Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Monday 30 December 2013

KANUNI YA 24, KUVURUGA MCHEZO

1. Wachezaji na viongozi wa timu itakayosababisha mchezo kuvurugika na hatimaye kuvunjwa, itapoteza mchezo huo hata kama ilikuwa inaongoza kwa magoli na timu pinzani itapewa ushindi wa pointi tatu na magoli matatu, iwapo timu pinzani inaongoza kwa magoli zaidi ya matatu, itabakia na idadi ya magoli hayo iliyokwishafunga.

BASI JIPYA LA AZAM FC "KAMA ULAYA"



Basi jipya la wachezaji wa klabu ya Azam FC ya Dar es Salaam, lililowasili nchini juzi likiwa tayari kusafirishwa visiwani Zanzibar ambako timu hiyo imekwenda kushiriki Kombe la Mapinduzi. Hili ni aina ya mabasi ambayo yanatumiwa na klabu za Ulaya kama Manchester United, Bayen Munich na Barcelona ambalo kwa Afrika Azam inaweza kuwa klabu ya kwanza kulimiliki.

MZUNGUKO WA PILI LIGI KUU NI VITA YA KUSAKA UBINGWA NA KUKWEPA RUNGU LA KUSHUKA DARAJA!!


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
NGWE ya lala salama ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014 unatarajia kuanza kushika kasi januari 25 mwakani.
Kwasasa timu zote 14 zinazoshiriki ligi hiyo zipo katika maandalizi ya vikosi vyao ili kufanya vizuri zaidi ya mzunguko wa kwanza.
Wataalamu wengi wa soka wanasema mzunguko wa pili kama ilivyo kawaida timu zinajigawa katika makundi matatu.

Sunday 29 December 2013

ROSE MUHANDO AWAKUNA WAKAZI WA TANGA UWANJA WA MKWAKWANI



Mwimbaji mahiri wa nyimbo za kiroho a.k.a Injili,na anaetamba na wimbo mpya wa Facebook,Rose Muhando akiwa sambamba na skwadi lake zima wakilishambulia jukwaa vilivyo jioni ya leo ndani ya uwanja wa Mkwakwani wakati wa muendelezo wa tamasha la Krisimasi lililofanyika leo Mkoani Tanga.Tamasha hilo ndio kwa mara ya kwanza linafanyika mkoani humo,limezindundiliwa jijini Dar siku ya Krisimasi ndani ya uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na watazamaji lukuki.Tamasha hilo baada ya kufanyika mkoani Tanga,kesho litafanyika jijini Arusha na baadae mkoani Dodoma likiwajumuisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za Injili.

Baada ya Jaguar kuonyesha hili gari jipya, Prezzo nae kalionyesha lake nje ndani


Unaambiwa wiki moja baada ya staa wa muziki Kenya (Jaguar) kuonyesha gari lake jipya aina ya Jaguar ambalo alionekana nalo alipokwenda kufanya show, zimetoka picha za nje ndani za gari analotembelea rapper CMB Prezzo wa Kenya ambae mara kadhaa waliingia kwenye headlines na Jaguar kwa malumbano mbalimbali ikiwemo kutambiana muziki, mali na uwezo wa kifedha.

NGASSA HATARINI KUKOSA KOMBE LA MAPINDUZI, TYPHOID YAMLAZA

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
MSHAMBULIAJI tegemeo wa Yanga SC, Mrisho Khalfan Ngassa anasumbuliwa na homa ya matumbo, typhoid ambayo inaweza kumfanya akose michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayotarajiwa kuanza wiki hii visiwani Zanzibar.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana, Ngassa alisema kwamba baada ya kuona hali yake si nzuri kiafya juzi alikwenda kupimwa na akakutwa na maradhi hayo.
“Nimepatiwa tiba na sasa hivi nipo katika dozi, nadhani nitahitaji angalau wiki mbili za kupumzika ili niwe sawa kabisa. Kwa ujumla nimekuwa nikijisikia vibaya kwa muda mrefu tu, ila nikawa nakula dawa za kutuliza maumivu,”alisema Ngassa.

Anaumwa typhoid; Mrisho Ngassa anahitaji kiasi cha wiki mbili kupumzika kutokana na kusumbuliwa na homa ya matumbo
Yanga SC wamepangwa Kundi C katika Kombe la Mapinduzi, michuano itakayoshirikisha timu 12, pamoja na mabingwa watetezi, Azam FC, Tusker ya Kenya na Unguja Combine.
Kundi kuna Mbeya City, Pemba Combine, Chuoni na URA kutoka Uganda wakati Kundi B lina timu za Simba SC, KMKM, AFC Leopards ya Kenya na KCC ya Uganda.

CHELSEA YAIKALISHA LIVERPOOL DARAJANI, SUAREZ AFANYIWA 'UNDAVA' KINOMA, SPURS NAYO YAUA 3-0



Shujaa; Samuel Eto'o akishangilia baada ya kufunga bao la ushindi, Chelsea ikiilaza Liverpool 2

KOCHA Mreno Jose Mourinho ametoka na furaha Uwanja wa Stamford Bridge jioni hii, baada ya timu yake, Chelsea kuilaza mabao 2-1 Liverpool katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Shukrani kwake mshambuliaji mkongwe, Samuel Eto'o aliyefunga bao la ushindi dakika ya 34 akimalizia pasi ya Oscar ndani ya sita.
Mabeki wa Chelsea walimchezea 'kindava' mshambuliaji Luis Suarez na akatoka uwanjani bila kufunga bao.

Liverpool ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya nne, mfungaji Skrtel, lakini Edin Hazard akasawazisha dakika ya 17.
Kwa ushindi huo, Chelsea inatimiza pointi 37 na kubaki nafasi ya tatu, wakati Liverpool inabaki na pointi zake 36.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo leo, Tottenham Hotspur imeifunga Stoke City mabao 3-0, wafungaji Soldado dakika ya 37, Dembele dakika ya 65 na Lennon dakika ya 69.



Ushindi raha; Lennon kulia akishangilia Adebayor baada ya kuifungia Spurs katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Stoke leo

TFF YASEMA: RAGE BADO MWENYEKITI HALALI SIMBA



Ismail Aden Rage ndiye Mwenyekiti halali wa Simba ambapo Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imemtaka kuitisha Mkutano Mkuu kwa mujibu wa taratibu za klabu ya Simba. (HM)
Kamati imebaini upungufu kadhaa wa kisheria kwenye uamuzi wa Kamati ya Utendaji ya Simba uliofanywa Novemba 18, 2013 kwa kumsimamisha Mwenyekiti wao. Upungufu huo ni pamoja na ukiukwaji wa Ibara ya 33 ya Katiba ya Simba juu uitishaji wa mkutano, ajenda ya kumsimamisha Mwenyekiti kuwasilishwa kwenye kikao kwa utaratibu wa mengineyo.

ARSENAL YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND nsa CHEALSE YA ICHAPA LIVERPOOL


Home » Unlabelled » ARSENAL YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND
MSHAMBULIAJI Olivier Giroud amemaliza ukame wa mabao katika mechi saba baada ya kuifungia Arsenal bao pekee la ushindi Uwanja wa St James' Park katika mchezo wa Ligi Kuu England.
Giroud alifunga bao hilo pekee dakika ya 65 akimtungua kipa Tim Krul kufuatia krosi maridadi ya Theo.
Kwa ushindi huo, Arsenal inarejea kileleni kwa kufikisha pointi 42 baada ya kucheza mechi 19, ikiishusha Manchester City hadi nafasi ya pili kwa pointi zake 41.

MAGOLIKIPA WA LIGI KUU YA VODACOM WAIFUNGA CLOUDS MEDIA MABAO 3-1.


Wachezaji wa timu ya Clouds Media Group wakifanya mazoezi mepesi kabla ya kuanza kwa mtanange wa kufunga mwaka dhidi ya timu ya magorikipa wanaocheza Ligi Kuu ya soka tanzania Bara.

Mbwiga akijifua.

Kocha mchezaji wa timu ya Clouds Media Group, Mbwiga Mbwiguke (kulia) akiwaongoza wachezaji wenzake katika mazoezi.

Friday 27 December 2013

TAZAMA MAYWEATHER 'ALIVYOWATANDIKA' PACQUIAO, AMIR KHAN NA MAIADANA

BONDIA Floyd Mayweather amefufua vita ya maneno na mpinzani wake, Manny Pacquiao pamoja na kuwakandia pia Amir Khan na Marcos Maidana kwa staili ile ile. Pamoja na kumuita Pacquiao majeruhi wa Juan (Manuel) Marquez akikumbushia kipigo cha Mfilipino huyo mwishoni mwa mwaka 2012 kwa Knockout (KO) kutoka kwa Mmexico huyo, Mayweather ameweka picha ya 'kubumba' akiwa amemsukumia konde zito usoni. "Sasa unaniambia nakwenda kula makombo ya Juan Marquez? Acha nizungumze na IRS juu ya hili," alitweet mbabe huyo.

NEYMAR NOUMAAAA, APIGA TANO PEKE YAKE MECHI LA HISANI LA MASTAA BRAZIL

WAKATI La Liga ikiwa mapumzikoni, nyota wa Barcelona, Neymar alitumia nafasi hiyo kurejea Brazil kushiriki mchezo maalum wa hisani dhidi ya mchezaji wa zamani wa Paris Saint-Germain na AC Milan, Leonardo.

Marafiki wa Neymar waliwafunga Marafiki wa Leonardo mabao8-6 huku Neymar akifunga mabao matano na kuonyesha uwezo mkubwa sana wa kandanda pamoja na kuonyesha tattoo yake mpya.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 atarejea Hispania mapema Januari akidhamiria kuiongoza Barca katika mashindano ya nyumbani na Ulaya kwa mafanikio, kabla ya kwenda kwenye Fainali za Kombe la Dunia nyumbani kwao, Julai mwakani.


Kitu kipya: Neymar ameonyesha tattoo yake mpya wakati wa mechi ya hisani mjini Goiania, Brazil

BAADA YA KATIBU MKUU - MSEMAJI WA SIMBA NAE AACHIA NGAZI MSIMBAZI



Thursday 26 December 2013

WENGI WAJITOKEZA KUUGAGA MWILI WA ALIYEKUWA KOCHA WA MAKIPA SIMBA MAREHEMU JAMES KISAKA yupo pia Jacob Steven JB

Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Kocha wa makipa wa Simba, marehemu James Kisaka likiingizwa kwenye basi la klabu hiyo, baada ya kutolewa heshima za mwisho katika misa iliyofanyika katika Kanisa la Muhimbili, Dar es Salaam. Marehemu Kisaka atasafirishwa kwenda kwao wilayani Muheza, Tanga kwa mazishi yatakayofanyika kesho. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

LUNYAMILA AENDELEA KUPATA NAFUU....

Viongozi wa Young Africans Sports Club pamoja na wachezaji wa zamani walipomtembelea kumjulia hali mchezaji Edibily Lunyamila katika hospitali Mwananyamala Disemba 24 mwaka huu.
Lunyamila anasumbuliwa na tatizo la mapafu, hali yake kwa sasa inaendelea vizuri.
Young Africans Sports Club tunamuombea Lunyamila apate nafuu ya haraka na kupona kabisa aweze kuendelea na shughuli zake za kila siku.

Abdallah Bin Kleb, Mohamed Bhinda, Juma Kaseja, Dr Nassoro Ally Matuzya, Kaise Edwin wakiwa nje ya wodi aliyolazwa mchezaji Edibily Lunyamila siku moja kabla ya Xmass wallipokwenda kumjulia hali

MISS TANZANIA 2013 ASHEREHEKEA SIKUKUU YA X - MASS PAMOJA NA WATOTO YATIMA MOROGORO


Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa Akikabidhi zawadi waliotoa katika kituo hicho kwa Mama Mkuu wa Wa shirika la Masista wa Moyo safi wa Maria Sista Flora Chuma..

JAMES KISAKA AFARIKI DUNIA,


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa kocha wa makipa wa Simba, James Kisaka (57) kilichotokea leo asubuhi (Desemba 25 mwaka huu) katika Hospitali ya Burhani, Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Kisaka kabla ya kuwa kocha alikuwa mchezaji katika nafasi ya kipa. Mbali ya Simba, timu nyingine alizowahi kudakia ni Ndovu ya Arusha, Volcano ya Kenya na Small Simba ya Zanzibar.

Logarusic: Mkinipa Yanga nafukuza mabeki wote



Kocha Mkuu wa Simba,Zdravko Logarusic.PICHA|MAKTABA
KOCHA Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, amempa pole mwenzake wa Yanga, Ernest Brandts, kwa kupewa notisi na uongozi wa timu hiyo, lakini akasema angekuwa anaifundisha Yanga angewatimua mabeki wanne wa kikosi hicho wakiwamo nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani.

Katibu mpya TFF aingia na mikwara



Katibu Mkuu mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa.
By Elius kambili,Mwananchi
KATIBU Mkuu mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa, ameliambia Mwanaspoti kuwa jambo atakaloanza nalo akiingia ofisini ni kuziba mirija yote ya watu kujipatia fedha isivyo halali kupitia shirikisho hilo.

Tuesday 24 December 2013

MTAWALA NA MWESIGA WAPATA MASHAVU TFF.





MOHAMED MATUMLA NASIBU RAMADHANI KUMARIZA UBISHA CHRXMAS


Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao leo katika

ukumbi wa friends corner hotel manzese Dar es salaam leo katikati ni promota wa mpambano huo kaike siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com



Promota kaike Siraju akiwainua juu mikono Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani kwa ajili ya mpambano wao wa kugombea pikipiki siku ya sikukuu ya Xmasi Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com

Simba wajazwa ‘manoti’

Dar es Salaam. Uongozi wa Simba umewazawadia wachezaji wake kitita cha Sh60 milioni baada ya kufanikiwa kuichapa Yanga mabao 3-1 katika pambano la Hisani lililopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Akizungumza jijini jana, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Sued Nkwabi alisema, fedha hizo zimetolea kama njia moja wapo ya kuonyesha kuthamini juhudi zilizofanywa na wachezaji hao na kufanikiwa ushindi.Simba Sports Club

MECHI YA MTANI JEMBE YAINGIZA MIL 422/-



Mechi ya Nani Mtani Jembe kati ya Yanga na Simba iliyochezwa juzi (Desemba 21 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 imeingiza sh. 422,611,000.

Mapato hayo ni kutokana na washabiki 52,589 waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 40,000. Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo walikuwa 19,044.

Monday 23 December 2013

HII NDIO TAARIFA RASMI YA KUFUKUZWA KOCHA WA YANGA ERNST BRANDTS



Uongozi wa klabu ya Young Africans SC
umempatia taarifa (Notice) ya siku ya
thelathini (30) kocha mkuu mholanzi Ernie
Brandts juu ya kusitisha mkataba wake
kuanzia jana Disemba 22 mwaka huu.
Maamuzi hayo yanafuatia muenendo wa
matokeo mabaya katika michezo iliyopita
ya Ligi Kuu, kirafiki na bonanza la Nani
Mtani Jembe dhidi ya Simba SC mwishoni
mwa wiki.

England,RATIBA: MICHEZO YA LIGI KUU SIKU YA BOXING DAY NA MWISHO WA MWAKA HUU


 DECEMBER 29 2013

IN CENTRAL AFRICA TIME(CAT)

Thursday 26 December 2013

Hull City v Manchester United The KC Stadium 14:45

Aston Villa v Crystal Palace Villa Park 17:00

Cardiff City v Southampton Cardiff City Stadium 17:00

BREAKING NEWZ: LUNYAMILA MAHUTUTI MWAANYAMALA


WINGA wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Edibily Lunyamila leo hii asubuhi amekimbizwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kusumbuliwa na kifua na sasa anapumua kwa msaada wa mashine.

Mtandao huu ulifanikiwa kufika hospitalini hapo muda mfupi baada ya winga huyo kukimbizwa hospitalini hapo baada ya kuzidiwa tangu jana usiku akiwa nyumbani kwake Mbezi jijini Dar es Salaam.

SOMA HABARI KAMILI http://hakileo.blogspot.com/2013/12/breaking-newz-lunyamila-mchezaji-wa.html#more

Mgimwa azushiwa kifo, Kikwete apasua kichwa

Na tanzania daima.
WAKATI mawaziri wanne wameng’olewa na wengine walioitwa mizigo wanatarajiwa kutimuliwa wakati wowote, Rais Jakaya Kikwete yupo katika wakati mgumu wa kusaka warithi wa nafasi hizo, Tanzania Daima limebaini.

Ugumu wa kusaka warithi wa mawaziri hao, umeongezeka zaidi jana baada ya Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk. William Mgimwa kuzushiwa kifo kutokana na afya yake kuzorota.

SOMA HABARI KAMILI
  http://hakileo.blogspot.com/2013/12/mgimwa-azushiwa-kifo-kikwete-apasua.html#more

MANJI AWAOMBA WANACHAMA WA YANGA WASIVUNJIKE MOYO



Mwenyekiti wa Yanga Bw.Yusuf Manji akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu, kushoto ni makamu mwenyekiti Clement Sanga

Mwenyekiti wa klabu ya Young Africans Bw. Yusuf Manji amewaomba wanachama, wapenzi na washabiki wasivunjike moyo kwa matokeo ya jana ya mchezo wa kirafiki dhidi ya ya Simba SC, mechi iliyochezwa katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Hatima ya Rage kujulikana leo

NA MWANANCHI
Dar es Salaam. Hatma ya Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage itajulikana leo wakati kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya mwenyekiti wake Jamal Malinzi atakapokutana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kikao hicho mbali na kumjadili Rage pia kitapitia ajenda mbalimbali ikiwemo uundwaji wa vyombo vya haki Kamati ya Nidhamu, Kamati ya Maadili na Kamati ya Uchaguzi.

LIVERPOOL KAMA SIMBA SC, YAUA 3-1 SUAREZ APIGA MBILI



Mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez akishangilia baada ya kufunga bao la pili dhidi ya Cardiff Uwanja wa Anfield leo

MSHAMBULIAJI Luis Suarez ameendeleza makali yake baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa Liverpool wa 3-1 dhidi ya Cardiff jioni hii Uwanja wa Anfield.

Sunday 22 December 2013

Bayern klabu bingwa ya dunia



Bayern Munich wamejiongezea taji jingine baada ya kuwafunga Raja Casablanca ya Morocco 2-0 na kutwaa Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia.
Katika mechi iliyopigwa jijini Marrakech kwenye falme ya Morocco, Wajerumani hao walijawa furaha kuongeza kombe hilo katika hazina yao
ambayo tayari ina makombe ya ubingwa wa Ulaya,

Saturday 21 December 2013

ONA PICHA ZA JINSI SIMBA ALIVYO MCHAPA YANGA JANA NA SHAMRA SHAMRA ZA KUPOKEA KOMBE NA MASHABIKI WALIOZIMIA.


Wachezaji wa Simba na Yanga wakisalimiana.

Kikosi cha Simba.

Kikosi cha Yanga.

Benchi la ufundi la timu ya Simba.

Benchi la Ufundi la Yanga.

Henry Joseph wa Simba (kushoto) akichuana na beki wa Yanga, David Luhende.

Henry Joseph wa Simba (kushoto) akichuana na beki wa Yanga, David Luhende.

Mashabiki wa Simba wakishangilia bao la kwanza la timu yao.

Raha ya ushindi.

Furaha kwa Simba.



Hamisi Kiiza akitafuta mbinu za kumtoka, Ramadhani singano.

Ivo Mapunda akiruka juu kuokoa moja ya hatari langoni mwake.

Mashabiki wa Yanga wakiwa hawaamini kilichotokea uwanjani baada ya kuchapwa 3-1 na watani zao wa jadi Simba.

Juma Kaseja akibembelezwa na Mbuyu Twite baada ya kusababisha

Mmoja wa mashabiki wa Yanga akitolewa nje baada ya kuzimia uwanjani.

Emmanuel Okwi akimtoka beki wa Simba.

Wachezaji wa akiba wa Simba wakishangilia baada ya filimbi ya mwisho.

Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic akishangilia baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 3-1.
Wachezaji wa Simba wakimnyanyua juu kocha wao, Zdravko Logarusic mara baada ya kumalizika kwa mchezo maalumu wa Nani Mtani Jembe uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba ilishinda 3-1.









Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe akimkabidhi kombe nahodha wa Simba Haruna Shamte.