Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 22 March 2014

SOMO : MAONO NA NDOTO * sehemu ya saba na nane*

Mtumishi Gasper Madumla.

Haleluya....
Nakusalimu nikikuambia;
Bwana Yesu asifiwe sana...

Leo tunaingia katika kipengele kipya kabisa kuhusu NDOTO.Maana katika siku sita zote tulikuwa tukijifunza kuhusu maono.

Wengi wametafsiri neno NDOTO kwa tafsiri tofauti tofauti,ingawa tafsiri nyingine si tafsiri sahihi. Leo tanajifunza tafsiri sahihi iliyo rahisi kabisa ya neno NDOTO.

Ndoto ni nini?
*Ndoto ni mtiririko wa picha zitembeazo katika akili ya mtu,pindi mtu huyo anapokuwa amelala.

Ndoto huja pale mtu anapokuwa amelala,na ndio maana huwezi kumkuta mtu ambaye ajalala,mtu atembeaye kisha akuambie ya kwamba alikuwa anaota ndoto wakati anatembea.

Hakika ukikutana na mtu kama huyo ni lazima utamshangaa !..
Na swali la kwanza utakalo muuliza mtu huyo ni hili;
"Je wakati unatembea ulikuwa umelala,hata uote?"
Na swali la namna hiyo ni swali la msingi kabisa,maana sote twajua kwamba; ili mtu aote inampasa alale.

Haleluya...
Groly to God....

Tofauti ya MAONO na NDOTO.
*Maono yanaweza kuonekana hata pasipo kulala,lakini NDOTO ni lazima muhusika alale ndipo aote

* Maono huusika na roho,wakati NDOTO huusika na akili.
Kumbuka;
Mtu anapolala roho yake i macho,roho ya mtu aliye hai ailali,hivyo mtu anaweza kupata maono akiwa hajalala au hata akiwa amelala(Kama tulivyojifunza siku sita za fundisho hili)
Lakini mtu hawezi kupata ndoto akiwa hajalala sababu ndoto husubiri kupumzika kwa akili.

*Maono huwa na maana na mafunuo ya msingi,NDOTO nyingi huwa hazina maana.
Ndiposa Mhubiri anasema;
" Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..."Mhubiri 5:3

>Wengi huota kwa sababu ya miangaiko ya mchana kutwa,wakilala tu pale akili inapopumzika,nao huota. Ndoto za namna hii huwa hazina maana.



*Watu wengi huota ndoto,wachahe sana huona maono.
>Hapa sasa;
Ninajua hata wewe utakuwa umeshawahi kuota ndoto nyingi sana,hata nyingine huzikumbuki hivi sasa,lakini vipi kuhusu maono? UMESHAWAHI KUPATA MAONO YOYOTE?

Leo hii wakitokea watu wawili kisha mmoja aanze kusema hivi;

"...Jana nilikutana na Mungu,akanionesha mambo makubwa kisha Mungu akaniambia..."

Huyu mtu wa kwanza,hawezi kuaminika kiurahisi kwa ushuhuda wake wa kuonana na nguvu za Mungu maana watu watamshangaa ! wakihoji kwamba inawezekanaje akutane na Mungu?

Haya;

Mtu wa pili naye aje na kusema hivi;
"...Jana nilikutana na shetani na mapepo yake...."

Watu wa leo watamuamini zaidi,na kumsikiliza huyu wa pili kwa sababu eti amekutana na shetani na mapepo yake.Ushuhuda wa mtu wa pili umepewa nafasi zaidi ya ushuhuda wa mtu wa kwanza aliyeshuhudia amekutana na Mungu/Nguvu za Mungu katika maono.

Bwana Yesu asifiwe sana...

Mimi siwashangai sana watu wa namna hiyo, wale wenye kukataa kumuamini mtu yule wa kwanza aliyesema ameonana na Mungu sababu kupata MAONO juu ya nguvu za Mungu sio rahisi hata kidogo,tofauti na kuonana na shetani na mapepo yake.

Ndio maana ninakuambia MAONO hupatikana kwa nadra sana,MAONO makubwa ni kwa wale watu wa rohoni,Bali NDOTO ni kwa watu wote.

Haleluya...

Ndoto ni njia mojawapo ya mawasiliano ya ki-Mungu au hata ya kipepo pia.
Nasema ni mawasiliano ya ki-Mungu kwa maana tumeona Mungu akisema na watu wake wengi katika ndoto,akiwaonya,akiwapa maelekezo,au akisema nao juu ya mambo yajayo.

Tazama hapa;
" Na hao walipokwisha kwenda zao,tazama,malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto akasema,Ondoka,umchukue mtoto na mama yake,ukimbilie Misri,ukae huko hata nikuambie;kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize." Mathayo 2:13.

Bwana Mungu anamfikishia taharifa Yusufu kwa njia ya malaika,akimueleza mabaya yanayotarajiwa kufanywa na Herode.
Ndoto ikawa kama chombo cha kukamilisha taharifa ya Mungu kwa Yusufu.Vivyo hivyo Mungu anaeweza kusema nawe kwa njia ya malaika juu ya mambo ya hatari ndani ya maisha yako.

Biblia inaweka wazi ya kwamba Bwana Mungu hujifunua katika maono,lakini husema nasi katika ndoto;

" Kisha akawaambia,
Sikilizeni basi maneno yangu;
Akiwapo nabii kati yenu,
Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,
Nitasema naye katika ndoto."Hesabu 12:6

Haleluya...

Katika nyakati hizi za mwisho,Bwana bado husema nasi katika ndoto,akitufunulia mambo yajayo….








MAONO NA NDOTO * sehemu ya nane *

Bwana Yesu asifiwe...

02.NDOTO
Ingawa ndoto nyingi zinazo-otwa huwa hazina maana Lakini zipo baadhi ya ndoto zenye maana na zenye kubeba ujumbe mkubwa.

Katika maandiko matakatifu,Biblia ;Zipo ndoto nyingi ambazo Bwana Mungu alikuwa akisema na watu wake tofauti tofauti katika muda tofauti tofauti.
Kulikuwa na wakati ambapo Bwana Mungu alipotaka kuwaonya watu wake,au pale alipotaka kuwapa maelekezo juu ya mambo yajayo alitumia njia ya NDOTO.

Hivyo;
Ndoto ikawa mojawapo ya njia ya mawasiliano baina ya Mungu na watu wake.

Jambo moja la msingi ambalo tunapaswa kujua siku ya leo ni hili;

*Uotapo ndoto yoyote usimwambie mtu yeyote Bali umuulize Bwana Mungu kwanza.

Haleluya...

Si kila mtu utakaye mshirikisha ndoto yako,atakuunga mkono wengine wataifisha hiyo ndoto. Yamkini Mungu amesema na wewe kwa njia ya ndoto,ujumbe huo ambao Bwana Mungu ameuachilia kwako una kuhusu wewe na Yeye kwanza,ndio maana mwingine amefichwa ila kwako limefichuliwa kwa ndoto.

Sasa ukienda kumuuliza mwanadamu,mwanadamu awaye yote hawezi kukujibu maana yeye mwenye mwili naye humuitaji BWANA MUNGU.
Ndiposa ninakuambia USIJE UKAANZA KUOMBA MSAADA KWA MWANADAMU KABLA YA KUMUOMBA MUNGU.

Maana ukiona wewe umepewa fursa ya kupata ndoto yenye ujumbe kamili basi ujue ni wewe ndio uliyekusudiwa ujumbe huo ili hufanyie kazi ndoto hiyo,na yamkini kupitia wewe ujumbe ukamilike.

Zingatia hili;
Sisemi usimshirikishe kabisa mtu,hapana!
Kwanza wa kuombwa majibu ya ndoto ni Mungu kisha ikiwa umeomba mbele za Bwana Mungu na hukupata majibu ya ndoto uliyoota ndiposa waweza ukamwendea mtu mwenye karama ya kufasiri ndoto,kwa huyo mtu wa Mungu aweza kukusaidia kuomba kwa Mungu na hatimaye Mungu akakufunulia hiyo ndoto yako.

Nimekwambia si wote watafurahia ndoto yako maana wengine watajaribu hata kuiua.
Tunamjua mtu mmoja aitwaye Yusufu.Alipoota tu akaenda kuwaambia watu ndugu zake. Ndugu zake wakamchukia hata kutaka kumuua.

" Yusufu akaota ndoto,akawapa ndugu zake habari,nao wakazidi kumchukia;" Mwanzo 37:5

Biblia inasema kwamba ndugu zake Yusufu wakamchukia Yusufu.Hawa ndugu hawakumchukia Yusufu kwa mambo mengine yoyote,isipokuwa walimchukia kwa sababu ya NDOTO alizoziota Yusufu.

Hatuoni Yusufu akimuuliza Bwana Mungu ili apewe maelekezo sahihi ya kile alichokiota,Bali tunachokiona ni kwamba mara Yusufu alipoota tu,akaenda moja kwa moja na kuwapasha habari ndugu zake.

Ndugu zake wakamchukia yeye kwanza,na wala hawakuchukia ndoto aliyoota. Baadaye tunaona wakataka kumuangamiza kwa sababu ya kile alichokiota.

Vivyo hivyo kwako mpendwa;
Waweza kuoto ndoto kubwa sana,na ukijaribu kwenda kuwashirikisha wanadamu pasipo kuanza na Mungu ujue hao wanadamu watakuchukia wewe na wala hawataichukia hiyo ndoto.

Haleluya...
Bwana Yesu asifiwe....

Nazungumza na mtu mmoja mahali hapa,
Bwana wa Bwana anastahili sifa....

Biblia inazidi kueleza kwamba Yusufu akaota ndoto nyingine. Ndoto nyingine aliyoiota Yusufu ilikuwa inafanana na ile ndoto ya kwanza aliyoiota.

Ukisoma Mwanzo 37:7-8 utakuta Yusufu akiwaeleza ndugu zake ndoto ya kwanza aliyoiota,lakini pia ukisoma Mwanzo 37:9-11 utakuta Yusufu yule yule akiwaeleza ndugu zake ndoto ya pili aliyoiota.

Ukilinganisha ndoto hizi mbili utangua kwamba;
DHIMA yake inafanana ingawa mahitaji yaliyotumika yalitofautiana.

Dhima ni ujumbe wa msingi.Ujumbe katika ndoto hizi mbili ulifanana.
Mahitaji ni vibebea ndoto ili dhima ikamilike. Mfano wa mahitaji/requirements ya ndoto ya kwanza yalikuwa ni MIGANDA wakati ndoto ya pili ilikuwa ni JUA,MWEZI na NYOTA.

Haleluya....
Nasema,Haleluya...

Jambo la pili tunalojifunza hapo ni kwamba;

*Ndoto yenye kubeba ujumbe mkubwa wa ki-Mungu,mara nyingi NDOTO hujirudia zaidi ya mara moja.

Ujumbe ambao Yusufu alioneshwa katika ndoto ulikuwa ni ujumbe mkubwa sana kiasi kwamba tunaona BWANA MUNGU akijaribu kumuelezea Yusufu mara mbili kwa jambo lile lile.

Leo;
Ukiona una ndoto yenye kupata kujirudia rudia hujue lipo kusudi la msingi ndani ya ndoto hiyo,tena usije ukaipuuzia hata kidogo.

Sisemi kwamba ni lazima ndoto yenye kusudi ijirudie rudie.Zipo baadhi za ndoto zenye maana kamili ambazo hujitokeza mara moja tu.Lakini nyingi hujirudia rudia kuonesha ya kwamba ipo kazi ya kufanya ndani ya ndoto za namna hizo.

Bwana Yesu asifiwe...

Biblia inazidi kueleza kwa habari ya ndoto ya Yusufu,kwamba;
"Ndugu zake wakamhusudu;bali baba yake akalihifadhi neno hili."Mwanzo 37:11

Wapo wachache wenye kulihifadhi neno lako ulisemalo katika ndoto uliyoiota.Nasema watu wa namna hii wenye kuhifadhi ndoto yako ni wachache sana katika ulimwengu huu.

Watu weliopewa kulihifadhi neno usemalo,ni wale ulioambatana nao kiroho.Biblia inamuelezea vizuri sana mzee Yakobo jinsi alivyo ambatana na Yusufu kijana wake mdogo aliyempata enzi ya uzee wake.(Mwanzo 37 :3)

Mfano mzuri wa muambatano wa kiroho ni Elisabeth na Mariamu
Tazama pale Mariamu alipomwendea Elisabeth;
Biblia inasema ;

"Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu,kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake;Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;"Luka 1:41

Haleluya...

Kulikuwa na muunganiko mkubwa wa kiroho baina ya nguvu ya Mungu iliyokuwapo ndani ya tumbo la Mariamu na nguvu iliyokuwapo ndani ya tumbo la Elisabeti.Huu ni mfano mmojawapo wa muunganiko wa kiroho wa kipekee/A very completely spiritual bond.

Muunganiko kama huu ndio ulimfanya Yakobo aweze kutunza neno la Yusufu kwa kile ambacho Yusufu alichokiota....

ITAENDELEA...

*Ikiwa bado hujaokoka,Basi bado hujachelewa kabisa,maana muda wenyewe ndio sasa;
piga namba hii na BWANA atakwenda kukuhudumia;
0655-111149.

Usikose fundisho hili mahali hapa hapa,maana yamkini yapo MAONO au NDOTO kwako,na unapenda kuyajua maana yake.Kupitia mafundisho haya,yatakupa msukumo wa kuanza upya kumuuliza Bwana Mungu,naye Bwana atayafunua MAONO na NDOTO hizo.

UBARIKIWE.

No comments:

Post a Comment