Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Friday 18 April 2014

BARCELONA SASA RADHI KUMUUZA MESSI

MSHAMBULIAJI Lionel Messi anaamini Barcelona sasa inamchukulia kama mtu wa kuuzwa na si tena nyota asiyegusika katika kikosi chao, imeripotiwa chaneli ya Televisheni ya Esport3 ya Katalunya.
Kusuasua kwa mazungumzo ya kuongeza mkatab baina ya mchezaji huyo na klabu ni kielelezo cha kwa nini Messi anafikiria muda wake umekwisha Barcelona.
Inaelezwa kwamba Wajumbe wa bodi wanaamini mchezaji huyo ana thamani zaidi ya kuuzwa kwa sasa kuliko kuendelea kuwatumikia uwanjani, jambo ambalo Messi analitambua pia na anaamini ni juu ya Barcelona kuhusu Mkataba wake unaomalizika mwaka 2018.

Mwisho? Lionel Messi anaweza kuondoka Barcelona kutokana na kusuasua kwa mazungumzo ya Mkataba mpya
Paris Saint-Germain inaweza kuwa tayari kumlipa mchezaji huyo mshahara wa Pauni Milioni 205, na kutokana na mpango wa ujenzi wa Uwanja mpya unaoweza kuigharimu Barcelona Pauni Milioni 493, inawezekana klabu hiyo ikafanya uamuzi usiofikirika na kumuuza mchezaji huyo ambaye amekuwa Barcelona tangu ana umri wa miaka 13.
Messi anataka kubaki Barcelona hadi atakapofikiri wakati wa kurejea klabu yake ya kwanza, Newell’s Old Boys ya Argentina umewadia, lakini Barcelona inaweza kumuuza kwa klabu nyingine ya Ulaya kati ya PSG hata Manchester City.


Babu kubwa duniani: Messi akiwa na tuzo ya Ballon d'Or ya mwaka 2012
MAFANIKIO YA LIONEL MESSI BARCELONA
2004:Mechi 420 mabao 351
La Liga 2004-5, 2005-6, 2008-9, 2009-10, 2010-11, 2012-13
Kombe la Mfalme: 2009, 2012
Ligi ya Mabingwa 2006, 2009, 2011
Rais wa sasa wa Barcelona, Josep Bartomeu alitaka kumpa mkataba mpya Messi kabla ya Fainali za Kombe la Dunia, lakini mchezaji huyo inafahamika anataka malipo ya Pauni Milioni 20.5 kwa mwaka na klabu inataka nusu ya haki ya matumizi ya picha zake, wakati kwa sasa mchezaji huyo anamiliki haki zote.
Kushindwa kuonyesha kiwango kilichotarajiwa katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na fainali ya Kombe la Mfalme kwa mara ya kwanza vimeifanya bodi ifikirie uamuzi wa kumpiga bei.

Tuesday 15 April 2014

Arsenal yaipiga Weastium united 3-1

BARCELONA WATWAA TAJI LA LIGI YA MABINGWA ULAYA KWA VIJANA, KINDA WAKE AFUNGA KUTOKA KATIKATI YA UWANJA

KINDA Munir El Haddadi jana alifunga bao tamu kutoka katikati ya Uwanja Barcelona ikitwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa vijana chini ya umri wa miaka 19 kwa kuifunga Benfica mabao 3-0 mjini Nyon, Usiwsi.
Munir alifunga mabao mawili jumla jana dakika za 33 na 87, wakati bao lingine lilifungwa na Rodrigo Tarin dakika ya tisa.
Timu ya kwanza ya Barca ipo katika wakati mgumu hivi sasa ikiwa imetolewa katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na wapinzani wao Hispania, Atletico Madrid na ikafungwa 1-0 na Granada Jumamosi katika La Liga.
Na baada ya kufungiwa kusajili hadi mwaka 2015 na FIFA, adhabu ambayo wameikatia rufaa, Wakatalunya hao wanaweza kupandisha viranga vyao vya akademi.


Wafalme: Nahodha wa Barca, Roger Riera akiwa ameshika taji la Ligi ya Mabingwa kwa vijana jana baada ya ushindi


Nyota wa baadaye: Munir El Haddadi akisherehekea ushindi wa Barca wa 3-0 jana

MAN CITY YAFUNIKA KLABU ZOTE DUNIANI KWA KULIPA MISHAHARA MIKUBWA, HAKUNA CHA BARCA WA REAL

KLABU ya Manchester City ndiyo inayoongoza duniani kwa kulipa mishahara mizuri wachezaji huku kiwango cha malipo ya mwaka kwa kila mchezaji kikiwa ni Pauni Milioni 5.3, au Pauni 102,653 kwa wiki, hiyo ni kwa mujibu wa taarifa mpya ya mlinganisho wa mapato ya klabu kubwa.
Klabu tano za Ligi Kuu ya England zimeingia kwenye 20 Bora na Liverpool iliyoifunga 3-2 City katika mbio za ubingwa Jumapili- inashika nafasi ya 20, kwa kumlipa kila mchezaji wastani wa Pauni Milioni 3.4 kwa mwaka.
Manchester United ni ya nane ikilipa Pauni Milioni 4.3 kwa mwaka, Chelsea ya 10 (Pauni Milioni 4) na Arsenal ya 11 (Pauni Milioni 3.9).

Walipwa vizuri: Manchester City imeongoza kwa kulipa wachezaji mishahara mikubwa duniani, ikikadiriwa kumlipa kila mchezaji wastani wa Pauni Milioni 5.3 kwa mwaka.

Kimwaga noti: Mmiliki wa City, Sheikh Mansour amewekeza mabilioni ya Pauni katika timu hiyo ili iwe mshindani katika ubingwa wa England
KLABU ZINAZOONGOZA KULIPA MISHAHARA MIZURI WACHEZAJI DUNIANI

NAFASI (MWAKA JANA)TIMULIGIMAKADIRIO YA MALIPO KWA MWAKA (WIKI)

NAFASI (MWAKA JANA)TIMULIGIMAKADIRIO YA MALIPO KWA MWAKA (WIKI)
1 (1)Manchester CityPremier League£5,337,944 (£102,653)
2 (5)New York YankeesMLB£5,286,628 (£101,666) 
3 (2)Los Angeles DodgersMLB£5,119,701 (£98,456) 
4 (3)Real MadridLa Liga£4,993,393 (£96,027) 
5 (4)BarcelonaLa Liga£4,901,327 (£94,256)
6 (16)Brooklyn NetsNBA£4,485,019 (£86,250) 
7 (9)Bayern MunichBundesliga£4,402,905 (£84,671) 
8 (12)Manchester UnitedPremier League£4,322,251 (£83,120)
9 (19)Chicago Bulls NBA£3,985,706 (£76,648) 
10 (8) ChelseaPremier League £3,984,536 (£76,626)
11 (15)ArsenalPremier League£3,901,923 (£75,037) 
12 (20) New York KnicksNBA £3,862,191 (£74,273) 
13 (14)Detroit TigersMLB£3,833,510 (£73,721) 
14 (11)Philadelphia Phillies MLB£3,811,638 (£73,301) 
15 (22)Boston Red SoxMLB £3,763,451 (£72,374)
16 (17)Miami Heat NBA £3,665,215 (£70,485) 
17 (23)San Francisco GiantsMLB£3,613,741 (£69,495)
18 (35)Juventus Serie A£3,512,696 (£67,552) 
19 (7)LA Lakers NBA £3,411,402 (£65,604)
20 (21)Liverpool