Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Tuesday 18 March 2014

KLABU ya Real Madrid imeungana na wapinzani wao nchini Hispania, Barcelona kutinga Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kufuatia ushindi wa mabao 3-1 usiku huu Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid ambao unawafanya wasonge mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 9-2 dhidi ya Schalke ya Ujerumani.

Mabao yaliyoipeleka Madrid Nane Bora ya Ligi ya Mabingwa yamefungwa na Cristiano Ronaldo mawili dakika za 21 na 74 akifikisha mabao 41 msimu huu, na lingine limefungwa na Alvaro Morata dakika ya 75.
Madrid ilishinda 6-1 katika mchezo wa kwanza ugenini, hivyo imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 9-2.

Mkali kweli: Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid ikiilaza 3-1 Schalke
Mchezaji ghali duniani, Gareth Bale akimkumbatia Ronaldo baada ya kuitumia pasi yake vyema kufunga

No comments:

Post a Comment