Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Friday 20 September 2013

MAMA SHAROMILIONEA HAJAKABIDHIWA MALI ZA MWANAE MPAKA LEO


Mama Sharomilionea
Mama mzazi wa Marehem msanii wa bongo movie (comedy) na Bongo Flava Sharomilionea amefunguka kuwa mpaka leo anashangaa hajakabidhiwa baadhi ya vitu vya thamani alivyokua akimiliki mtoto wake kipindi yuko hai, na tayari imeshapita miezi 8 tangu Sharomilionea afariki kutokana na Ajali ya Gari aliyoipata mwaka jana mwezi wa kumi na  moja mita chache kabla hajafika kijijini kwa Lusungu Muheza Tanga,

KAKA AOMBA AC MILAN ISIMLIPE MSHAHARA MPAKA ATAKAPOPONA

Mchezaji wa kiungo cha kati wa AC Milan Kaka ameitaka klabu yake kutomlipa mshahara wake huku akiendelea kupona kutokana na jereha lake la paja ambalo alilipata wakati wa mchezo wake wa kwanza tangu kujiunga na kilabu hiyo. (HM)

Mchezaji huyo wa kimataifa wa timu ya Brazil aliondolewa uwanjani na jeraha hilo katika dakika ya 70 ya mechi waliyokwenda sare ya mabao mawili na timu ya Rossoneri.
Alirejea Milan bila malipo yoyote mapema mwezi huu baada ya kuhamia M

KOMBE LA DUNIA 2022: UEFA NA FA ZAGOMA MUDA WA KUCHEZWA KWA MICHUANO HIYO

2022-fifa-world-cup-awarded-to-qatar2_718e4.png
Hali ya hati hati kuhusu fainali za kombe la dunia mwaka 2022 zifanyike wapi, imechukua mkondo mpya baada ya viongozi wa soka Ulaya kukubali kuwa fainaliz hizo haziwezi kuchezewa nchini Qatar wakati wa majira ya joto.
Nchi hiyo ilipata nafasi ya kuandaa michuano hiyo kwa njia ambayo wengi wamepinga ikisemekana viwango vya joto nchini Qatar vinaweza kufika nyuzi hamsini majira ya joto.(P.T)

MASOGANGE, MELISA WAACHIWA HURU


maso aca5c
Johannesburg. Mtanzania Agnes Gerald, maarufu Masogange, ameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg, baada ya kulipa faini ya R30,000 (Sh4.8 milioni) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumika kutengeneza dawa za kulevya.(hd)www.hakileo.blogspot.com
Wakati Masogange akitozwa faini hiyo mwenzake, Melissa Edward ameachiwa huru na mahakama hiyo, baada ya kukosekana ushahidi wa kumtia hatiani.
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai cha Afrika Kusini(Hawk), Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya, bali kemikali aina ya ephedrine.
Hata hivyo, Mahakama ilibaini kuwa, Melissa hana hatia kwa kuwa ilionekana kuwa amemsindikiza Masogange, ambaye alimwomba amsaidie kubeba mzigo huo.
"Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu kumsaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini hayakuwa yake. Mizigo yote iliandikwa jina la Agness Gerald na si Melissa," alisema Kapteni Ramaloko.
Kapteni Ramaloko alisema, Melissa alijitetea kuwa hakuwa amesafiri pamoja na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na Masogange alimwomba amsaidie kubeba mizigo hiyo, kwani ilikuwa mikubwa.

KAMPENI YA USHOGA: MAN UNITED, SPURS & NORWICH ZAGOMEA!


BUTI-NYUZI_ZA_USHOGA

BAADHI ya Klabu za Ligi Kuu England, zikiwemo Mabingwa Manchester United, Tottenham na Norwich City, zimegoma kutoa sapoti kwenye Kampeni ya Kutetea Haki za Ushoga.

NAY WA MITEGO ATIWA MBARONI NA POLISI MKOANI MOROGORO


Kwa mujibu wa askari mmoja wa kikosi cha usalama wa barabarani aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa kuwa si msemaji wa jeshi hilo, walimkamata msanii…

Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ baada ya kunaswa na polisi wa usalama barabarani.
Kwa mujibu wa askari mmoja wa kikosi cha usalama wa barabarani aliyeomba hifadhi ya jina lake

BABY MADAHA AONYWA KUHUSU UNGA NA POMBE

www.tabasamuleo.blogspot.com


Stori: Gladness Mallya
MWANADADA anayefanya vizuri katika anga la Muziki Bongo,  Baby Joseph Madaha,  ametahadharishwa na baadhi ya wadau wa burudani hapa nchini  kutoshawishika na matumizi ya  madawa ya kulevya pamoja na unywaji wa pombe kupindukia kufuatia taarifa za hivi karibuni kuweka wazi mpango wake wa kupiga kambi nchini Kenya.
Baby Madaha.
Madaha ambaye ‘amekwaa dili’ la kufanya  kazi chini ya Kampuni ya Candy n’ Candy Records inayoongozwa na Joe Kairuki na iliyoko jijini Nairobi,   ameshauriwa hivyo kufuatia madai ya msanii mwenzake Rehema Chalamila kutopea zaidi kwenye matumizi ya madawa hayo baada ya kuhamia nchini humo kwa mgongo wa kazi ya muziki.

SIMBA KUKICHAPA NA MBEYA CITY

Kikosi cha Simba SC.
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaingia raundi yake ya tano kesho (Septemba 21 mwaka huu) kwa mechi huku vinara Simba wakiwakaribisha Mbeya City kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Uwanja wa Mkwakwani, Tanga utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Mgambo Shooting Stars na Rhino Rangers ya Tabora. Mtibwa Sugar itakuwa mgeni wa Tanzania Prisons katika pambano litakalochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya. 

YANGA YADAIWA NUSU BILLION


121 4841f
Yanga inayokabiliwa na kazi nzito ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Bara inapaswa kutafuta Sh. 428.5 milioni (karibu nusu bilioni) kwa ajili ya kuwalipa wachezaji wanne, viongozi wawili na kumpa fedha mmoja akailipe fidia klabu ya Simba. (HM)

MAKALA;Soka na siasa katika uhusiano wa kipekee-1




Soka na siasa kwa upande mwingine vyote vina vitu kadhaa vyenye ufanano kuliko ambavyo wengi wangeweza kudhania.
KWA hapa England watu wanapozungumzia siasa hujenga taswira ya wanaume na wanawake, wengi wao wazee wakiwa wamekaa kwenye mabenchi ya kijani bungeni.


Watu hao huwa kwenye ukumbi wa kawaida, tofauti kabisa na ule wa kisasa mno wa Dodoma nyumbani Tanzania.


Siasa ya hapa inachukuliwa na wengi kuwa ni masuala yanayochosha, yasiyo na mvuto yanayohusisha mijadala mingi bila kufikia hitimisho la pamoja.


Unapozungumzia soka kwa upande mwingine, picha inayowajia wengi ni ya wachezaji nyota wenye mvuto na viwango vya hali ya juu kisoka katika Ligi Kuu England, maarufu EPL. Naam, wanafikiria pia nje ya uwanja jinsi wachezaji hao, baadhi wakiwa ni mamilionea vijana, wakiendesha magari ya kisasa na ya bei mbaya mitaani, wakiishi maeneo ya hali ya juu ambayo watu wengi hawana hata ndoto za kuishi huko.

"Yanga yaapa ushindi dhidi ya Prisons"





By MWANDISHI WETU

Wachezaji wa Yanga walikiri kwamba hawakuwahi kukumbana na presha kubwa ya mashabiki wa timu pinzani mkoani kama ilivyokuwa wikiendi iliyopita jambo ambalo linawafanya wajiulize mara mbili kabla ya kurudi uwanjani ingawa wadau wa Mbeya wanadai kwamba Prisons haina mashabiki wengi kama Mbeya City.
WACHEZAJI wa Yanga wakiongozwa na nahodha wao, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wametangaza hali ya hatari kwa Prisons kwamba iwe isiwe hata kama vurugu zitajirudia, lazima washinde.

Lakini vuta pumzi kwanza. Kabla ya kushuhudia mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya, kesho Jumatano usiku, tayari utakuwa umejua vitu vitano muhimu vya kuvutia kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu, zitachezwa mechi saba siku hiyo hiyo.


Kwanza; Yanga ipo Mbeya ikicheza na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine, inarudi kwenye uwanja huo ambao ilikumbana na presha kubwa ya mashabiki wa Mbeya City Jumamosi iliyopita na kuambulia sare ya bao 1-1.

Mwombeki: Nikichezeshwa na Henry Joseph ni balaa




STRAIKA wa Simba, Betram Mwombeki ametamka kwamba kiungo Henry Joseph Shindika ni bonge la mchezaji na tangu aanze kuichezea Simba iwe kwenye ligi au mazoezi amegundua vitu vingi kwake.


“Kuna viungo wengi Simba, nawakubali uwezo wao kila mmoja na mchango kwenye timu, lakini kilichonivutia zaidi ni uwezo wa Henry anapokuwa uwanjani, ana nguvu, akili, uzoefu na ameuzoea mpira. Anajua ni wapi akuwekee mpira kutokana na kasi na mbinu ulizonazo mshambuliaji,” alisema Mwombeki.

Thursday 19 September 2013

Mourinho ;mimi ndio wa kulaumiwa


Meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho anasema yeye ndiye anayepaswa kuwajibika kufuatia kipigo cha timu yake ilipochuana na Basel kutoka Uswizi 2-1 katika mechi ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya.Mourinho uwanjaniwww.tabasamuleo.blogspot.com
Alikua mcheza kiungo Oscar aliyeifungulia Chelsea bahati ya uwezekano wa kushinda mechi hiyo lakini Mohamed Salah akarudisha kabla ya Marco Streller kufunga kwa kichwa bao la ushindi kwa Basel.
"tunaposhindwa sizungumzii wachezaji au mtu binafsi, huzungumzia jukumu langu," alisema Mourinho. "anayewajibika ni mimi."
Samuel Eto'o
Samuel Eto'o
Nyota aliyesajiliwa hivi karibuni Samuel Eto'o alianza mechi na mshambuliaji Demba Ba kuletwa baadaye katika kipindi cha pili, huku mshambuliaji mwingine Fernando Torres hakua hata kwenye meza ya wachezaji waliorodheshwa.
Hata hivyo meneja huyo kutoka Ureno alisisitiza kua hana wasiwasi juu ya kikosi chake hususan washambuliaji wake, licha ya ukosefu wa magoli.
"ninawaamini washambuliaji wangu watatu kwa msimu mzima," Aliongezea

Bingwa wa masumbwi afariki


Ken Norton na Mohamed Ali
Ken Norton na Mohamed Ali

Bingwa wa zamani wa dunia katika ndondi uzani wa Heavyweight mmarekani Ken Norton amefariki akiwa na umri wa miaka 70.Ken Norton uzeeni
Anakumbukwa zaidi kuwa kumshinda gwiji wa masumbwi Mohammad Ali mwaka 1973.
Sawa na mabondia wengi wa uzani mkubwa enzi zake, Ken Norton anakumbukwa kwa jinsi alivyopigana na Mohamed Ali.
Na kwenye pigano lao la kwanza la mwaka 1973, Norton ambaye hadi wakati huo hakujulikana sana alimkomesha Ali na kumshinikiza makonde www.hakileo.blogspot.comtangu mwanzo hadi mwisho.