Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Wednesday 24 June 2015

Liverpool yamsajili Firmino wa Brazil

Liverpool imesajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino

Klabu ya Liverpool imemsajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino kutoka klabu ya Hoffenheim kwa kanadarasi ya miaka mitano itakayogharimu pauni millioni 29.

Mkataba huo utaandamana na ukaguzi wa kimatibabu ambao utafanyika baada ya mchezaji huyo kurudi kutoka Chile ambapo amekuwa akiichezea Brazil katika michuano ya Copa America.

Firmino ambaye amefunga mabao 47 katika mechi 151 akiwa katika kilabu ya Hoffenheim atakuwa mchezaji wa pili wa Liverpool aliyeghali mno.

Kilabu hiyo ya Anfield ilimfanya mchezaji Andy Carroll kuwa mchezaji ghali alipojiunga nayo kwa kitita cha pauni milioni 35 kutoka Newcastle mwaka 2011.

tabasamu leo

MICHEZO ,BURUDANI , INJILI
Hutoa habari za aina mbali mbali ikiwemo habari za:

HABARI


Haki haiombwi bali hudaiwa

Monday 12 May 2014


           KWA HABARI ZA MICHEZO,KITAIFA NA KIMATAIFA BONYEZA HAPAKWA HABARI ZA MICHEZO,KITAIFA NA KIMATAIFA BONYEZA HAPA

WWW.HAKILEO.BLOGSPOT.COM

ESSIEN NA BOATENG WAITWA KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA GHANA PIA KIFAHAMU KIKOSI CHOTE CHA GHANA

GHANA imewajumuisha Michael Essien na Kevin-Prince Boateng katika kikosi cha awali cha wachezaji 26 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.
Kikosi hicho kitapunguzwa na kubaki wachezaji 23 baada ya mchezo wa kirafiki na Uholanzi Mei 31, ambacho ndiyo watakwenda Brazil.
Essien na Boateng wameitwa baada ya kurejea kwenye soka ya kimataifa mwaka jana, kufuatia awali kuomba kujipumzisha kuichezea timu hiyo.

Kazini: Nyota wa AC Milan na mchezaji wa zamani wa Chelsea, Michael Essien ameitwa kwenye kikosi cha Ghana

Ghana ipo Kundi G pamoja na Marekani, Ujerumani na Ureno.

KIKOSI KAMILI HIKI HAPA;
Makipa: Stephen Adams (Aduana Stars), Fatau Dauda (Orlando Pirates), Adam Kwarasey (Stromsgodset)
Mabeki: Harrison Afful (Esperance), Jerry Akaminko (Eskisehirspor), John Boye (Stade Rennes), Samuel Inkoom (Platanias), Jonathan Mensah (Evian Thonon Gaillard), Daniel Opare (Standard Liege), Jeffrey Schluup (Leicester City), Rashid Sumaila (Mamelodi Sundowns)
Viungo: David Accam (Helsingborg), Afriyie Acquah (Parma), Albert Adomah (Middlesbrough), Emmanuel Agyemang Badu (Udinese), Kwadwo Asamoah (Juventus), Christian Atsu (Vitesse Arnhem), Andre Ayew (Olympique Marseille), Michael Essien (AC Milan), Rabiu Mohammed (Kuban Krasnodar), Sulley Muntari (AC Milan), Mubarak Wakaso (Rubin Kazan)
Washam uliaji: Jordan Ayew (Sochaux), Kevin Prince Boateng (Schalke 04), Asamoah Gyan (Al Ain), Abdul Majeed Waris (Valenciennes).
CHANZO BIN ZUBEIRY


WWW.HAKILEO.BLOGSPOT.COM

Saturday 10 May 2014

YANGA WATAKIWA KIGALI KABLA YA AGOSTI 9 KOMBE LA KAGAME

Na Baby Akwitende, Dar es Salaam
MASHINDANO ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu Kombe la Kagame yamepangwa kufanyika kuanzia Agosti 9 hadi 23 mwaka huu jijini Kigali nchini Rwanda.
Tanzania Bara itawakilishwa na Yanga katika mashindano hayo yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati ( CECAFA).
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana , Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, alisema timu zote wanachama wa shirikisho hilo zinatarajiwa kushiriki.

Kikosi cha Yanga SC

Musonye alisema kuwa bado sekretarieti haijateua timu mwalikwa katika mashindano hayo kutokana na mabadiliko ya kalenda ya michuano hiyo ambayo hufanyika kila mwaka kati ya mwezi Mei na Juni.
"Ratiba kamili ya mashindano hayo itatolewa baadaye", alisema Musonye.
Mlezi wa CECAFA na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ameshathibitisha kutoa zawadiambayo ni Dola za Marekani 60,000 ambazo alianza kutoa tangu mwaka 2002.
Wadhamini wengine waliothibitisha kudhamini mashindano ya mwaka huu ni kituo cha televisheni cha Super Sport.

Bingwa mtetezi wa mashindano hayo ni Atraco ya Burundi na mfungaji bora wa michuano hiyo alikuwa ni Amissi Tambwe, anayeichezea Simba akitokea kwa mabingwa hao.

Thursday 1 May 2014

TFF YATEUA WAKILI KUCHUNGUZA USAJILI WA DOMAYO AZAM FC

Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam
KUTOKANA na tukio lililotokea jana (Aprili 30 mwaka huu) kwenye kambi ya timu ya Taifa (Taifa Stars) iliyopo Tukuyu mkoani Mbeya likihusisha usajili wa baadhi ya timu, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemteua Wakili Wilson Ogunde kuchunguza mlolongo mzima wa tukio hilo.
Taarifa ya TFF kwa BIN ZUBEIRY leo asubuhi imesema kwamba, baada ya kukamilisha uchunguzi wake, Wakili Ogunde ataishauri TFF kuhusu hatua za kisheria na kikanuni za kuchukua.

Frank Domayo akisaini Azam FC jana
TFF imesema katika taarifa yake inatoa wito kwa wachezaji, klabu na wadau wa mpira wa miguu kufuata kanuni na taratibu katika utendaji wao.
Viongozi wa Azam FC jana walikwenda kwenye kambi ya Taifa Stars kukamilisha taratibu za usajili na kiungo Frank Domayo, aliyemaliza Mkataba wake Yanga SC.
Baada ya kufanikiwa kumsainisha Mkataba wa miaka miwili, wasimamizi wa kambi waliwaitia Polisi viongozi wa Azam FC ambao hata hivyo baadaye waliachiwa. Lakini inadaiwa fomu za usajili zilichanwa.
Azam si klabu ya kwanza kusajili mchezaji katika kambi ya timu ya taifa, kwani vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga ndiyo waasisi wa mchezo huo.
Mwaka jana Simba SC walisaini Mkataba mpya na kiungo wao, Amri Kiemba akiwa katika kambi ya Taifa Stars, hoteli ya Tansoma mjini Dar es Salaam.

Inaruhusiwa kwa wakubwa tu; Kiongozi wa Yanga SC, Seif Ahmed 'Magari' alimtoa kambi ya Taifa Stars, beki Kevin Yondan akiwa Simba SC na kumsainisha mwaka 2012.

Yanga SC iliwasajili Domayo kutoka JKT Ruvu, Kevin Yondan kutoka Simba SC wote wakiwa katika kambi ya Taifa Stars Dar es Salaam miaka miwili iliyopita.

CHELSEA NJE ULAYA, YAPIGWA 3-1 DARAJANI...FAINALI NI ATLETICO NA REAL MADRID

CHELSEA imeaga Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kufungwa mabao 3-1 na Atletico Madrid ya Hispania usiku huu Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Atletico sasa itakutana na jirani zao, Real Madrid katika fainali mwezi ujao nchini Ureno, ambao jana waliwang’oa mabingwa watetezi, Bayern Munich kwa 4-0 mjini Munich na kufanya ushindi wa jumla wa 5-0.

Heshima sasa; Diego Costa kushoto akishangilia na mchezaji mwenzake, Koke baada ya kufunga bao la pili



Fernando Torres alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya 36 kwa pasi ya Azpilicueta baada ya kazi nzuri ya Willian, lakini Adrian Lopez akaisawazishia Atletico dakika ya 44 kwa pasi ya Juanfran.
Diego Costa akafunga bao la pili kwa penalti dakika ya 61 kabla ya Arda Turan kumaliza kazi dakika ya 72 na Atletico imefuzu kwa ushindi wa jumla wa 3-1 baada ya sare ya 0-0 katika mchezo wa kwanza Madrid wiki iliyopita.
Mabadiliko yaliyofanywa na kocha Jose Mourinho dakika ya 54 kumtoa beki Ashley Cole na kumuingiza mshambuliaji Samuel Eto’o ndiyo yaliigharimu Chelsea. Eto’o ndiye aliyesababisha penalti iliyofungwa na Costa.

Wednesday 30 April 2014

MAYWEATHER AONYESHA JEURI YA FEDHA, SASA ATAKA KUNUNUA TIMU MAREKANI

KAMA anavyotamba katika ngumi za kulipwa hadi sasa akiwa hajapoteza pambano licha ya kupigana na mabondia wakali duniani, Floyd Mayweather anataka kununua klabu ya mpira wa kikapu Marekani, inayomilikiwa na milionea anayekabiliwa na kashfa ya ubaguzi.
Hakuna ajabu kwa mkali huyo wa kutupa mikono kwenye miili ya wenzake, anayekwenda kwa jina la utani Money Mayweather juu ya hilo, kwa sababu ana uwezo kifedha.
Floyd Jnr anataka kutoa dola za Kimarekani Milioni 40 ambazo ni sehemu tu ya pato lake la pambano la Jumamosi wiki hii, atakalolipwa dola bilioni 1.8 ili kuinunua Los Angeles Clippers.
Mutu ya fweza: Floyd Mayweather akiwasili ukumbi wa MGM Grand kuelekea pambano lake na Marcos Maidana

Kuhusu Marcos Maidana, Muargentina anayetarajiwa kupambana naye mjini Las Vegas, Mayweather amesema: "Amekuwa babu kubwa katika mapambano yake manne yaliyopita. Ana wastani wa asilimia 80 ya Knockout (KO). Hivyo siwezi kumdharau huyu jamaa,".
Kuhusu Clippers, ambayo mmiliki wake Donald Sterling amefungiwa maisha kujihusisha na masuala ya mpira wa kikapu baada ya kupatikana na hatia ya kuwatolea maneno ya kibaguzi watu weusi wa timu yake wakiwemo wachezaji, Mayweather amesema: "Ninataka kuinunua Clippers? Ndiyo. Naweza kuwaunganisha pamoja watu ambao watakuwa tayari.
"Kununua timu ya Ligi Kuu ya kikapu ni kitu fulani ambacho nataka kuongeza katika kampuni yetu inayokua kwa kasi ya Mayweather Promotions, ambayo sasa si kwa ajili ya ngumi tu, bali tunajihusisha pia na mavazi, muziki na sinema,"alisema.


Kifungo cha maisha: Mmiliki wa Los Angeles Clippers, Donald Sterling hawezi kujihusisha na masuala ya mpira wa kikapu baada ya kutoa kauli ya kibaguzi hadharani

KATIBU MKUU WA FIFA AWASILI KESHO DAR

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Jerome Valcke anawasili nchini kesho (Mei 1 mwaka huu) ambapo atafungua semina ya mawasiliano kwa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).

Valcke ambaye atafuatana na maofisa wengine saba wa FIFA baadaye kesho hiyo hiyo (Mei 1 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi kwenye hoteli ya Double Tree by Hilton iliyopo Oysterbay, Dar es Salaam.

Sunday 27 April 2014

MADOGO WA NGORONGORO WALIVYOWATOA WAKENYA JANA NA KUJIWEKA KWA NIGERIA


Kiungo wa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes, Mudathir Yahya akimtoka kiungo wa Kenya katika mchezo wa jana kuwania tiketi ya Fainali za Afrika nchini Senegal mwakani. Tanzania iliitoa Kenya kwa penalti 4-3 baada ya sare ya jumla ya 0-0. Ngorongoro sasa itamenyana na Nigeria katika hatua inayofuata.


Kevin Friday wa Tanzania akimuacha chini beki wa Kenya

Wachezaji wa Tanzania wakishangilia baada ya mechi


Ally Bilal wa Tanzania akimtoka Hillary Dan wa Kenya


Mange Chagula wa Tanzania kushoto akigombea mpira na Hillary Dan wa Kenya aliye tayari kusaidiwa na wenzake


Kipa wa Kenya, Farouk Shikhalo akidaka mpira huku akilindwa na beki wake, Hillary Dan aliye mbele ya Ally Bilal wa Tanzania

Kevin Friday wa Tanzania kulia akimtoka Victor Ndinya wa Kenya

Mange Chagula wa Tanzania akiteleza na mpira mbele ya Evans Makari wa Kenya

Iddi Suleiman wa Tanzania akiwatoka mabeki wa Kenya

Iddi Suleiman wa Tanzania akimuacha chini beki wa Kenya

Benchi la Ufundi la Tanzania wakati wa penalti jana

Thursday 24 April 2014

REAL MADRID NA BAYERN MUNICH KATIKA PICHA JANA BERNABEU


Juu kwa juu: Cristiano Ronaldo (katikati) akiwa ameruka juu zaidi ya Alaba (wa pili kushoto) na Dante kuwania mpira wa juu katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana Uwanja wa Bernabeu mjini Madrid, Hispania. Real ilishinda 1-0.
Franck Ribery wa Bayern Munich (kushoto) akimfukuzia Daniel Carvajal wa Real
Mfungaji wa bao pekee la Real, Karim Benzema akishangilia baada ya kufunga Uwanja wa Santiago Bernabeu
Kula gwala, kamalizie kazi: Ronaldo akimpisha Gareth Bale dakika ya 74
Philipp Lahm na Gareth Bale (kulia wakigombea mpira wa juu
Beki Mbrazil wa Bayern, Dante (kushoto) akipitia mpira miguuni mwa Angel di Maria wa Real
Thomas Muller (katikati) wa Bayern akililia penalti
Beki wa Real Madrid, Sergio Ramos (kushoto) akiosha mbele ya mshambuliaji wa Bayern, Bastian Schweinsteiger
Schweinsteiger akimdhibiti kiungo wa Real Madrid, Xabi Alonso (katikati)
Mabeki wa Real, Pepe (kushoto) na Sergio Ramos (katikati) wakienda hewani kuondosha hatarini mpira wa juu kutoka kwa Ribery



Kipa wa Real, Iker Casillas (kulia) akiokoa mpira kichwani kwa Javier Martinez
Cristiano Ronaldo akimtoka Jerome Boateng