Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 15 March 2014

DANIEL STURRIDGE MCHEZAJI BORA WA MWEZI ENGLAND, SAM ALLARDYCE KOCHA BORA

MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Daniel Sturridge ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya England kwa mwezi Februari, baada ya kufunga mabao matano katika mechi nne.
Nyota huyo ameisaidia Liverpool kushinda dhidi ya Swansea na Fulham pamoja na kuitandika mabao 5-1 Arsenal timu hiyo ya Anfield ikiweka hai matumaini ya kutwaa ubingwa.
Kocha wa West Ham, Sam Allardyce, ameshinda tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi baada ya kuiongoza timu yake kushinda mechi nne.

Mkali wa mwezi: Daniel Sturridge akiwa na tuzo ya Mchezaji Bora wa Februari

YANGA SC HAIJASHINDA MECHI MOROGORO MBELE YA MTIBWA SUGAR KWA MIAKA MITANO SASA, LEO ITAVUNJA MWIKO?

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
YANGA SC haijashinda mechi Uwanja wa Jamhuri Morogoro dhidi ya Mtibwa Sugar kwa miaka minne sasa na leo inashuka kwenye Uwanja huo kumenyana na Wakata Miwa hao wa Manungu.
Septemba 19 mwaka 2009 ndipo Yanga SC iliposhinda kwa mara ya mwisho Uwanja wa Jamhuri wakati huo ikiwa chini ya kocha Mserbia, Profesa Dusan Savo Kondic na tangu hapo kila inapokwenda huko matokeo mazuri kwao yamekuwa sare.
Wachezaji wa mwisho kuipa Yanga SC ushindi Uwanja wa Jamhuri dhidi ya Mtibwa walikuwa ni Nurdin Bakari aliyefunga dakika ya 55 na Mrisho Ngassa dakika ya 57, lakini zaidi ya hapo mechi zilizofuata Wana Jangwani hao ama wamefungwa, au kutoa sare.
Watavunja mwiko? Kikosi cha sasa cha Yanga SC kinakabiliwa na changamoto ya kuvunja mwiko wa kutoshinda mechi Uwanja wa Jamhuri mbele ya Mtibwa Sugar kwa miaka mitano sasa

Monday 10 March 2014

MAN UNITED YATUA URENO KUSAJILI BONGE LA KIUNGO KABAJI LINALOCHEZA TIMU MOJA NA RONALDO

KLABU ya Manchester United imeanza mazungumzo na Sporting Lisbon juu ya kumsaini kiungo mkabaji William Carvalho.
Kocha wa United, David Moyes amemtambulisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 kama mchezaji muhimu zaidi katika usajili wake wa msimu ujao na tayari imewasilisha maombi ya kumsajili Sporting.

Kifaa cha uhakika: United ipo kwenye mazungumzo na Sporting Lisbon ya Ureno kwa ajili ya William Carvalho kushoto

GOR MAHIA YAPIGWA 8-2 TUNISIA NA KUAGA LIGI YA MABINGWA, AFRIKA MASHARIKI HATUNA CHETU 16 BORA

Na Vincent Opiyo, Tunis
MABINGWA wa Kenya, Gor Mahia wametolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 5-0 jana na wenyeji Esperance kwenye Uwanja wa Rades mjini Tunis katika mchezo wa marudiano, Raundi ya Kwanza.
Matoeko hayo yanafanya Gor iage kwa kipigo cha jumla cha mabao 8-2 baada ya awali kufungwa mabao 3-2 nyumbani, Nairobi, Kenya.
Heithem Jouini alifunga mabao matatu dakika za 44, 48 na 56 na Harrison Afful na Idriss Mhrisi nao walifunga dakika za 54 na 74 kukamilisha ushindi mnono wa wenyeji.

Gor Mahia na Esperance katika mechi ya kwanza Nairobi. Picha kwa hisani ya Futaa.com

Mchezo huo ilikuwa ufanyike Jumapili, lakini ukasogezwa mbele kufuatia mvua kubwa mjini Tunis siku hiyo.

BABU YANGA SC ASEMA AL AHLY HII SI LOLOTE NA HADHANI KAMA ITAVUKA HATUA IFUATAYO

Na Tarek Talaat, Alexndria
KOCHA Mkuu wa klabu ya Yanga SC ya Tanzania, Mhoalnzi Hans Van der Pluijm amesema kwamba vigogo wa Misri Al Ahly wamepoteza makali yao na si timu tisho tena ile aliyokuwa anaijua yeye, licha ya kuitoa timu yake jana kwa penalti mjini Alexandria.
“Ilivyo, Al Ahly hii si timu kali tena ambayo sote tulikuwa tunaijua na ikiwa wataendelea kucheza kama hivi katika hatua ijayo, nina uhakika watataabika,”.
“Tulikuwa karibu kuwatoa nje ya mashindano, lakini penalti ni mchezo wa bahati, na ninajivunia kiwango chetu,”alisema Pluijm baada ya mechi jana.

Hawana kitu; Hans van der Pluijm kulia akiwa na Msaidizi wake, Charles Boniface Mkwawsa

RONALDO APIGA BONGE LA BAO REAL IKIUA 3-0 LA LIGA NA KUPAA KILELENI

MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo ameipaisha kileleni mwa LIga timu ya Real Madrid baada ya kufunga bao zuri la kichwa akiruka juu kama mcheza mpira wa kikapu katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Levante usiku huu.

Ronaldo aliyefunga dakika ya 11 akiunganisha kona ya Angel Di Maria, pia alimsetia Marcelo kuifungia Real Madrid bao la pili dakika ya 49 na akamponza David Navarro kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Karabelas alifunga dakika ya 81 kuipa Real bao la tatu, hiyo ikiwa mechi ya 29 wanacheza bila kufungwa. Real sasa inatimiza pointi 67 baada ya kucheza mechi 27 na kutulia kileleni, ikifuatiwa na Atletico Madrid pointi 64 baada ya mechi 27, wakati mabingwa watetezi, Barcelona ni ya tatu kwa pointi zake 63 baada ya kucheza mechi 27 pia.

Anatisha kijana: Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid dhidi ya Levante

YANGA SC YAFA KIUME MISRI, YATOLEWA KWA PENALTI 4-3, DIDA ALIOKOA MBILI, OSCAR, BAHANUZI NA TWITE WAKAKOSA... Home » Unlabelled » YANGA SC YAFA KIUME MISRI, YATOLEWA KWA PENALTI 4-3, DIDA ALIOKOA MBILI, OSCAR, BAHANUZI NA TWITE WAKAKOSA...

Na Salum Esry, Alexandria
YANGA SC imetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya jumla ya kufungana bao 1-1 na Al Ahly katika mechi mbili za Dar es Salaam na Alexandria.
Yanga SC iliyoshinda 1-0 wiki iliyopita Dar es Salaam, leo imefungwa 1-0 baada ya dakika 90 kwenye mchezo wa marudiano Uwanja wa Border Guard mjini Alexandria.
Kipa Deo Munishi ‘Dida’ alipangua penalti mbili mfululizo ya nne na ya tano zilizopigwa na Saed Mowaeb na Hossan Ashour, wakati za Abdalllah Said, Gedo, Mahmoud Trezeguet na Mohamed Nagieb zilimpita, lakini Yanga SC nao wakakosa penalti mbili mfululizo ya nne na ya tano.


Yanga na Al Ahly wakimenyana leo Cairo

Oscar Joshua alipiga penalti nzuri ikaguswa na kipa Sherif Ekramy Ahmed na kugonga mwamba na kurudi uwanjani, wakati Said Bahanuzi akapiga nje upande wa kushoto wa lango.
Sherif Ekramy Ahmed alipangua penalti ya mwisho ya Yanga SC iliyopigwa na Mbuyu Twite na kuwavusha Hatua ya 16 Bora mabingwa hao wa Afrika.
Waliofunga penalti za Yanga SC ni Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Didier Kavumbangu na Emmanuel Okwi.
Hadi mapumziko hakuna timu iliyofanikiwa kupata bao, Yanga SC wakicheza mchezo wa kujihami na mashambulizi ya kushitukiza.
Mrisho Ngassa alicheza vyema katika safu ya kiungo mchezeshaji akiwapa pasi nzuri washambuliaji Emmanuel Okwi, Simon Msuva, Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza.
Kiungo mkabaji Frank Domayo alishirikiana vizuri na mabeki wa kati Kevin Yondan na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wakati mabeki wa pembeni Mbuyu Twite kulia na Oscar Joshua kushoto walifanya kazi nzuri ya kuzuia na kusaidia mashambulizi.

Sunday 9 March 2014

ARSENAL YAIGONGA EVERTON 4-1


Olivier Giroud na Mesut Ozil wakishangilia bao la nne kwa Arsenal dhidi ya Everton katika dakika ya 85. Bao hilo limefungwa na Giroud.

MANCHESTER CITY YATUPWA NJE KOMBE LA FA



wachezaji wa timu ya Wigani wakimpongeza Jodri Gomez baada ya kupachika goli kwa njia ya mkwaju wa penati.