Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Monday 7 April 2014

FIFA YAITANGAZIA NEEMA TANZANIA, TAYARI IMEIPA DOLA MILIONI 6 TFF

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
TANZANIA itanufaika na msaada mkubwa kutoka Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), wenye la kuboresha soka ya nchi hiyo na nyingine zote za Afrika, imesema taarifa ya FIFA.
Akizungumza wakati wa kufunga semina ya siku tatu mjini Johannesburg, Afrika Kusini Alhamisi, ambayo ilihudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 26 wanachama wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valcke ametoa ahadi ya kuipa sapoti kubwa soka ya Afrika ili siku moja timu zake ziweze kucheza Fainali ya Kombe la Dunia.


Washiriki wa semina ya siku tatu ya FIFA mjini Johannesburg, Afrika Kusini wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kufunga semina hiyo Alhamisi
Chini ya Mtendaji Mkuu wa Fainali za Kombe la Dunia 2010 na Rais wa Shirikisho la Soka Kenya (SAFA), Danny Jordaan, semina hiyo ambayo ilimalizika Alhamisi, ilifikia makubaliano ya kuongeza umakini katika kuboresha mambo mbalimbali, ikiwemo kiwango cha soka, utawala bora na kutatua matatizo yote sugu katika soka ya Afrika kwa msaada wa FIFA.
“Programu zote ambazo tutajadili kwenye hii semina, tunaweza kuwahakikishia kuwa hadi kufika mwaka 2022 mambo yatakuwa safi, na hii ni kwa mshikamano wa pamoja baina yetu,”alisema Valcke na kuongeza; “Tutahakikisha mnaimarika na kusonga mbele, ambayo itafanya ligi zenu ziwe bora, mtaendeleza mradi wa soka za vijana kwa kila mmoja anayetaka kucheza soka Afrika. Tutakusaidieni ili muwe bora, na tunataka timu za Afrika muda si mrefu zifike fainali ya Kombe la Dunia la FIFA.”
Kwa upande wake, Suketu Patel, Rais wa Baraza la Vyama vya Soka Kusini mwa Afrika (COSAFA) na Makamu wa Rais wa CAF, ameishukuru FIFA na kuzitaka nchi za Afrika kuonyesha bidii ya kusaka maendeleo. “Lazima tuwashukuru FIFA,” alisema na kuongeza. “Kila nchi mwanachama (wa FIFA) amepata kiasi cha dola (za Kimarekani) Milioni 6 kwa muongo uliopita. Sasa tujiulize tumefanyia nini kwa fursa hiyo ambayo tumekuwa tukipewa? Tumeitumia kuboresha miundombinu, au hali bado ni ile ile kama ilivyokuwa kabla ya misaada hii?,”alihoji.
Marais, Makatibu Wakuu na Wakurugenzi wa Ufundi wa vyama na mashirikisho ya soka wanachama wa CAF walihudhuria semina hiyo kutoka nchi za Angola, Botswana, Misri, Eritrea, Ethiopia, Gambia, Ghana, Kenya, Lesotho, Liberia, Lybia, Malawi, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Shelisheli, Sierra Leone, Somalia, Sudan Kusini, Sudan, Swaziland, Tanzania, Uganda, Zambia, Zimbabwe na wenyeji Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment