Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 12 October 2013

MH. Temba apata mtoto wa kiume


Kutoka TMK, msanii ambaye aliwahi kuwa mchezaji basketball hadi kupewa nafasi ya kujiunga na jeshi kutokana na kucheza mchezo huo lakini lishindikana kutokana na kuwa na tatoo. Habari nzuri ni kwamba Temba amepata mtoto mwingine na kufanya idadi ya watoto wake kuwa wawili. Mtoto huyo wa kiume amepewa jina laMelyvin ambaye pia dada yake anaitwa Mishell
Mtoto Melyvin

Mishell Temba

IVORY COAST YAICHARAZA SENEGAL BAKORA 3-1 NA KUBISHA HODI KOMBE LA DUNIA

WASHAMBULIAJI Didier Drogba, Salomon Kalou na Gervinho wote wamefunga jana Ivory Coast ikiifumua 3-1 Senegal na kuongeza matumaini ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia mwakani.Drogba alifunga kwa penalti dakika ya tano, kabla ya winga wa zamani wa Arsenal, Gervinho kufunga la pili dakika tisa na baadaye kipindi cha pili Salomon Kalou akafunga la tatu mjini Abidjan.



Tembo wauwaji: Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia ushindi wao leo

Sasa Ivory Coast watahitaji sare au kufungwa si zaidi ya wastani wa bao moja katika mchezo wa marudiano moja ili kujikatia tiketi ya Brazil mwakani. Seneal yenyewe itahitaji kushinda 2-0 tu nyumbani, ili kujihakikishia kurejea Fainali za Kombe la Dunia.(P.T)




Didier Drogba ameifungia Ivory Coast leo

YANGA YAUA , SHUJAA NGASSA NA KIIZA, SIMBA SC YAENDELEA KUNG'ARA KILELENI

YANGA SC imeshinda mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ugenini msimu huu baada ya kuilaza Kagera Sugar mabao 2-1 Uwanja wa Kaitaba, Bukoba jioni hii, wakati watani wao wa jadi, Simba SC pia wameshinda 1-0 dhidi ya Prisons Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Jonas Mkude

Uwanja wa Taifa, bao pekee la Simba SC limefungwa na Jonas Mkude dakika ya 62, wakati Uwanja wa Kaitaba, mabao ya Yanga yamefungwa na Mrisho Ngassa dakika ya kwanza na Hamisi Kiiza 57, wakati la Kagera limefungwa na Godfrey Wambura dakika ya 47. Coasal Union na Ashanti zimetoka 1-1 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. 

NI WAKATI WA UKOMBOZI KWA BARA LA AFIKA,HOTU HIYO KUTOLEWA NA MWANAHARAKATI OSCAR SAMBA.

ZALI KWA WAANDISHI WA HABAI ZA MICHEZO, KWENDA BRAZIL KURIPOTI KOMBE LA DUNIA


WE NI MWANDISHI WA HABARI NA UNGEPENDA KWENDA BRAZIL KURIPOTI KOMBE LA DUNIA - MAOMBI YATAANZA KUPOKELEWA DESEMBA 7


VITAMBULISHO KURIPOTI KOMBE LA DUNIA
Maombi ya vitambulisho kwa waandishi wa habari (Accreditation) wanaotaka kuripoti Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil kwa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) yataanza kupokelewa kwa mtandao Desemba 7 mwaka huu kupitia akaunti ya FIFA Media Channel.

Baada ya tuhuma za madawa ya kulevya Masogange apigwa faini ya Sh5milioni, aachiwa huru


Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini (hawk) Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya bali kemikali aina ya ephedrine.
WATANZANIA wawili Agness Gerard ‘Masogange’ na Melissa Edward wameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg baada ya kutakiwa kulipa faini ya Sh 4.8 milioni (Randi 30,000) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumiwa kutengeneza dawa za kulevya.

Refa wa Fifa kuchezesha Simba, Yanga



Mwamuzi Israel Nkongo akitolewa uwanjani na polisi wa kikosi cha FFU mara baada ya kutokea vurugu mwaka jana.Picha na Maktaba

MWAMUZI Israel Nkongo wa Dar es Salaam amepangwa kuchezesha mechi ya Simba na Yanga itakayofanyika katika Uwanja wa Taifa, Oktoba 20.

Nkongo, ambaye ni mwamuzi mwenye beji ya Fifa, alipigwa na wachezaji wa Yanga wakiongozwa na Stephano Mwasyika na Nadir Haroub ‘Cannavaro’, katika mechi ambayo Azam walishinda 3-1 wakati timu hizo zilipokutana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Machi 10 mwaka jana.

Taarifa kuhusu ishu ya Henry Joseph wa Simba


Imefahamika kwamba kiungo mkongwe wa Simba Henry Joseph ataendelea kubaki kwenye timu B na huo ni uamuzi wa benchi la ufundi la timu hiyo.
Kocha Msaidizi wa Simba Jamhuri Kihwelo anasema Henry atabaki hapo hadi atakapobadilika ‘anatakiwa kubadilika na kuonyesha juhudi kwamba alikuwa anacheza nje basi atuonyeshe kweli anastahili kuwa katika timu ya kwanza na atatoa msaada’

BOATENG HATAWAKILISHA GHANA,KUMASI

Mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya taifa ya Ghana, Kevin-Prince Boateng atakosa mechi ya mkondo wa kwanza ya kujitafutia nafasi kwenye dimba la kombe la dunia dhidi ya Misri, kutokana na jeraha la goti.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, alipata jeraha hilo wakati wa mechi ya klabu yake ya Schalke ya Ujerumani kwenye mechi za ligi ya Bundesliga. 

UHOLANZI YAICHAKAZA HUNGARY 8-1, VAN PERSIE APIGA HAT TRICK, AVUNJA REKODI



MSHAMBULIAJI Robin van Persie amekuwa mfungaji bora wa kihistoria wa Uholanzi kufutaia kufunga mabao matatu peke yake (hat trick) usiku huu katika ushindi wa 8-1 dhidi ya Hungary.
Mshambuliaji huyo wa Manchester United aliingia katika mchezo huo wa kufuzu Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil, akiwa ana mabao 38 katika mechi 78 za Orange, na wenyeji hawakuwa na presha kwa kuwa walikwishajihakikishia tiketi ya Brazil Septemba mwakani.

Matumaini ya England kukata tiketi ya kushiriki kombe la dunia 2014 yaongezeka


Wayne Rooney akishangilia baada ya kupachika bao la kwanzahttp://www.dailymail.co.uk
Na Flora Martin Mwano

Timu ya soka ya Uingereza na imeongeza matumaini ya kufuzu katika Kombe la Dunia baada ya kuifunga Montenegro mabao 4-1 katika mechi iliyopigwa usiku wa kuamkia leo.

Mabao ya Uingereza yamepachikwa na Wayne Rooney dakika ya 48, Branko Boskovic dakika ya 62, Andros Townsend dakika ya 78 na Daniel Sturridge katika dakika ya 90 kwa mkwaju wa penati.

Thursday 10 October 2013

Tazama tatoo mpya ya Rihanna na video yake akisikilizia maumivu wakati wa kuchora



Badgalriri kama anavyojiita kwenye Instagram, hivi karibuni amechora tatoo mpya kwenye mkono wake. Rihanna alichora tatoo hiyo ya asili ya huko New Zealand alipoenda kufanya show, unaambiwa style uchoraji wa tatoo hii unaleta maumivu makali zaidi ya tatoo za kawaida.Angalia hii video uone jinsi Rihanna alivyokuwa anasilizia maumivu ya kuchorwa hiyo tatoo.

BARTON : FERGUSON ALIKUWA HANA UWEZO WA KUPANGA HATA KONI




Kiungo mtukutu wa Queens Park Rangers Joey Bartonameibuka tena kwenye vichwa vya vyombo vya habari baada ya kudai kocha wa zamani wa Manchester Utd Sir Alex Ferguso hakuwa na uwezo wa kufundisha,
Barton alidai nchini England mameneja wanathaminiwa sana kuliko makocha.
'Sina maana ya kutomuheshimu Sir Alex Ferguson - alikuwa meneja mkubwa lakini hakuwa na uwezo wa kufundisha,

Baada ya kukutana na picha yake hotelini hiki ndicho alichokifanya Diamond


Diamond Platnamz ambae yuko Hongkon kwa sasa, ameamua kutia saini kwenye moja ya picha yake aliyokuta imebandikwa katika ukuta wa hoteli moja ya ki-africa,

Nakaaya Sumari ajifungua mtoto wa kiume, na hii ndio picha aliyoionyesha


Msanii wa hit ya "Mr Politician" Nakaaya Sumari, amepata mtoto wa kiume aliejifungua Oct 5,na amempa jinaKai Samwel kwasababu anaamini kuwa ni mtoto huyo ni mfalme kwake. Nakaaya ameamua kuonyesha picha ya mtoto huyo lakini ikionyesha sehem za miguu pekaa.




"On the 5th of Oct. God blessed me with a son. I named him Kai Samuel. For he is King. I too get to be called a mother. Its the best feeling in the world... a love i cant explain. May our father in heaven sheild you my son. And may you serve him all of your days. In Jesus name". ameandika Nakaaya kupitia ukurasa wake wa facebookwww.hakileo.blogspot.com

Mwigizaji Lulu aamua kujichora tatto baada ya watu kumhukum na kuwataka kumuachia Mungu jukumu hilo


Msanii wa Bongo Movie Tanzania, Elizabeth Michael "Lulu" ameamua kuchora tattoo iliyoandikwa "Only God Can Judge Me" chini yashingo upande wa bega lake la kushoto, baada ua kuona watu wamekuwa wakimhukum kwa mambo ayafanyao kulliko Mungu ambae ndie mwenye cheo chake, na kuwataka watu kumuachia jukumu hilo Mungu pekee, na kucha kujipa u-busy usio wa lazima

LADY JAYD ATOA SOMO,JINSI YA KUUTUNZA MWILI KUPUNGUZA TUMBO NA KUPUNGUZA MAFUTA.........KUNAHITAJI VITU VINGI TOFAUTI NA VYA ZIADA ILI KUPATA SHAPE UNAYOIPENDA

Kutokana na maombi niliopokea kwa njia ya mails nyingi kutoka kwa wadau, baada ya kukata tumbo kwa wiki mbili, waliuliza ni diet gani nimetumia ili kufanikisha zoezi hilo.

Jibu langu ni hili:

Hii sio ya kitaalamu bali ni mimi ninavyofanya na ndio inayonisaidia kupunguza tumbo.
Kwasababu vitu vya formula mimi huwa siwezi kuvifuata na huwa naviona vigumu sana kwahiyo huwa najaribu kuishi vile ninavyoweza.

Na kizuri zaidi ni kwamba hii sio diet ya kujinyima.
Ila unaweza usifanikiwe pia kutokana na mwili wako kwakua tumeumbwa tofauti lakini unaweza kujaribu kama itafanya kazi

Tukianza na asubuhi nikiamka mimi kama Binti Machozi, naanza kunywa maji glass 3 kabla ya kupiga mswakwi.
Na nikiisha amka nakunywa maji ya uvugu vugu yaliokamuliwa ndimu au limao glass zingine tatu kabla ya kunywa Chai.
Ukizoea maji ni matamu kuliko hata biere
Kuwa Teja wa Maji kuna raha yake pia

ROONEY;BADO NINAHITAJI KUCHEZA NAFASI YA USHAMBULIAJI



Mshambuliaji wa man U, Wyne Rooney

Mshambuliaji wa manchester United Wyne Rooney amezidi kusisitiza anahitaji kucheza nafasi ya mshambiliaji wa kuongoza mashambulizi katika timu hiyo ya mashetani wekundi yeynye maskani yake jijini manchester.akizungumza na waandishi wa habari rooney amesama,,

YANGA YAJIFUA NTUNGAMO



Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Young Africas leo jioni wamefanya mazoezi katika viwanja vya shule ya seminari ya wakatoriki Ntungamo - Kashura pembeni kidogo ya mji wa Bukoba kujiandaa na mchezo wa siku ya jumamosi dhidi ya wenyeji Kagera Sugar katika uwanj wa Kaitaba. Kelvin Yondani aliyeripotiwa na chombo kimoja cha habari kwamba ameondolewa kwenye timu taarifa hizo hazina ukweli kwani mlinzi huyo kisiki wa kati ni miongoni mwa wachezaji waliofanya mazoezi jioni ya leo pamoja na kikosi cha Yanga.

Young Africans ambayo iliwasili katika mji wa Bukoba majira ya saa 5 asubhi ikitokea jijini Dar es salaam ambapo ilipitia jijini Mwanza kabla ya kutua kwenye mji huu ambao una mandhari mazuri na hali ya hewa safi.

NI RAHA TUPU, SASA P-SQUARE KUTUA BONGO NOV- 23-2013‏


Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa wasanii wa Muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – square kutoka nchini Nigeria chini ya udhamini wa Vodacom, watakaowasili Tarehe 23 Mwezi ujao. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. Pamoja nae katika picha ni Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela).
Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa wasanii wa muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama P – Square kutoka nchini Nigeria pamoja na mdhamini Mkuu,Tarehe 23 Mwezi ujao ndipo watawasili nchini. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. Pamoja nae katika Picha ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa ambo ndio wadhamini wa onesho hilo.

DIAMOND na WEMA SEPETU waigiza move moja inaitwa "TEMPTATIONS", Pia Diamond amfariji "I REAL LOVE MY PENNY,SIJARUDIANA NA WEMA"


Leo ilikuwa kama gumzo katika account ya Instagram baada ya kuonekana picha hizi Diamond akiwa na Wema Sepetu pande za China.

WAJUE wachezaji watano kutoka Afrika watanaocheza ligi ya NBA



Hasheem Thabeet (Tanzania)

Ndio mchezaji mrefu kuliko wote kwenye ligi ya NBA kwa sasa, majuzi wakati timu yake ya Oklahoma City Thunder ikicheza na Charlotte Bobcats Hasheem alicheza vizuri akiwa na point 13 alizofunga pamoja na kudaka Rebounds 10, huu utakua msimu wake wa pili akiwa na OKC.

Lenox Lewis kurudi ulingoni?




Bondia Muingereza Lenox Lewis huenda akareja ulingoni miaka kadhaa baada ya kustaafu mchezo huo .

Lennox ambaye mara ya mwisho alistaafu akiwa bingwa asiyepingwa wa masumbwi ya uzito wa juu ameshawishiwa kurudi ulingoni na mapromota toka Urusi ambao wanataka kuandaa pambano baina yake na Vittali Klitschko .

Mapromota wa Bondia wa Ukraine Vitali Klitschko ambaye pia ni mwanasiasa wanataka Lenox Lewis arudiane na Klitschko baada ya kumshinda wakati walipopambana mwaka 2003.


Hii ilikuwa mwaka 2003 wakati Lenox Lewis alipomchapa Vitali Klitschko kwa Knock Out .
Hata hivyo Lennox amesema kuwa anataka kupambana na mdogo wa Vitali ambaye ni Wladmir Klitschko lakini atakubali kurudi ulingoni endapo atahakikishiwa malipo ya dola milioni 100 .

Ebwana hii ndio stori nzima kuhusu hii vita ya maneno Twitter kati ya Jack Wilshere na Kevin Pietersen




Kiungo wa Arsenal na timu ya taifa ya England Jack Wilshere amepinga wazo la kutoa uraia kwa wachezaji wasio na asili ya England na kutoa fursa ya kuichezea timu ya taifa ya England .

Wilshere alizungumza hayo wakati anajibu maswali ya waandishi wa habari juu ya mawazo ya kocha wa England Roy Hodgson ambaye amevutiwa na kipaji cha kiungo wa Manchester United Adnan Januzaj hadi ya kufikiria kumshawishi aichezee England .

CHICHARITO ATAJA SABABU KWA NINI ATAONDOKA MAN U



MSHAMBULIAJI Javier Hernandez amesema anaweza kuondoka Manchester United ili kusaka timu ambayo atapata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza.
Mshambuliaji huyo anayefahamika kama Chicharito hapewi nafasi kubwa katika klabu ingawa mwezi uliopita aliifungia timu hiyo bao la ushindi katika Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One dhidi ya Liverpool na zaidi ya mechi hiyo alianza katika mechi nyingine moja tu, United ikifungwa nyumbani na West Brom.

Eto'o akubali kuichezea Cameroon baada ya rais Biya kuingilia kati



Samuel Eto'o
Rais wa Cameroon Paul Biya amemsihi mshambulizi wa timu ya taifa ya soka Samuel Eto'o kutostaafu kucheza soka la Kimataifa.
Mshambulizi huyo wa Chelsea amekutana na wawakilishi wa rais Biya jijini Yaounde kujadiliana kuhusu hatima ya Eto'o ambaye tayari alikuwa ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa.

Wednesday 9 October 2013

IFAHAMU DAMU YA KIARABU,YENYE URAIA WA UJERUMANI,ILIYOKULIA HISPANIA NA KWENDA LONDON


Kiungo wa Arsenal,Mesut Ozil

NYOTA aliyesajiliwa kwa gharama kubwa msimu huu katika kikosi cha Arsenal ni Mesut Ozil. Nyota huyu tayari amethibitisha ubora wake kwa kuonyesha uwezo wa kujitambua, kutuliza na kutoa pasi sahihi, pia ana uwezo wa kucheza kitimu.

Ozil ambaye ni raia wa Ujerumani mwenye asili ya Uturuki alisajiliwa na Arsenal msimu huu kwa Pauni 42.5 milioni akitokea klabu ya Real Madrid na kusaini mkataba wa kuitumikia Arsenal kwa miaka mitano.
Baada ya kusaini mkataba huo, Ozil alipohojiwa na vyombo vya habari alisema: “Ni kweli nilitaka kubaki Real Madrid, lakini baadaye niligundua kwamba kocha au benchi la ufundi halina imani na mimi. Mimi ni mchezaji ninayependa kuaminika, ndiyo maana nimehama Madrid na kujiunga na Arsenal ambayo inaonyesha itaniamini.”

MZEE YUSUPH ALITAWALA JUKWAA DAR LIVE.



Kiongozi wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf akiwapagawisha mashabiki.

Mzee Yusuf na Khadija Yusuf wakiwapa raha mashabiki.

MREMBO SALOME AMWANDALIA MNUSO OMMY DIMPOZ JIJINI MARYLAND, MAREKANI


Mrembo Salome Frederick akiwa na mgeni wake Omary Nyembo 'Ommy Dimpoz' nyumbani kwake Maryland nchini Marekani wakati wa mnuso aliomwandalia.

Baadhi ya waalikwa akiwemo Promota "DMK" katika picha ya pamoja wakati wa chakula nyumbani kwa Salome Frederick jijini Maryland. Salome alimwalika Dimpoz pamoja na baadhi ya marafiki zake kwa chakula cha jioni kilichoandaliwa nyumbani kwake.

Tuesday 8 October 2013

Diamond amchamba alievujisha wimbo wake wa ‘nikifa kesho’,SASA ANACHAMBUA SHERIA.


‘Kuvujisha Nyimbo yangu hakuwezi kunipunguzia wala Kunidhuru chochote… Sanasana utanizidishia Umaarufu na kunipa Show zaidi… Kama nimeacha kurecord nyimbo Studio kwako Uspanick, Relax.. tafta Msanii mwingine Mkali zaidi yangu umrecordie Ngoma Ahit kushinda mimi… .ila Kuvujisha Unajisumbua bure’ – Diamond

‘Hisia zangu zapelekea kuandika haya nikiwa na uzuni ndani yake kwa kuwa muda nilioutmia na akili nliotumia dhairi ni Mungu Pekee anajua ndio Maana aina budi namwachia Mungu pia….Imani iliyo ndani yangu nikiamini kuwa kutoa ya Moyoni uufanya Moyo kujengeka Upya, Mwenyezi Mungu Atanijenga Upya na kuwaandalia kitu kipya hivI karibuni’ – Diamond

TP MAZEMBE YAPAA , YAINYUKA 2-1 STADE MALIEN NUSU FAINALI AFRIKA



MABAO ya Rainford Kalaba na Tresor Mputu yameipa TP Mazembe ushindi wa 2-1 ugenini katika Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji Stade Malien mjini Bamako, Mali.
Morikaman Koita alifunga bao pekee la wenyeji katika mchezo huo, wakati Mazembe ilipata bao la kuongoza mapema dakika ya 14 kupitia kwa Mzambia, Rainford Kalaba.

RAISI WA CAMEROON AMSHAWISHI ETO'O KUTOSTAAFU SOKA LA KIMATAIFA



Rais wa Cameroon Paul Biya amemshawishi mwanasoka Samuel Eto'o kutafakari upya mipango yake ya kujizulu kutoka soka ya kimataifa.
Mshambulizi huyo wa Chelsea alikutana na waakilishi wa Rais mjini Yaounde kujadili mustakabali wa mchezaji huyo kuhusu soka ya kimataifa.

Sasa atakwenda Ufaransa kujiunga na timu ya taifa inayojiandaa kucheza dhidi ya Tunisia katika michuano ya kufuzu kwa kombe la Dunia Brazil mwaka 2014. Baada ya kukutana na Eto'o, alikubali kuchezea Cameroon kwa mara nyingine.

BARCA WATAKA KUMNG'OA JANUZAJ MAN U



Januzaj akivinjari mitaa ya Manchester


KLABU ya Barcelona iko tayari kumchukua Adnan Januzaj kutoka Manchester United iwapo atakataa ofa ya kuongeza Mkataba.

Kinda huyo mwenye umri wa miaka 18, amejipatia umaarufu mkubwa baada ya kufunga mabao mawili katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Sunderland Jumamosi.

Lakini Barca imekuwa ikifuatilia kipaji cha mwanasoka huyo tangu hajajiunga na United kutoka Anderlecht mwaka 2011. Barca wanaamini sana kwamba Januzaj atahamia tu Nou Camp wakati atakapomalizia miezi minane iliyobaki katika Mkataba wake.

Gus Poyet ateuliwa kuwa kocha mpya wa klabu ya Sunderland huko England


Kocha mpya wa Sunderland
Gus Poyet ameteuliwa kuwa Kocha mpya ya klabu ya soka ya Sunderland inayoshiriki katika ligi kuu ya soka nchini Uingereza.
Poyet ambaye pia amewahi kuwa Kocha wa klabu ya Brighton ya Uingereza inayoshiriki katika daraja la kwanza atakuwa Mkufunzi wa Sunderland kwa miaka miwili kwa mujibu wa mkataba aliotia saini.

Monday 7 October 2013

KARIBU TABASAMU PRODUCTION.

Kwa huduma za kupiga picha za VIDEO na MNATO  pia KUHARIRI MIKANDA YA VIDEO  ,tuna kukaribisha TABASAMU PRODUCTION karibu sasa kwani huduma zetu ni nafuu kabisa.  Tunapatika na kwa MOROMBO  mkoano Arusha katika majengo ya chuo cha ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLLEGE.
WASILIANA NASI KWA SIMU namba 0759859287 AU barua pepe ifwatayo ; tabasamuleo@gmail.com.
KWA MAELEZO ZAIDI TAZAMA VIDEO HII.

HATIMAE UCHAGUZI TFF K UFANYIKA OKTOBA 27- TENGA ANENA.



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewahakikishia Watanzania kuwa uchaguzi wa kupata Kamati mpya ya Utendaji ya shirikisho utafanyika Oktoba 27 mwaka huu kama ilivyopangwa.
"Wazungu wanasema ije mvua au jua, uchaguzi utafanyika. Isipokuwa tunachotaka kuhakikisha ni kuwa unakuwa uchaguzi huru na wa haki," amesema Rais Tenga wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF leo mchana (Oktoba 7 mwaka huu).

Nusu fainali ya Michuano ya Klabu bingwa na shirikisho barani Afrika kusakatwa jumapili


Michuano ya nusu fainali ya kwanza kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika na shirikisho zinachezwa mwishoni mwa juma hili.
rfikiswahili
Michuano ya nusu fainali ya kwanza kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika na shirikisho zinachezwa mwishoni mwa juma hili.
Orlamndo Pirates ya Afrika Kusini wakiwa nyumbani jana Jumamosi walitoka sare ya kutofunga na mabingwa wa mwaka wa 2011 Esperence ya Tunisia.

Kocha wa Zambia Herve Renard aruhusiwa kuondoka,sasa kurejea Ufaransa



Herve Renard
Shirikisho la soka nchini Zambia FAZ limetangaza kuwa limempa nafasi ya kuondoka kocha wa timu ya taifa ya Chipolopolo Mfaransa Herve Renard.

Renard alianza kuifunza Zambia mwaka 2008 na akaondoka mwaka 2010 kabla ya kurejeshwa tena mwaka 2011 na kuiongoza Chipolopolo kunyakua taji la klabu bingwa barani Afrika mwaka 2012 nchini Gabon.

Picha za matembezi ya Ommy Dimpoz pamoja na show aliyofanya huko Hollywood






Omari Nyembo famous as Ommy Dimpoz hivi sasa bado yupo Marekani kwenye kwa ajili ya show zake. Ommy Dimpoz akiwa huk Marekani ametembelea sahemu mbalimbali huko Hollywood, hizi ni picha akiwa huko pamoja na show yake