Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Sunday 16 March 2014

PIRLO AIPAISHA ZAIDI YA KILELENI JUVE SERIE A

MKONGWE Andrea Pirlo ameiwezesha Juventus kupaa kwa pointi 17 zaidi kileleni mwa Serie A kufuatia bao lake pekee la ushindi dakika ya 89 kwa mpira wa adhabu wakiilaza Genoa 1-0.
Mabingwa hao watetezi walikutana na mchezo mgumu Uwanja wa Luigi Ferraris mbele ya Genoa, lakini walipambana hadi mwishoni mwa mechi hiyo Pirlo alipofunga bao linalozidi kuwakatisha tamaa, Roma walio katika nafasi ya pili ambao wanacheza leo.
Mechi nyingine za jana usiku, Fiorentina iliilaza mabao 3-1 Chievo Uwanja wa Artemio Franchi na AC Milan ikalala 4-2 nyumbani mbele ya Parma.

Shujaa: Wachezaji wa Juventus wakimpongeza Pirlo baada ya kufunga bao la ushindi dhidi ya Genoa katika mchezo wa Serie A jana
Utu uzima dawa: Andrea Pirlo akishangilia baada ya kufunga kwa mpira wa adhabu

No comments:

Post a Comment