Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Monday 12 May 2014


           KWA HABARI ZA MICHEZO,KITAIFA NA KIMATAIFA BONYEZA HAPAKWA HABARI ZA MICHEZO,KITAIFA NA KIMATAIFA BONYEZA HAPA

WWW.HAKILEO.BLOGSPOT.COM

ESSIEN NA BOATENG WAITWA KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA GHANA PIA KIFAHAMU KIKOSI CHOTE CHA GHANA

GHANA imewajumuisha Michael Essien na Kevin-Prince Boateng katika kikosi cha awali cha wachezaji 26 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.
Kikosi hicho kitapunguzwa na kubaki wachezaji 23 baada ya mchezo wa kirafiki na Uholanzi Mei 31, ambacho ndiyo watakwenda Brazil.
Essien na Boateng wameitwa baada ya kurejea kwenye soka ya kimataifa mwaka jana, kufuatia awali kuomba kujipumzisha kuichezea timu hiyo.

Kazini: Nyota wa AC Milan na mchezaji wa zamani wa Chelsea, Michael Essien ameitwa kwenye kikosi cha Ghana

Ghana ipo Kundi G pamoja na Marekani, Ujerumani na Ureno.

KIKOSI KAMILI HIKI HAPA;
Makipa: Stephen Adams (Aduana Stars), Fatau Dauda (Orlando Pirates), Adam Kwarasey (Stromsgodset)
Mabeki: Harrison Afful (Esperance), Jerry Akaminko (Eskisehirspor), John Boye (Stade Rennes), Samuel Inkoom (Platanias), Jonathan Mensah (Evian Thonon Gaillard), Daniel Opare (Standard Liege), Jeffrey Schluup (Leicester City), Rashid Sumaila (Mamelodi Sundowns)
Viungo: David Accam (Helsingborg), Afriyie Acquah (Parma), Albert Adomah (Middlesbrough), Emmanuel Agyemang Badu (Udinese), Kwadwo Asamoah (Juventus), Christian Atsu (Vitesse Arnhem), Andre Ayew (Olympique Marseille), Michael Essien (AC Milan), Rabiu Mohammed (Kuban Krasnodar), Sulley Muntari (AC Milan), Mubarak Wakaso (Rubin Kazan)
Washam uliaji: Jordan Ayew (Sochaux), Kevin Prince Boateng (Schalke 04), Asamoah Gyan (Al Ain), Abdul Majeed Waris (Valenciennes).
CHANZO BIN ZUBEIRY


WWW.HAKILEO.BLOGSPOT.COM

Saturday 10 May 2014

YANGA WATAKIWA KIGALI KABLA YA AGOSTI 9 KOMBE LA KAGAME

Na Baby Akwitende, Dar es Salaam
MASHINDANO ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu Kombe la Kagame yamepangwa kufanyika kuanzia Agosti 9 hadi 23 mwaka huu jijini Kigali nchini Rwanda.
Tanzania Bara itawakilishwa na Yanga katika mashindano hayo yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati ( CECAFA).
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana , Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, alisema timu zote wanachama wa shirikisho hilo zinatarajiwa kushiriki.

Kikosi cha Yanga SC

Musonye alisema kuwa bado sekretarieti haijateua timu mwalikwa katika mashindano hayo kutokana na mabadiliko ya kalenda ya michuano hiyo ambayo hufanyika kila mwaka kati ya mwezi Mei na Juni.
"Ratiba kamili ya mashindano hayo itatolewa baadaye", alisema Musonye.
Mlezi wa CECAFA na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ameshathibitisha kutoa zawadiambayo ni Dola za Marekani 60,000 ambazo alianza kutoa tangu mwaka 2002.
Wadhamini wengine waliothibitisha kudhamini mashindano ya mwaka huu ni kituo cha televisheni cha Super Sport.

Bingwa mtetezi wa mashindano hayo ni Atraco ya Burundi na mfungaji bora wa michuano hiyo alikuwa ni Amissi Tambwe, anayeichezea Simba akitokea kwa mabingwa hao.

Thursday 1 May 2014

TFF YATEUA WAKILI KUCHUNGUZA USAJILI WA DOMAYO AZAM FC

Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam
KUTOKANA na tukio lililotokea jana (Aprili 30 mwaka huu) kwenye kambi ya timu ya Taifa (Taifa Stars) iliyopo Tukuyu mkoani Mbeya likihusisha usajili wa baadhi ya timu, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemteua Wakili Wilson Ogunde kuchunguza mlolongo mzima wa tukio hilo.
Taarifa ya TFF kwa BIN ZUBEIRY leo asubuhi imesema kwamba, baada ya kukamilisha uchunguzi wake, Wakili Ogunde ataishauri TFF kuhusu hatua za kisheria na kikanuni za kuchukua.

Frank Domayo akisaini Azam FC jana
TFF imesema katika taarifa yake inatoa wito kwa wachezaji, klabu na wadau wa mpira wa miguu kufuata kanuni na taratibu katika utendaji wao.
Viongozi wa Azam FC jana walikwenda kwenye kambi ya Taifa Stars kukamilisha taratibu za usajili na kiungo Frank Domayo, aliyemaliza Mkataba wake Yanga SC.
Baada ya kufanikiwa kumsainisha Mkataba wa miaka miwili, wasimamizi wa kambi waliwaitia Polisi viongozi wa Azam FC ambao hata hivyo baadaye waliachiwa. Lakini inadaiwa fomu za usajili zilichanwa.
Azam si klabu ya kwanza kusajili mchezaji katika kambi ya timu ya taifa, kwani vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga ndiyo waasisi wa mchezo huo.
Mwaka jana Simba SC walisaini Mkataba mpya na kiungo wao, Amri Kiemba akiwa katika kambi ya Taifa Stars, hoteli ya Tansoma mjini Dar es Salaam.

Inaruhusiwa kwa wakubwa tu; Kiongozi wa Yanga SC, Seif Ahmed 'Magari' alimtoa kambi ya Taifa Stars, beki Kevin Yondan akiwa Simba SC na kumsainisha mwaka 2012.

Yanga SC iliwasajili Domayo kutoka JKT Ruvu, Kevin Yondan kutoka Simba SC wote wakiwa katika kambi ya Taifa Stars Dar es Salaam miaka miwili iliyopita.

CHELSEA NJE ULAYA, YAPIGWA 3-1 DARAJANI...FAINALI NI ATLETICO NA REAL MADRID

CHELSEA imeaga Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kufungwa mabao 3-1 na Atletico Madrid ya Hispania usiku huu Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Atletico sasa itakutana na jirani zao, Real Madrid katika fainali mwezi ujao nchini Ureno, ambao jana waliwang’oa mabingwa watetezi, Bayern Munich kwa 4-0 mjini Munich na kufanya ushindi wa jumla wa 5-0.

Heshima sasa; Diego Costa kushoto akishangilia na mchezaji mwenzake, Koke baada ya kufunga bao la pili



Fernando Torres alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya 36 kwa pasi ya Azpilicueta baada ya kazi nzuri ya Willian, lakini Adrian Lopez akaisawazishia Atletico dakika ya 44 kwa pasi ya Juanfran.
Diego Costa akafunga bao la pili kwa penalti dakika ya 61 kabla ya Arda Turan kumaliza kazi dakika ya 72 na Atletico imefuzu kwa ushindi wa jumla wa 3-1 baada ya sare ya 0-0 katika mchezo wa kwanza Madrid wiki iliyopita.
Mabadiliko yaliyofanywa na kocha Jose Mourinho dakika ya 54 kumtoa beki Ashley Cole na kumuingiza mshambuliaji Samuel Eto’o ndiyo yaliigharimu Chelsea. Eto’o ndiye aliyesababisha penalti iliyofungwa na Costa.

Wednesday 30 April 2014

MAYWEATHER AONYESHA JEURI YA FEDHA, SASA ATAKA KUNUNUA TIMU MAREKANI

KAMA anavyotamba katika ngumi za kulipwa hadi sasa akiwa hajapoteza pambano licha ya kupigana na mabondia wakali duniani, Floyd Mayweather anataka kununua klabu ya mpira wa kikapu Marekani, inayomilikiwa na milionea anayekabiliwa na kashfa ya ubaguzi.
Hakuna ajabu kwa mkali huyo wa kutupa mikono kwenye miili ya wenzake, anayekwenda kwa jina la utani Money Mayweather juu ya hilo, kwa sababu ana uwezo kifedha.
Floyd Jnr anataka kutoa dola za Kimarekani Milioni 40 ambazo ni sehemu tu ya pato lake la pambano la Jumamosi wiki hii, atakalolipwa dola bilioni 1.8 ili kuinunua Los Angeles Clippers.
Mutu ya fweza: Floyd Mayweather akiwasili ukumbi wa MGM Grand kuelekea pambano lake na Marcos Maidana

Kuhusu Marcos Maidana, Muargentina anayetarajiwa kupambana naye mjini Las Vegas, Mayweather amesema: "Amekuwa babu kubwa katika mapambano yake manne yaliyopita. Ana wastani wa asilimia 80 ya Knockout (KO). Hivyo siwezi kumdharau huyu jamaa,".
Kuhusu Clippers, ambayo mmiliki wake Donald Sterling amefungiwa maisha kujihusisha na masuala ya mpira wa kikapu baada ya kupatikana na hatia ya kuwatolea maneno ya kibaguzi watu weusi wa timu yake wakiwemo wachezaji, Mayweather amesema: "Ninataka kuinunua Clippers? Ndiyo. Naweza kuwaunganisha pamoja watu ambao watakuwa tayari.
"Kununua timu ya Ligi Kuu ya kikapu ni kitu fulani ambacho nataka kuongeza katika kampuni yetu inayokua kwa kasi ya Mayweather Promotions, ambayo sasa si kwa ajili ya ngumi tu, bali tunajihusisha pia na mavazi, muziki na sinema,"alisema.


Kifungo cha maisha: Mmiliki wa Los Angeles Clippers, Donald Sterling hawezi kujihusisha na masuala ya mpira wa kikapu baada ya kutoa kauli ya kibaguzi hadharani

KATIBU MKUU WA FIFA AWASILI KESHO DAR

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Jerome Valcke anawasili nchini kesho (Mei 1 mwaka huu) ambapo atafungua semina ya mawasiliano kwa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).

Valcke ambaye atafuatana na maofisa wengine saba wa FIFA baadaye kesho hiyo hiyo (Mei 1 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi kwenye hoteli ya Double Tree by Hilton iliyopo Oysterbay, Dar es Salaam.

Sunday 27 April 2014

MADOGO WA NGORONGORO WALIVYOWATOA WAKENYA JANA NA KUJIWEKA KWA NIGERIA


Kiungo wa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes, Mudathir Yahya akimtoka kiungo wa Kenya katika mchezo wa jana kuwania tiketi ya Fainali za Afrika nchini Senegal mwakani. Tanzania iliitoa Kenya kwa penalti 4-3 baada ya sare ya jumla ya 0-0. Ngorongoro sasa itamenyana na Nigeria katika hatua inayofuata.


Kevin Friday wa Tanzania akimuacha chini beki wa Kenya

Wachezaji wa Tanzania wakishangilia baada ya mechi


Ally Bilal wa Tanzania akimtoka Hillary Dan wa Kenya


Mange Chagula wa Tanzania kushoto akigombea mpira na Hillary Dan wa Kenya aliye tayari kusaidiwa na wenzake


Kipa wa Kenya, Farouk Shikhalo akidaka mpira huku akilindwa na beki wake, Hillary Dan aliye mbele ya Ally Bilal wa Tanzania

Kevin Friday wa Tanzania kulia akimtoka Victor Ndinya wa Kenya

Mange Chagula wa Tanzania akiteleza na mpira mbele ya Evans Makari wa Kenya

Iddi Suleiman wa Tanzania akiwatoka mabeki wa Kenya

Iddi Suleiman wa Tanzania akimuacha chini beki wa Kenya

Benchi la Ufundi la Tanzania wakati wa penalti jana

Thursday 24 April 2014

REAL MADRID NA BAYERN MUNICH KATIKA PICHA JANA BERNABEU


Juu kwa juu: Cristiano Ronaldo (katikati) akiwa ameruka juu zaidi ya Alaba (wa pili kushoto) na Dante kuwania mpira wa juu katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana Uwanja wa Bernabeu mjini Madrid, Hispania. Real ilishinda 1-0.
Franck Ribery wa Bayern Munich (kushoto) akimfukuzia Daniel Carvajal wa Real
Mfungaji wa bao pekee la Real, Karim Benzema akishangilia baada ya kufunga Uwanja wa Santiago Bernabeu
Kula gwala, kamalizie kazi: Ronaldo akimpisha Gareth Bale dakika ya 74
Philipp Lahm na Gareth Bale (kulia wakigombea mpira wa juu
Beki Mbrazil wa Bayern, Dante (kushoto) akipitia mpira miguuni mwa Angel di Maria wa Real
Thomas Muller (katikati) wa Bayern akililia penalti
Beki wa Real Madrid, Sergio Ramos (kushoto) akiosha mbele ya mshambuliaji wa Bayern, Bastian Schweinsteiger
Schweinsteiger akimdhibiti kiungo wa Real Madrid, Xabi Alonso (katikati)
Mabeki wa Real, Pepe (kushoto) na Sergio Ramos (katikati) wakienda hewani kuondosha hatarini mpira wa juu kutoka kwa Ribery



Kipa wa Real, Iker Casillas (kulia) akiokoa mpira kichwani kwa Javier Martinez
Cristiano Ronaldo akimtoka Jerome Boateng

TARIMBA: NINA DHAMIRA YA KURUDI KUONGOZA YANGA SC

Na Amran Muhina, Dar es Salaam
RAIS wa zamani wa klabu ya Yanga SC ya Dar es Salaam, Tarimba Abbas amesema kwamba ana dhamira ya kurudi kuiongoza klabu hiyo, katika uchaguzi ujao uliopangwa kufanyika Juni 15, mwaka huu.
Tarimba ameiambia BIN ZUBEIRY jana kwamba, kwa sasa bado mapema mno kuzungumzia jambo hilo ingawa kama mwana-Yanga ana haki yake kikatiba.
“Ni mapema mno kusema nitagombea, maana uchaguzi ni mpaka Juni ni kipindi kirefu sana, lakini kama mwana-Yanga dhamira ninayo ingawa inaweza isiwe sasa, ila ninachoweza kusema ni mapema mno kuzungumzia jambo hilo,” alisema Tarimba.


Tarimba kulia akizungumzia pembeni ya Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom, Kevin Twissa

Tarimba ambaye kwa sasa ni kada wa CCM, Diwani wa Kata ya na Mkurugenzi wa Tume ya Michezo ya Kubahatisha ni kati ya watu ambao wana Yanga SC wanawataka sana waingie kuongoza klabu hiyo pamoja na Davis Mosha.
Angu Shadrack na wanachama wenzake vijana wa Kariakoo wanajipanga kumfuata Davis Mosha kumshawishi achukue fomu za kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti, wakati Tarimba Abbas wanataka awania Uenyekiti wa klabu hiyo.
“Tunajipanga kuwafuata Mosha na Tarimba kuwaomba wagombee, hawa viongozi wetu wa sasa wametuangusha sana, tunataka watu ambao hatutawajaribu, tunajua ni watu wa kazi na wana mapenzi na Yanga,”alisema Angu.
Gazeti la Spoti Leo la leo nalo limewanukuu wanachama wa Yanga wakisema wanaamini Tarimba anastahili kuvaa viatu vya Manji kutokana na uwezo mkubwa aliouonyesha wakati akiwa Rais wa Yanga mwanzoni mwa miaka ya 2000.
“Tumeshakaa mara kadhaa wana-Yanga kujadili nani anafaa kuongoza baada ya Manji kumaliza muda wake, lakini wengi mawazo yetu yameangukia kwa Tarimba. Tunaamini ni kiongozi mzuri na anaweza kuipeleka Yanga pazuri,” alisema Juma Mohammed ‘Kamanda’ aliyejitambulisha anatoka Yanga Bomba.
Naye mwanachama mwingine wa Yanga, Suleiman Mussa, alisema wameanza mikakati ya kuangalia nani atafaa kuiongoza Yanga na wanajipanga kwenda kumuona Tarimba ili kumshawishi wakati ukifika ajitose kwenye uchaguzi huo.

Wednesday 23 April 2014

DIEGO COSTA AWAPA ISHARA NZURI CHELSEA...NI DALILI ZA KUHAMIA DARAJANI

MSHAMBULIAJI wa Atletico Madrid, Diego Costa anaweza kuwa katika jaribio la kuing'oa Chelsea katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, lakini alikuwa mwenye furaha kupita kiasi wakati anawapungia mkono mashabiki wa timu hiyo baada ya mechi ya jana.
Inafahamika mshambuliaji huyo ni chaguo la kwanza la kocha Jose Mourinho katika orodha ya wachezaji anaotaka kuwasajili msimu ujao na kitendo cha kuwapungia kwa furaha mashabiki wa Chelsea jana kimezidi kuongeza dalili za kuhamia kwake London.
Chelsea ilitoka sare ya bila kufungana na Atletico Madrid Uwanja wa Vicente Calderon, inamaanisha mchezo bado upo kati kwa kati kuelekea mechi ya marudiano Jumatano ijayo.

Anawapa dalili? Diego Costa akiwapungia mkono mashabiki wa Chelsea baada ya mechi usiku wa jana

Upinzani: Mshambuliaji huyo anaweza kuja kuwa mchezaji mwenzake John Terry msimu ujao, japokuwa jana walizinguana sana uwanjani
Baada ya filimbi ya mwisho mashabiki wa Chelsea walibaki uwanjani wakati baadhi ya wachezaji wanapita mbele yao kuondoka.

REAL HATARINI KUWAKOSA GARETH BALE NA RONALDO LEO DHIDI YA BAYERN, WOTE WAGONJWA

WINGA Gareth Bale yuko shakani kuichezaea Real Madrid katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich kutokana na kusumbuliwa nugonjwa wa mafua.
Nyota huyo wa Wales hajasafiri na wenzake kwa ajili ya mchezo wa kwanza leo Uwanja wa Sangtiago Bernabeu.
Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti pia anatilia shaka uzima wa Cristano Ronaldo. Nyota huyo wa Ureno anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya muda mfupi kabla ya mchezo wa leo.

Shaka tupu: Gareth Bale anasumbuliwa na mafua kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Bayern Munich

Pigo: Madrid inaweza kumkosa Bale na Cristiano Ronaldo leo
Ikiwa Bale ataukosa mchezo wa leo, litakuwa pigo kwa Ancelotti, ambaye alimwagia sifa nyingi winga huyo katika Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo wa leo.
Bale anang'ara kwa sasa, baada ya kufunga bao la ushindi katika fainali ya Copa del Rey dhidi ya Barcelona wiki iliyopita na kocha wake akasema mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 86 kutoka Tottenham atakuwsa mkali zaidi msimu ujao Hispania ambao utakuwa wa pili kwake Real.
"Gareth ni mtoto mkali,"alisema Ancelotti. "Anavutia kwa kujiamini kiasi cha kutosha hususan kutokana na bao alilofunga dhidi ya Barcelona katika fainali,"alisema.

Friday 18 April 2014

BARCELONA SASA RADHI KUMUUZA MESSI

MSHAMBULIAJI Lionel Messi anaamini Barcelona sasa inamchukulia kama mtu wa kuuzwa na si tena nyota asiyegusika katika kikosi chao, imeripotiwa chaneli ya Televisheni ya Esport3 ya Katalunya.
Kusuasua kwa mazungumzo ya kuongeza mkatab baina ya mchezaji huyo na klabu ni kielelezo cha kwa nini Messi anafikiria muda wake umekwisha Barcelona.
Inaelezwa kwamba Wajumbe wa bodi wanaamini mchezaji huyo ana thamani zaidi ya kuuzwa kwa sasa kuliko kuendelea kuwatumikia uwanjani, jambo ambalo Messi analitambua pia na anaamini ni juu ya Barcelona kuhusu Mkataba wake unaomalizika mwaka 2018.

Mwisho? Lionel Messi anaweza kuondoka Barcelona kutokana na kusuasua kwa mazungumzo ya Mkataba mpya
Paris Saint-Germain inaweza kuwa tayari kumlipa mchezaji huyo mshahara wa Pauni Milioni 205, na kutokana na mpango wa ujenzi wa Uwanja mpya unaoweza kuigharimu Barcelona Pauni Milioni 493, inawezekana klabu hiyo ikafanya uamuzi usiofikirika na kumuuza mchezaji huyo ambaye amekuwa Barcelona tangu ana umri wa miaka 13.
Messi anataka kubaki Barcelona hadi atakapofikiri wakati wa kurejea klabu yake ya kwanza, Newell’s Old Boys ya Argentina umewadia, lakini Barcelona inaweza kumuuza kwa klabu nyingine ya Ulaya kati ya PSG hata Manchester City.


Babu kubwa duniani: Messi akiwa na tuzo ya Ballon d'Or ya mwaka 2012
MAFANIKIO YA LIONEL MESSI BARCELONA
2004:Mechi 420 mabao 351
La Liga 2004-5, 2005-6, 2008-9, 2009-10, 2010-11, 2012-13
Kombe la Mfalme: 2009, 2012
Ligi ya Mabingwa 2006, 2009, 2011
Rais wa sasa wa Barcelona, Josep Bartomeu alitaka kumpa mkataba mpya Messi kabla ya Fainali za Kombe la Dunia, lakini mchezaji huyo inafahamika anataka malipo ya Pauni Milioni 20.5 kwa mwaka na klabu inataka nusu ya haki ya matumizi ya picha zake, wakati kwa sasa mchezaji huyo anamiliki haki zote.
Kushindwa kuonyesha kiwango kilichotarajiwa katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na fainali ya Kombe la Mfalme kwa mara ya kwanza vimeifanya bodi ifikirie uamuzi wa kumpiga bei.

Tuesday 15 April 2014

Arsenal yaipiga Weastium united 3-1

BARCELONA WATWAA TAJI LA LIGI YA MABINGWA ULAYA KWA VIJANA, KINDA WAKE AFUNGA KUTOKA KATIKATI YA UWANJA

KINDA Munir El Haddadi jana alifunga bao tamu kutoka katikati ya Uwanja Barcelona ikitwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa vijana chini ya umri wa miaka 19 kwa kuifunga Benfica mabao 3-0 mjini Nyon, Usiwsi.
Munir alifunga mabao mawili jumla jana dakika za 33 na 87, wakati bao lingine lilifungwa na Rodrigo Tarin dakika ya tisa.
Timu ya kwanza ya Barca ipo katika wakati mgumu hivi sasa ikiwa imetolewa katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na wapinzani wao Hispania, Atletico Madrid na ikafungwa 1-0 na Granada Jumamosi katika La Liga.
Na baada ya kufungiwa kusajili hadi mwaka 2015 na FIFA, adhabu ambayo wameikatia rufaa, Wakatalunya hao wanaweza kupandisha viranga vyao vya akademi.


Wafalme: Nahodha wa Barca, Roger Riera akiwa ameshika taji la Ligi ya Mabingwa kwa vijana jana baada ya ushindi


Nyota wa baadaye: Munir El Haddadi akisherehekea ushindi wa Barca wa 3-0 jana

MAN CITY YAFUNIKA KLABU ZOTE DUNIANI KWA KULIPA MISHAHARA MIKUBWA, HAKUNA CHA BARCA WA REAL

KLABU ya Manchester City ndiyo inayoongoza duniani kwa kulipa mishahara mizuri wachezaji huku kiwango cha malipo ya mwaka kwa kila mchezaji kikiwa ni Pauni Milioni 5.3, au Pauni 102,653 kwa wiki, hiyo ni kwa mujibu wa taarifa mpya ya mlinganisho wa mapato ya klabu kubwa.
Klabu tano za Ligi Kuu ya England zimeingia kwenye 20 Bora na Liverpool iliyoifunga 3-2 City katika mbio za ubingwa Jumapili- inashika nafasi ya 20, kwa kumlipa kila mchezaji wastani wa Pauni Milioni 3.4 kwa mwaka.
Manchester United ni ya nane ikilipa Pauni Milioni 4.3 kwa mwaka, Chelsea ya 10 (Pauni Milioni 4) na Arsenal ya 11 (Pauni Milioni 3.9).

Walipwa vizuri: Manchester City imeongoza kwa kulipa wachezaji mishahara mikubwa duniani, ikikadiriwa kumlipa kila mchezaji wastani wa Pauni Milioni 5.3 kwa mwaka.

Kimwaga noti: Mmiliki wa City, Sheikh Mansour amewekeza mabilioni ya Pauni katika timu hiyo ili iwe mshindani katika ubingwa wa England
KLABU ZINAZOONGOZA KULIPA MISHAHARA MIZURI WACHEZAJI DUNIANI

NAFASI (MWAKA JANA)TIMULIGIMAKADIRIO YA MALIPO KWA MWAKA (WIKI)

NAFASI (MWAKA JANA)TIMULIGIMAKADIRIO YA MALIPO KWA MWAKA (WIKI)
1 (1)Manchester CityPremier League£5,337,944 (£102,653)
2 (5)New York YankeesMLB£5,286,628 (£101,666) 
3 (2)Los Angeles DodgersMLB£5,119,701 (£98,456) 
4 (3)Real MadridLa Liga£4,993,393 (£96,027) 
5 (4)BarcelonaLa Liga£4,901,327 (£94,256)
6 (16)Brooklyn NetsNBA£4,485,019 (£86,250) 
7 (9)Bayern MunichBundesliga£4,402,905 (£84,671) 
8 (12)Manchester UnitedPremier League£4,322,251 (£83,120)
9 (19)Chicago Bulls NBA£3,985,706 (£76,648) 
10 (8) ChelseaPremier League £3,984,536 (£76,626)
11 (15)ArsenalPremier League£3,901,923 (£75,037) 
12 (20) New York KnicksNBA £3,862,191 (£74,273) 
13 (14)Detroit TigersMLB£3,833,510 (£73,721) 
14 (11)Philadelphia Phillies MLB£3,811,638 (£73,301) 
15 (22)Boston Red SoxMLB £3,763,451 (£72,374)
16 (17)Miami Heat NBA £3,665,215 (£70,485) 
17 (23)San Francisco GiantsMLB£3,613,741 (£69,495)
18 (35)Juventus Serie A£3,512,696 (£67,552) 
19 (7)LA Lakers NBA £3,411,402 (£65,604)
20 (21)Liverpool 

Wednesday 9 April 2014

YANGA SC YAIPUMULIA AZAM FC KILELENI, BINGWA MWAKA HUU ATAKUWA BINGWA KWELI

Na Renatus Mahima, Dar es Salaam
YANGA SC imepunguza pengo la pointi inazozidiwa na vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Azam FC hadi kubaki pointi moja, kufuatia kuibwaga Kagera Sugar ya Bukoba mabao 2-1 jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Matokeo hayo yanaifanya timu hiyo inayofundishwa na babu Mholanzi, Hans van der Pluijm kutimiza pointi 52, baada ya kucheza mechi 24, wakati Azam FC iliyocheza mechi 23 ina pointi 53 kileleni.
Hamisi Kiiza ‘Diego’ aliifungia Yanga SC bao la kwanza dakika ya tatu, akiunganisha krosi maridadi ya Mrisho Ngassa.

Hamisi Kiiza aliifungia Yanga bao la kwanza dakika ya tatu tu

Didier Kavumbangu aliifungia Yanga SC bao la pili dakika 36 akimlamba chenga kipa Agatony Anthony baada ya kupokea krosi nzuri ya Simon Msuva na kuituliza kifuani kwanza, kabla ya kumtesa kipa wa timu ya Bukoba.
Sifa zimuendee Mrisho Ngassa kwa bao hilo, kwani ndiye aliyeanzisha shambulizi hilo kwa kuwatoka wachezaji wa Kagera na kumchomekea Simon Msuva mpira kwenye njia akapiga krosi.
Hilo lilikuwa bao la 30 katika mashindano yote kwa Kavumbangu ndani ya mechi 60 alizoichezea Yanga SC katika misimu miwili. Msuva naye amecheza mechi ya 30 leo akijivunia kutoa krosi ya bao.
Beki Ernest Mwalupani alikuwa mwenye bahati kwa kuonyeshwa kadi ya njano dakika ya 64 na refa Maalim Abbas wa Rukwa akimtuhumu kuwapendelea wenyeji katika kosa ambalo lilistahili kadi nyekundu.
Daudi Jumanne aliifungia Kegara Sugar bao la kufutia machozi dakika ya 62 kwa shuti kali.
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Mbuyu Twite, Frank Domayo, Simon Msuva, Hassan Dilunga, Didier Kavumbangu, Mrisho Ngassa/Hussein Javu dk63 na Hamisi Kiiza/Nizar Khalfan dk86.
Kagera Sugar; Agatony Anthony, Salum Kanoni, Mohamed Hussein, Ernest Mwalupani, Maregesi Mwangwa, George Kavilla, Benjamin Asukile/Juma Mpola dk55, Daudi Jumanne, Adam Kingwande/Zuberi Dabi dk61, Themi Felix/Hamisi Kitaganda dk84 na Paul Ngway.
Kutoka Mlandizi, Pwani mchezo kati ya wenyeji Ruvu Shooting na Azam FC ya Dar es Salaam uliokuwa ufanyike jioni ya leo Uwanja wa Mabatini Mlandizi mkoani Pwani umeahirishwa hadi kesho kufuatia mvua kubwa.
Timu hazikuwahi hata kuingia uwanjani kupasha misuli moto kutokana na mvua kubwa na Uwanja kujaa maji na ilipowadia Saa 10:20 waamuzi wa mechi hiyo waliingia uwanjani kukagua na kuvunja mchezo.
Kilifuatia kikao cha pande zote nne, baina ya viongozi wa Ruvu na Azam pamoja na TFF na marefa ambao waliafikiana mechi ichezwe kesho iwapo hali itakuwa nzuri.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ alikuwepo na kushuhudia hali hiyo.
Isihaka Shirikisiho wa Tanga ndiye aliyetarajiwa kuwa refa wa mchezo wa leo, akisaidiwa na Hassan Zani na Agness Pantaleo wote wa Arusha na refa wa akiba mwenyeji, Simon Mbelwa.
Azam yenye pointi 53 itaendelea kuishi kileleni mwa Ligi hata Yanga SC inayocheza na Kagera Sugar hivi sasa mjini Dar es Salaam itashinda, kwani wana Jangwani hao watatimiza pointi 52 huku pia wakiwa wamecheza mechi moja zaidi

BAYERN MUNICH YAING'OA MAN UNITED, BARCELONA NAYO YATUPWA HUKO KWA WASIOJUA

MANCHESTER United ya England imeaga Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kufungwa mabao 3-1 na wenyeji Bayern Munich Uwanja wa Allianz-Arena mjini Munich, Ujerumani usiku huu.
Hiyo inamaanisha United imeaga kwa kipigo cha jumla ya mabao 4-2, baada ya awali kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 Uwanja wa Old Trafford mjini Manchester.
United leo ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 57, mfungaji beki wake Mfaransa, Patrice Evra aliyefumua shuti kali kwa guu la kushoto baada ya kupokea pasi ya Antonio Valencia.


Sekunde 22 baadaye Mcroatia Mario Mandzukic akaisawazishia Bayern akitumia fursa ya wachezaji wa United kuzubaa kwa furaha ya bao, wakidhani biashara imekwisha na kumbe mpira ni hadi filimbi ya mwisho.

Tuesday 8 April 2014

112 WAFANIKIWA KUINGIA HATUA YA PILI KATIKA MASHINDANO YA KUSAKA VIPAJI VYA UIGIZAJI TANZANIA


Majaji wa Shindano la Kusaka la Vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents wakijadiliana jambo wakati wa Zoezi la kusaka vipaji vya uigizaji kuingia Hatua ya pili kwa washiriki waliofanikiwa kupita kwenye mchujo.Kulia ni Single Mtambalike (Rich Rich), Ivon Chery (Monalisa) na Roy Sarungi.

Washiriki waliofanikiwa kuingia kwenye hatua ya pili wakifanyiwa usaili kwaajili ya hatua ya pili sasa

Muongozaji wa Mradi wa Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents, Bw Stanford Kihole (kulia) akitoa maelekezo kwa washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili katika mashindano ya kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania likiwa limeaingia hatua ya pili Mkoani Mwanza

ROONEY FITI KABISA, AWAPASHIA KIKAMILIFU BAYERN MUNICH LEO

MSHAMBULIAJI Wayne Rooney amerejesha matumaini ya Manchester United kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuanza mazoezi kwa ajili Robo Fainali ya pili dhidi ya mabingwa watetezi, Bayern Munich Uwanja wa Allianz Arena kesho.
Rooney alikosa mechi ya Ligi Kuu England United ikiifunga mabao 4-0 Newcastle mwishoni mwa wiki kutokana na maumivu ya mguu, lakini sasa kuna uwezekano kesho akacheza
Ryan Giggs pia alifanya mazoezi baada ya kukosa mechi dhidi ya Newcastle, lakini Marouane Fellaini, ambaye alitolewa nje Uwanja wa St James Park baada ya kuumia na Rafael hawakushiriki mazoezi leo.
Baada ya sare ya 1-1 nyumbani, United sasa wanatakiwa kushinda ugenini dhidi ya Bayern ili kutinga Nusu Fainali.

Mazoezi makali: Rooney akifanya mazoezi kuelekea mchezo wa marudiano na Bayern Munich

AZAM NA YANGA KATIKA WIKI YA VITA KALI UBINGWA WA BARA

Na Boniface Wambura, Dar es Salaam
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inaendelea kesho (Aprili 9 mwaka huu) huku timu za Azam na Yanga ambazo zipo nafasi mbili za juu zikiendelea kuchuana.
Azam itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting katika mechi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Mabatini uliopo Mlandizi mkoani Pwani. Nayo Yanga itakuwa mwenyeji wa Kagera Sugar katika Uwanja wa Taifa jijini.
Yanga, Azam, Ruvu Shooting na Kagera Sugar zote zimeshinda mechi zao za raundi ya 23 wakati mechi za kesho zitakuwa kwa ajili ya kukamilisha raundi ya 24 ya ligi hiyo ambayo inatarajia kukamilika Aprili 19 mwaka huu.

Yanga na Azam kesho zinaingia katika wiki ngumu ya kusaka ubingwa

Ligi hiyo itaingia raundi ya 25 Aprili 12 na 13 mwaka huu ambapo timu zote 14 zitakuwa viwanjani. Aprili 12 mwaka huu itakuwa Mtibwa Sugar vs Ruvu Shooting (Manungu, Morogoro), Coastal Union vs JKT Ruvu (Mkwakwani, Tanga), na Tanzania Prisons vs Rhino Rangers (Sokoine, Mbeya).

Monday 7 April 2014

FIFA YAITANGAZIA NEEMA TANZANIA, TAYARI IMEIPA DOLA MILIONI 6 TFF

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
TANZANIA itanufaika na msaada mkubwa kutoka Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), wenye la kuboresha soka ya nchi hiyo na nyingine zote za Afrika, imesema taarifa ya FIFA.
Akizungumza wakati wa kufunga semina ya siku tatu mjini Johannesburg, Afrika Kusini Alhamisi, ambayo ilihudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 26 wanachama wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valcke ametoa ahadi ya kuipa sapoti kubwa soka ya Afrika ili siku moja timu zake ziweze kucheza Fainali ya Kombe la Dunia.


Washiriki wa semina ya siku tatu ya FIFA mjini Johannesburg, Afrika Kusini wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kufunga semina hiyo Alhamisi
Chini ya Mtendaji Mkuu wa Fainali za Kombe la Dunia 2010 na Rais wa Shirikisho la Soka Kenya (SAFA), Danny Jordaan, semina hiyo ambayo ilimalizika Alhamisi, ilifikia makubaliano ya kuongeza umakini katika kuboresha mambo mbalimbali, ikiwemo kiwango cha soka, utawala bora na kutatua matatizo yote sugu katika soka ya Afrika kwa msaada wa FIFA.
“Programu zote ambazo tutajadili kwenye hii semina, tunaweza kuwahakikishia kuwa hadi kufika mwaka 2022 mambo yatakuwa safi, na hii ni kwa mshikamano wa pamoja baina yetu,”alisema Valcke na kuongeza; “Tutahakikisha mnaimarika na kusonga mbele, ambayo itafanya ligi zenu ziwe bora, mtaendeleza mradi wa soka za vijana kwa kila mmoja anayetaka kucheza soka Afrika. Tutakusaidieni ili muwe bora, na tunataka timu za Afrika muda si mrefu zifike fainali ya Kombe la Dunia la FIFA.”
Kwa upande wake, Suketu Patel, Rais wa Baraza la Vyama vya Soka Kusini mwa Afrika (COSAFA) na Makamu wa Rais wa CAF, ameishukuru FIFA na kuzitaka nchi za Afrika kuonyesha bidii ya kusaka maendeleo. “Lazima tuwashukuru FIFA,” alisema na kuongeza. “Kila nchi mwanachama (wa FIFA) amepata kiasi cha dola (za Kimarekani) Milioni 6 kwa muongo uliopita. Sasa tujiulize tumefanyia nini kwa fursa hiyo ambayo tumekuwa tukipewa? Tumeitumia kuboresha miundombinu, au hali bado ni ile ile kama ilivyokuwa kabla ya misaada hii?,”alihoji.
Marais, Makatibu Wakuu na Wakurugenzi wa Ufundi wa vyama na mashirikisho ya soka wanachama wa CAF walihudhuria semina hiyo kutoka nchi za Angola, Botswana, Misri, Eritrea, Ethiopia, Gambia, Ghana, Kenya, Lesotho, Liberia, Lybia, Malawi, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Shelisheli, Sierra Leone, Somalia, Sudan Kusini, Sudan, Swaziland, Tanzania, Uganda, Zambia, Zimbabwe na wenyeji Afrika Kusini.