu za Uganda, URA na KCC, leo zinaingia vitani dhidi ya timu nyingine mbili kubwa Tanzania, Azam FC na Simba SC za Dar es Salaam katika Nusu Fainali za Kombe la Mapinduzi, Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Timu ya Halmashauri ya Jiji la Kampala (KCC) itaanza kumenyana na Azam FC Saa 10:00 jioni kabla ya timu ya Mamlaka ya Mapato Uganda (URA) kuumana na Simba SC Saa 2:00 usiku.
Ni mtihani mgumu kwa Tanzania na kuna hatari Fainali ya Kombe la Mapinduzi mwaka huu ikakutanisha timu ya nyumbani na ya Uganda, au zote za wageni kutokana na ukweli kwamba KCC na URA ni tishio.

Kikosi cha Simba SC Kombe la Mapinduzi

REAL MADRID YAUA 2-0 KOMBE LA LIGI HISPANIA


Benzema akishangilia bao lake jana

WINGA Gareth Bale amecheza dakika 90 kwa mara ya kwanza 2014 wakati Real Madrid ikiinda mechi ya kwanza ya Kombe la Hispania hatua ya 16 bora na kuifunga 2-0 Osasuna.
Karim Benzema alifunga bao lake la 99 dakika ya tisa akiwa na jezi ya Real Madrid na kinda wa miaka 20, Jese akafunga la pili dakika ya 60. Lakini Real walipoteza nafasi kibao za kuongeza mabao kipindi cha pili ukiwemo mkwaju wa Bale uliotokana na Ronaldo kuchezewa rafu katika eneo la hatari.




Cristiano Ronaldo made a superhuman effort at the back post but couldn't keep his header down

UCHAGUZI WA TASWA FEBRUARI 16...


UCHAGUZI Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), unatarajiwa kufanyika Februari 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

YAYA TOURE ASHINDA TENA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA

Kiungo wa Manchester City Yaya Toure raia wa Ivory Coast ametawazwa kwa mwaka wa tatu mfululizo kuwa mwanasoka bora wa bara la Afrika.

Yaya aliwashinda Mnigeria John Obi Mikel aliyeshika nafasi ya pili na Didier Drogba.

Wednesday 8 January 2014

CHEKA KUZIPIGA NA MRUSI FEBRUARI DAR

Na Dina Ismail, Dar es Salaam
BONDIA Francis Cheka, anatarajiwa kupanda ulingoni Februari 8, mwaka huu kuzipiga na bingwa wa zamani wa WBA, Mrusi Valery Brudov katika pambano la uzito wa Light Heavy, ambalo bado haijafahamika kama litakuwa la ubingwa au la.
Cheka anataka kurejesha heshima baada ya hivi karibuni kupigwa na Fedor Chidinov nchini Urusi na kupokonywa taji lake la WBF, alilolipata Agosti mwaka jana kwa kumchapa Phil Williams wa Marekani mjini Dar es Salaam.

Cheka akimuadhibu Mmarekani, je ataendeleza ubabe wake Dar?

Akizungumza na Waandishi wa Habari mjini Dar es Salaam jana, Promota wa pambano hilo, Jay Msangi ambaye pia alikuwa promota wa pambano la awali alisema, ameamua kumuandalia Cheka pambano hilo kali pia ili aweze kuendelea kujenga rekodi yake kikamilifu.

ARSENE WENGER ANATAKA KUSAJILI MMOJA KATI YA HAWA WASHAMBULIAJI. WEWE SHABIKI WA ARSENAL UNGEPENDA YUPI ASAJILIWE KABLA YA DIRISHA DOGO KUFUNGWA.

Diego Costa ( Atletico Madrid )

Salomon Kalou ( Lille )

Monday 6 January 2014

KWELI EUSEBIO NDIYE MCHEZAHI BORA KUWAHI KUTOKEA NCHINI URENO ? na SHAFFIH

RONALDO AFIKISHA MABAO 400 USIKU HUU AKIIFUNGIA MAWILI REAL IKIUA 3-0 LA LIGA

MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo usiku huu amefunga bao la 400 katika jumla ya mechi 652 alizocheza, wakati Real Madrid ikiifunga Celta Vigo 3-0 na kuwakaribia vinara wa La Liga, Barcelona kileleni.
Ronaldo alifunga mabao yake katika dakika za 20 na 90 akimalizia krosi za Dani Carvajal na baadaye Gareth Bale, aliyetokea benchi kipindi cha pili, wakati bao lingine la Real limefungwa na Benzema dakika ya 67.

PIGO ARSENAL NA ENGLAND, WALCOTT NJE MIEZI SITA...ATAKOSA HADI KOMBE LA DUNIA

TIMU ya taifa ya England na Arsenal zimepata pigo kubwa baada ya Theo Walcott kutakiwa kuwa nje kwa kipindi chote kilichobaki cha msimu pamoja na Kombe la Dunia, baada ya kuumia goti.
Winga huyo alitolewa nje Jumamosi katika mechi ya Kombe la FA Arsenal ikiifunga Tottenham baada ya kuumia na baada ya vipimo anatakiwa kuwa nje kwa mzi sita kwa sababu ya maumivu ya goti la mguu wa kushoto.
Habari hizo hakika ni pigo kubwa kwa kocha wa timu ya taifa ya England, Roy Hodgson kuelekea Fainali za Kombe la Dunia katikati ya mwaka huu nchini Brazil.


Maumivu: Theo Walcott anatakiwa kuwa nje kwa miezi sita baada ya kuumia goti la mguu wa kulia

AZAM WAIFANYIA ‘ROHO MBAYA’ ASHANTI MAPINDUZI, WAICHAPA KIDUDE NA KUIPANDISHA BOTI KUREJEA ILALA

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
HATUA ya makundi ya Kombe la Mapinduzi imehitimishwa usiku huu kwa mchezo wa mwisho wa Kundi C, Azam FC ikiilaza Ashanti United bao 1-0 Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Bao pekee la Azam leo limefungwa na Mganda, Brian Umony dakika ya 60, akiunganisha krosi ya Kipre Tchetche kutoka wingi ya kulia.

Kipre Tchetche akimpongeza Brian Umony baada ya kufunga leo Uwanja wa Amaan

Kwa matokeo hayo, Ashanti inayofundishwa na kocha mkongwe, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ inaaga mashindano haya. Ashanti ilihitaji sare tu katika mchezo wa leo ili ifuzu Robo Fainali, lakini imalambwa kidude.

JINAMIZI LA FERGUSON LAENDELEA KUMTAFUNA DAVID MOYES.....



Imeandikwa na Jöel Chuku Verminatör

Suala hapo lipo wazi sana ... Wenye upeo na wasiotekwa na mapenzi na timu iyo waliona tangu msimu uliopita ila wale walio wenzangu wenye mahaba niue wakaona timu yao inanguvu...
Msimu uliopita Manchester ilichukua taji, kwakua Rooney na van persie walikua wapo vizuri hasa van persie hakupata maumivu ya mara kwa mara ila kiujumla team iyo ilikua ya kawaida sana kwa wachezaji ambao ferguson Alikua ana watumia ...

Sunday 5 January 2014

Azam: Kombe la Mapinduzi letu tena


NA MWANDISHI WETU

Baada ya timu yao kufuzu kucheza hatua inayofuata ya mashindano ya Kombe la Mapinduzi, benchi la ufundi la Azam FC limesema ‘muziki’ wao ndiyo kwanza umeanza kunoga huku wakiahidi kutwaa taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo.

HATIMAYE LEWANDOSKI AJIUNGA NA BAYERN MUNICH KWA MKATABA WA MIAKA MITANO



Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Robert Lewandowski atajiunga na klabu ya Bayern Munich kwa uhamisho huru mwishoni wa mwa msimu huu, mabingwa wa Ujerumani wametangaza.

Mshambuliaji huyo wa Poland, ambaye aliisadia Dortmund kushinda makombe mawili mfululizo ya Bundesliga 2011 na 2012, amesaini mkataba wa miaka mitano.

Lewandowski alitangaza nia yake ya kuondoka Westfalenstadion pindi mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu, na akawa anahusishwa na kujiunga na wapinzani wao Bayern.

Lewandoski, 25, alijaribu kulazimisha kuuzwa kipindi cha kiangazi kilichopita lakini Dortmund waligoma kumuuza na kusisitiza lazima amalize mkataba wake.

Mwenyekiti wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge alitangaza dili la Lewandoski, akisema: "Tuna furaha uhamisho huu umekamilika kwa mafanikio.

"Robert Lewandowski ni mmoja ya washambuliaji bora ulimwenguni, atakiongezea ubora kikosi chetu cha FC Bayern."

Mkwasa awashukia Okwi, Kiiza

NA SOMOE NG`ITU

Boniface Mkwasa

Kocha mkuu wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Yanga, Boniface Mkwasa, amekerwa na utovu wa nidhamu wa nyota wawili wa Kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza, hivyo kuhitaji kufanyika kikao na uongozi wa klabu hiyo ili kuwajadili.

Wachezaji hao wawili ndiyo pekee ambao hadi jana walikuwa hawajaripoti katika mazoezi ya timu hiyo inayojiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara na mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.