Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Friday 8 November 2013

Hizi ni picha 7 za kinachoonekana ndani ya video mpya ya Shilole ‘nakomaa na jiji’


Video mpya ya hii single ya Shilole – ‘nakomaa na jiji’ itakuepo on millardayo.com usiku huu mtu wangu.











NIGERIA U17 MABINGWA WA DUNIA 2013

Wachezaji wa U17 wa Nigeria wakishangilia na kombe lao la dunia baada ya kuifunga Mexico mabao 3-0 kwenye fainali iliyopigwa Uwanja wa Mohammad Bin Zayed, Abu Dhabi jana.

Tanzanite Yatua Salama Maputo Kikosi cha timu ya Taifa ya wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite) kimewasili salama


Kikosi cha timu ya Taifa ya wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite) kimewasili salama jijini Maputo, Msumbiji tayari kwa mechi ya marudiano ya raundi ya kwanza ya Kombe la Dunia itakayochezwa kesho (Novemba 9 mwaka huu).

UHAI CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI NOV 17



Michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 wa klabu za Ligi Kuu inaanza kutimua vumbi Novemba 17 mwaka huu katika viwanja vya Karume na Azam Complex, Dar es Salaam.

Droo ya michuano hiyo inayodhaminiwa na Maji Uhai imefanyika leo (Novemba 8 mwaka huu) mbele ya waandishi wa habari katika ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambapo timu zimepangwa katika makundi matatu.

Kundi A linaundwa na timu za Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Mbeya City na Yanga, wakati kundi B ni Ashanti United, Mgambo Shooting, Oljoro JKT na Ruvu Shooting. Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, Rhino Rangers na Tanzania Prisons ndizo zinazounda kundi C.

Mechi za ufunguzi kundi A Novemba 17 mwaka huu ni kati ya Azam na Coastal Union (saa 2 asubuhi- Karume), Yanga na Mbeya City (saa 8 mchana- Karume). Kundi B ni Ruvu Shooting na Ashanti United (saa 4 asubuhi- Karume), Oljoro JKT na Simba (saa 10 jioni- Karume).

MWISHO WA UTEJA WA MIAKA 10 WA ARSENAL KWA MAN UNITED UMEWADIA?



ILIKUWA Novemba 28, mwaka 2011, Arsenal ilipoondoka imetota vibaya Uwanja wa Old Trafford ikitandikwa mabao 8-2, siku ambayo Wayne Rooney alifunga Hat-trick na Ashley Young akafunga mawili. Danny Welbeck pia alifunga.

Thursday 7 November 2013

AZAM FC NA KOCHA WAKUBALI KUACHANA; YASEMEKANA JUMA KASEJA AMEJIUNGA YANGA




Taarifa za kipa nyota, Juma Kaseja kutua Yanga zimewachanganya watu wengi. Ingawa zimekuwa hazina uhakika, lakini Salehjembe imepata taarifa za uhakika kwamba mchana huu ndiyo amemalizana na Yanga. Lakini bado watu wamekuwa wakihaha kutaka kujua kuhusiana na suala hilo.

Mmoja wa viongozi wa Yanga alisema; "Sitaki kulizungumzia kwa sasa, kama kuna walioandika sawa, lakini kumalizana

YANGA YAUA 3-0 NA KUPAA KILELENI LIGI KUU BARA, AZAM 3-3 NA MBEYA CITY CHAMAZI



Mpira nyavuni; Bao la kwanza la Azam leo Chamazi

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
YANGA SC imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku Azam FC ikitoka sare ya 3-3 na Mbeya City, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, mabao ya Yanga yalifungwa na Simon Msuva dakika 23, Mrisho Ngassa dakika ya 23 na Jerry Tegete dakika ya 53.
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, hadi mapumziko, timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1, Azam wakitangulia kupata bao kupitia kwa Humphrey Mieno dakika ya 13 na Mbeya City wakasawazisha kupitia kwa Mwagane Yeya 'Morgan' dakika ya 30.



Ngassa ameifungia Yanga Taifa leo

Mabao yote yalitokana na mipira ya pembeni, Mieno akifunga kwa kuunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu uliopigwa na Farid Mussa nje kidogo ya 18, kufuatia kipa David Burhan kudakia nje ya eneo lake na Mwagane aiunganisha krosi ya Deus Kaseke.

Wednesday 6 November 2013

MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA ARSENAL YAIKALISHA BORUSSIA DORTMUND, ETO'O APIGA MBILI CHELSEA IKIUA WAJERUMANI...MESSI KAMA KAWA, AIPIGIA MBILI BARCA IKIINYANYASA AC MILAN ULAYA



Zama za ushindi: Aaron Ramsey (kulia) na Mesut Ozil wakishangilia bao pekee la ushindi la Arsnal

BAO pekee la Aaron Ramsey dakika ya 62, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya wenyeji Borussia Dortmund nchini Ujerumani.

Hilo linakuwa bao la 13 kwa mchezaji huyo msimu huu na bao la tano katika michuano ya Ulaya msimu huu. Pamoja na kufungwa, wenyeji ndio waliocheza vyema usiku huu na kabla ya Arsenal kupata bao lake, hawakuweza kutengeneza nafasi hata moja ya kufunga.

ABDI BANDA- COASTAL UNION NI TIMU NZURI TU



Na BARAKA MBOLEMBOLE
Kiungo- mlinzi wa timu ya soka ya Coastal Union, Abdi Banda, amesema kuwa timu yao ni nzuri kila idara, lakini wamekosa bahati tu katika ufungaji wa mabao. Banda aliyasema hayo kabla ya mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu Tanzania Bara, ambao klabu yake ilipoteza katika uwanja wa Chamanzi, dhidi ya timu ya JKT Ruvu.

WENGER AWAAMBIA ARSENAL WASUBIRI KUHUSU KUONGEZA MKATABA



KOCHA Arsene Wenger atawataka Arsenal wawe na subira juu ya mustakabali wake katika klabu hiyo hadi watakapofuzu kwa hatua ijayo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Pamoja na hayo, Arsenal wanajiamini kwamba Wenger atasaini Mkataba a kuendelea kufanya kazi ambao utamuwezesha kupata Pauni Milioni 7.5 kwa mwaka Mfaransa huyo.

Tuesday 5 November 2013

NAHODHA SIMBA SC AISUBIRIA ASHANTI





NAHODHA wa Simba, Nassor Masoud ‘Chollo’ amesema kikosi chake kipo kamili kuweza kuivaa Ashanti United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Bara keshokutwa Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba inaingia katika mchezo huo huku ikiwa inashika nafasi ya nne ikiwa na pointi 21 baada ya mechi 12, wakati Ashanti yenyewe ina pointi 10 ikiwa katika nafasi ya 11 baada ya kucheza mechi 12 pia.
Ashanti ni miongoni mwa timu tatu zilizopanda msimu huu wa Ligi Kuu huku nyingine zikiwa ni Mbeya City na Rhino Rangers ya Tabora, imeonyesha kuzinduka katika ligi hiyo baada ya kuanza kwa kusuasua hapo awali.
Akizungumza na mtandao huu, Chollo amesema anaamini wachezaji wenzake wapo tayari kwa mchezo huo ambao ni muhimu kwao kuweza kujiongezea pointi muhimu ambazo zitaiwezesha timu hiyo kupaa kutoka nafasi ya nne wanayoshika sasa.

Sunday 3 November 2013

ANGETILE OSIAH MALABEJA ANG'OLEWA TFF, WAMBURA ANAKAIMU NAFASI YAKE



Na Mahmoud Zubeiry, Posta
KIKAO cha kwanza cha Kamati mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) jana chini ya Rais, Jamal Emil Malinzi kimemuengua Katibu Mkuu wa kuajiriwa, Angetile Osiah Malabeja.
Rais Malinzi, alifungua kikao kwa ajenda ya kumuengua Angetile na Wajumbe wakaafiki, lakini wanamng'oa kistaarabu.
Angetile amepewa likizo ya hadi atakapomaliza Mkataba wake mwezi ujao na kwa sasa, aliyekuwa Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface Wambura Mgoyo atakatimu nafasi yake.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI