Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 26 October 2013

NEY WAMITEGO APIGWA MARUFUKU KUVAA MLEGEZO JUKWANI NA BASATA


Ney wa Mitego ambae ni staa wa single za ‘muziki gani’ na ‘salamu zao’ amethibitisha kupewa barua na baraza la sanaa Tanzania ikiwa ni onyo la kutoendelea kuvaa suruali mlegezo kwenye majukwaa mbalimbali anayoonekana.

Kwenye interview yake na millardayo.com Ney amesema alipigiwa simu sana na namba moja lakini alikua amelala, alipoamka akakuta missedcalls nyingi so ikabidi apige ndio akaambiwa BASATA kuna barua yake ambapo baada ya kushindwa kwenda alipelekewa Manzese.

Hawa ndio washindi wa Fiesta Super Nyota 2013


Kwenye Super Nyota ya mwaka jana 2012 washindi walikua ni Ney Lee kutoka 87.8 Mbeya pamoja na Young Killer kutoka 88.1 Mwanza lakini mwaka huu washindi ni hawa Eddy Boy kutoka Mwanza pamoja na K Style na

DIAMOND PLATNUMZ kufanya remix ya NUMBER ONE na DAVIDO


I said NGOLOLO Dance

PICHA ZA NANI MATANI JEMBE JIJINI MBEYA

Wasani wa kundi la chacharito group wakiwaburudisha wateja katika kampeni ya nani matani jembe kupitia bia yake ya kilimanjaro premiu lager inayo washindanisha mashabiki wa yanga na simba promosheni hiyo ilifanyika katika bar ya New SITY PUB iliyopo mwanjerwa jijini la Mbeya

Wasani wa kundi la chacharito group wakiwaburudisha wateja katika kampeni ya nani matani jembe kupitia bia yake ya kilimanjaro premiu lager inayo washindanisha mashabiki wa yanga na simba promosheni hiyo ilifanyika katika bar ya New SITY PUB iliyopo mwanjerwa jijini la Mbeya

MATOKEO LIGI KUU ENGLAND, ARSENAL YAENDELEA KUTAKATA ; Liverpool 4 , Manchester United 3



ARSENAL imeibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Crystal Palace katika mchezo wa Ligi Kuu England leo na kuendelea kujinafasi kileleni mwa ligi hiyo.

Mikel Arteta alifunga bao moja kwa penalti dakika ya 47 kabla ya kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa na Olivier Giroud akafunga la pili dakika ya 87.

SOKA, MABINTI WA KIBONGO (TANZANITE) WAWAFUMUA MSUMBIJI 10-0 TAIFA

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
TIMU ya soka ya taifa ya wanawake kwa vijana chini ya umri wa miaka 20, The Tanzanites imeifunga Msumbiji mabao 10-0 katika mechi ya kwanza ya raundi ya Kwanza ya Kombe la Dunia kwa mabinti wa umri huo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni ya leo.
Katika mchezo huo uliohudhuria na mashabiki wachache mno, hadi mapumziko, tayari Tanzanites walikuwa mbele kwa mabao 5-0.

Neema Paul kushoto akishangilia na Theresa Yona baada ya kuifungia bao la kwanza Tanzania katika ushindi wa 10-0 jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Bao la kwanza lilifungwa dakika ya sita na Neema Paul aliyeunganisha pasi ya Theresa Yona, kutoka wingi ya kushoto, wakati mfungaji bora wa michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars iliyofanyika mwaka huu Nigeria, Shelder Boniface alifunga la pili dakika ya 24 baada ya kupangua ngome na kumpiga chenga hadi kipa.
Deonesia Daniel akafunga bao la tatu kwa shuti kali la mpira wa adhabu lililotinga moja kwa moja nyavuni dakika ya 32 na dakika ya 41, Amina Ali akafunga la nne kwa shuti kali kutoka nje ya eneo la mita 18.

Wachezaji wa Tanzania wakishangilia mabao 10-0

BOLLYHOOD, UNAMKUMBUKA ANJALI MTOTO KATIKA KUCH KUCH HOTA HAE

 
Huyu ni yule mtoto aliigiza kama mtoto wa SHAHRUKH KHAN aliyezaliwa kisha mama yake RANI anafariki. Alipofikisha miaka 8 anapewa kitabu alichoachiwa na mama yake kinachohusu hadithi ya baba yake na rafiki wa baba yake KAJOL.

YAHYA MWENYEKITI MPYA BODI YA LIGI, SAIDI MAKAMU MWENYEKITI

Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara, imepata viongozi wapya kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Golden Jubilee Towers, Dar es Salaam.

Katika uchaguzi huo, Hamad Yahya Juma wa Mtibwa Sugar alichaguliwa kuwa mwenyekiti wakati Saidi Mohamed wa Azam alichaguliwa kuwa makamu mwenyekiti.

MAGAZETI YA MICHEZO LEO JUMAMOSI






www.hakileo.blogspot..com

TAIFA STARS YAANZA KUJINOA ADDIS ABABA

NA BONIFACE WAMBURA

Taifa Stars imetua jijini Addis Ababa, Ethiopia leo (Mei 28 mwaka huu) alfajiri kwa ndege ya EgyptAir ambapo itaweka kambi ya wiki moja kujiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco (Lions of the Atlas) itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.

Stars iliyotua na kikosi cha wachezaji 21 imefikia hoteli ya Hilton, na imeanza mazoezi leo (Mei 28 mwaka huu) saa 12 jioni kwenye Uwanja wa Addis.

ANCELOTTI HAJAAAMUA KUHUSU BALE KAMA ATAANZA AU...



KOCHA Carlo Ancelotti hajaamua kama atamuanzisha Gareth Bale katika mechi ya El Clasico kesho, lakini amesema nyota huyo wa Wales yupo tayari.
Mtaliano huyo, akizungumza katika Mkutano wa Real Madrid na Waandishi wa Habari leo mchana amesema kwamba maamuzi yoyote kuhusu Bale atayafanya baada ya mazoezi ya mwisho kuelekea mechi hiyo jioni ya leo kabla ya mechi na Barcelona Uwanja wa Camp Nou Jumamosi jioni.

DEFOE AING'ARISHA SPURS IKIISHINDA FC SHERIFF 2-0



MSHAMBULIAJI Jermain Defoe kwa mara nyingine amedhihirisha hajachuja baada ya kuifungia bao Tottenham katika ushindi wa 2-0 dhidi ya FC Sheriff Tiraspol kwenye Europa League na kuvunja rekodi ya mabao ya Martin Chivers iliyodumu kwa miaka 40 katika michuano ya Ulaya. (HM)

Shujaa wa miaka ya sabini, Big Chiv, mshindi wa Kombe la UEFA akiwa na Spurs mwaka 1972, alisema amefurahi kufikiwa idadi yake ya mabao, 22 na mshambuliaji tegemeo la Spurs hivi sasa.

uchaguzi TFF; NYAMLANI AANZA KAMPENI KWA AHADI TISA ZA KUMMALIZA MALINZI



MGOMBEA nafasi ya U-Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Jumanne Nyamlani amezindua kampeni zake za kuwania ukuu wa shirikisho hilo akipambana na Jamal Malinzi. (HM)
Akizindua kampeni zake jana jijini Dar es Salaam, Nyamlani aliweka wazi jinsi atakavyoendeleza mipango ya sasa ya TFF kwa kuwa alishiriki katika kuiandaa na kuipanga chini ya uongozi wa sasa wa Leodegar Tenga.

Nyamlani anaenda mbali zaidi kwa kuweka pia ahadi zake tisa za kutekeleza endapo atapewa ridhaa ya kuliongoza shirikisho hilo. Miongoni mwa ahadi hizo za Nyamlani ni pamoja na;

Moja: KUIMARISHA USIMAMIZI NA MENEJIMENTI YA SOKA KATIKA NGAZI ZOTE.
Nyamlani anasema akiwa rais wa TFF, kwa kushirikiana na viongozi wa klabu na vyama vya soka vya wilaya na mikoa pamoja na serikali ataimarisha usimamiaji na menejimenti ya soka katika ngazi zote kwa kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa viongozi pamoja na kusimamia sheria na taratibu za uendeshaji wa soka Tanzania.

PINTO AAHIDI KUBORESHA SOKA TANZANIA AKICHAGULIWA TFF



MWENYEKITI wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Abbas Pinto ametoa taarifa kwa vyombo vya Habarii juu ya sababu za kuwania kwake Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), hii hapa;
"Ndugu waandishi nagombea nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji katikauchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupitia Kanda ya Pwani na Morogoro na nimeamua kugombea nafasi hiyo ili kuleta mabadiliko ya kweli na kuleta fikra endelevu.

Mark Hughes aiponda klabu yake ya zamani Manchester United dhidi ya Stoke City


Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Manchester United Mark Hughes ambaye kwa sasa anainoa Stoke City
bbc.co.uk
Na Martha Saranga Amini
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Manchester United Mark Hughes anaamini klabu hiyo ni dhaifu kidogo wakati huu ikiandaa kuikabilia Stoke City jumamosi katika ligi ya mabingwa katika uwanja wa Old Trafford.
Meneja mpya David Moyes amejihakikishia mwanzo mzuri tangu aliziba pengo la Alex Ferguson katika msimu wa mwisho huku upande wake akipoteza alama 13 katika mechi 8.

Mwamuzi wa mchuano Manchester City na CSKA Moscow kuondolewa kibaruani baada ya kushindwa kudhibiti ubaguzi wa rangi


Kiungo mshambuliaji wa Man City Yaya Toure amelalamika kufuatia kelele za kejeli kutoka kwa mashabiki wa SCKA Moscow ya Urusi ambazo hazikuchukuliwa hatua yoyote na Mwamuzi wa mchuano.
RFI
Na Martha Saranga Amini

Mwamuzi aliyesimamia mchuano wa Manchester City dhidi ya CSKA Moscow ametakiwa kuondolewa kibaruani baada ya kushindwa kudhibiti tabia mbaya inayolalamikiwa katika viwanja vya michezo ya Ubaguzi wa rangi.
Kiungo mshambuliaji wa Man City Yaya Toure alilalamika Ovidiu Hategan kuhusu maneno ya kejeli za kiubaguzi wa rangi kutoka kwa mashabiki wa CSKA katika mchuano wa ligi ya mabingwa iliyofanyika nchini Urusi.

histoia leo,SIKU BOLI ZOZO ALIPOIBUKIA JANGWANI! (YANGA NA SIMBA1994)

Kikosi cha Yanga cha mwaka 1994. Kutoka kushoto waliosimama ni Salum Kabunda 'Ninja', Constantine Kimanda, Steven Casmir Nemes, Kenneth Pius Mkapa, Selemani Mkati. Waliochuchumaa kutoka kushoto ni Nico Bambaga 'Machine', Sekilojo Chambua, Edibily Lunyamila, James Tungaraza 'Boli Zozo', na Said Mwamba 'Kizota'.
Na Daniel Mbega
YOUNG Africans, ambayo mwaka 1993 iliteswa sana na wapinzani wake wa jadi, Simba, baada ya kutamba misimu miwili ya nyuma, hatimaye Jumamosi Februari 26, 1994 iliingia kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwakabili ‘wanyama hao wakali’ wa Msimbazi, ambao mwaka huo walikuwa wameongeza makucha yao kwa kuwasajili wachezaji mahiri na wauaji wa mabingwa hao watetezi wa Tanzania Bara, Yanga.

Thursday 24 October 2013

SOMA HII,Picha 10 za mashabiki wa Diamond wakiwa na mavazi / mapozi kama yeye


Hakika Diamond ana mashabiki wanaomkubali na kufatlia kila akifanyacho kuanzia mavazi mpaka mapoz ya picha zake. leo hii kupitia ukurasa wakw wa instagram amepokea picha tisa baada ya kuuliza swali hili

Unahisi una picha yoyote ambayo imefanana na yangu kwa Poz ama hata Mavazi.. it doesn't matter if you are a Boy or Girl....Now ambatanisha kama hivi halaf Hash tagg neno #Minadiamond itanifikia halaf ntaipost na kuku Cc: hapa kila mtu aone na Kucomment.... kumbuka ni #Minadiamond #Minadiamond.

JE,WAJUA ? Mzee Majuto ameutaja Mshahara wake wa movie kwa mwezi hapa


Ni nadra sana kwa Mastaa wengi wa Tanzania kukubali kusema kiwango anachopata kwa mwezi kutokana na kazi yake ya umaarufu ila kwa Mzee Majuto ni kinyume, amekubali kusema kila kitu kwenye kipato cha movie zake za vichekesho ambazo mpaka sasa ndio zinashika namba 1 kwa mauzo Tanzania?

VIONGOZI WA VILABU VYA LIGI DARAJA LA KWANZA KUWENI MAKINI NA UCHAGUZI WA BODI YA LIGI,MNAPIGWA CHANGA LA MACHO.




Uchaguzi wa viongozi wa bodi ya ligi unataraji kufanyika leo, ila kuna ubabaishaji mkubwa kwenye mchakato huu wa uchaguzi na kama ingekuwa ni uwezo wangu basi ningelisimamisha zoezi hili mpaka pale taratibu zitakapofuatwa.

Wednesday 23 October 2013

DOGO JANJARO: SIJAFUKUZWA NA OSTAZ JUMA ILA NIMEJITOA MWENYEWE MTANASHATI


Janjaro msanii kutoka Arusha lakini makazi yake yapo Dar amefunguka na DJCHOKAblog kuwa hajafukuza na Ostaz Juma Namusoma kwenye kampuni yake ya Mtanashati bali amejitoa mwenyewe kwa hiari yake. Janjaro amesema amechoka na matendo tu ya Ostaz na alikuwa tu akiyavumilia lakini kwa sasa ameshakuwa mkubwa so nataka nikae kivyangu vyangu nifanye mambo yangu kama wasanii wengine ambao hawana meneja na wanafanya poa. Namnukuu Janjaro akisema...

Yanga watoa kali ya mwaka,WAKATA RUFA


Na Doris Maliyaga, Mwananchi
Tukio la kwanza la vurugu lilitokea Dar es Salaam baada ya kumalizika mechi ya Yanga dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa.

Mbeya.
 Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wamekata rufaa kwa kamati ya Ligi kutaka mchezo wao dhidi ya Mbeya City uliofanyika Jumamosi iliyopita urudiwe kwenye uwanja huru.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine ulimalizika kwa sare ya 1-1 na kufanikiwa kuingiza Sh100 milioni baada ya mashabiki 20,000 kushuhudia mechi hiyo.

Kabla ya mchezo huo kuanza kulitokea vurugu za mashabiki baada ya mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa Mbeya City kulipiga mawe basi la Yanga wakati linaingia uwanjani pamoja na gari dogo aina ya Noah lililokuwa limebeba viongozi wa Yanga nalo lilipigwa mawe na kioo cha nyuma cha gari kuvunjika.

AMA KWELI MBUZI WA MASIKINI HAZAI, DOGO JANJA ATIMULIWA MTANASHATI ENTERTEAINMENT,kisa Bangi na Pombe.

Abdulaziz Chende 'Dogo Janja'.
Msanii chipukizi wa muziki wa Hip Hop, Abdulaziz Chende maarufu kwa jina la Dogo Janja, ametimuliwa katika kundi la Mtanashati Entertainment.
Baadhi ya mashabiki wa Dogo Janja wakati wakimsubiri Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Juni 22, 2012.

WAGOSI WAIBANA SIMBA MBAVU HUKU YANGA IKICHINJA.

Yanga SC leo imeweka kimbindoni pointi tatu baada ya kuichabanga mabao 3 - 0 timu ya Rhino Rangers kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Hamis Kiiza aliyefunga mawili katika dakika ya 12 na 81 wakati lingine likifungwa na Frank Domayo mnamo dakika ya 72.

Wakati Yanga wakitoka vifua mbele leo, watani wao Simba SC wao wameshikwa sharubu baada ya kulazimishwa sare ya 0 - 0 na Coastal
Wachezaji wa Simba SC, Haruna Shamte (kushoto) na Joseph Owino wakijadiliana jambo baada ya sare ya 0-0 dhidi ya Coastal Union leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga. (Picha na Richard Bukos / GPL,TANGA).

Yanga SC leo imeweka kimbindoni pointi tatu baada ya kuichabanga mabao 3 - 0 timu ya Rhino Rangers kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Hamis Kiiza aliyefunga mawili katika dakika ya 12 na 81 wakati lingine likifungwa na Frank Domayo mnamo dakika ya 72.

Wakati Yanga wakitoka vifua mbele leo, watani wao Simba SC wao wameshikwa sharubu baada ya kulazimishwa sare ya 0 - 0 na Coastal Union ya mkoani Tanga. Mechi hiyo imepigwa katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.

kumekucha,JAMAL MALINZI AZINDUA KAMPENI ZA KUWANIA URAIS WA TFF KWA KISHINDO KIKUBWA



Jamali Malinzi mgombea urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF akizungumza na waandishi wa habari na wadau wa mpira wa miguu  kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro Kempiski jijini Dar es salaam leo ,wakati akizindua rasmi Kampeni zake za kuwania uongozi huo ambapo ameelezea mikakati yake mbalimbali ya kuendeleza soka , hata hivyo ameahidi kuendeleza yote mazuri ambayo yamefanywa na uongozi unaomaliza muda wake chini ya Leodger Tenga.

JAMAL MALINZI AJIPANGA UCHAGUZI TFF,SASA ATO ILANI YAKE,ISOME KWAUNDANI ZAIDI




UCHAGUZI WA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF) 2013
ILANI YANGU YA UCHAGUZI
Utangulizi
Ndugu zangu,

Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema aliyetulinda na kutuwezesha kufika hapa tulipo.

Tarehe 19 Novemba 2009 Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati anazindua ziara ya Kombe la FIFA la dunia uwanja wa Taifa, Dar Es Salaam pamoja na mambo mengine alisema, namnukuu:
‘‘Kwa Watanzania wenzangu tuichukulie ziara ya Kombe la Dunia nchini mwetu kama ni changamoto kubwa kwetu inayotutaka tufanye vizuri zaidi katika soka ili tulingane na heshima hii tuliyopewa. Hasa ni changamoto kwa viongozi wa soka wa ngazi zote pamoja na wachezaji na wapenzi wa mpira wa miguu nchini. Kuja kwa kombe hili ni deni kwetu na kulilipa kwetu sisi ni kuzinduka, tuendeleze kiwango chetu cha soka nchini ili na sisi siku moja TUSHIRIKI FAINALI ZA KOMBE HILI(msisitizo ni wa kwangu). Hili jambo linawezekana. Wapo wenzetu Afrika wameweza, kwa nini sisi tusiweze? Wao ni watu kama sisi, maadam wameweza na sisi tutaweza.

Picha: Kanye West amvisha pete Kim siku ya birthday yake, akodisha uwanja mzima wa baseball kwa dola

HABARI NA DJ FETTY BLOGU
Kanye West atoa bonge la surprise kwa mama mtoto wake Kim Kardashian kwenye birthday yake ambayo ilikua ni siku ya jumatatu ya jana ( October 21) baada ya kumuomba amuoe na kumvisha pete ya Diamond(sio diamond msanii) yaani almasi, yenye Carate 15 katika uwanja wa baseball wa AT&T, Francisco.

Kutana na picha 7 za utengenezwaji wa video mpya ya Madee ‘Tema mate tumchape’


HABARI NA MILLARD AYO WEB.
Baada ya kuvunja rekodi kwa mara ya kwanza kwa single yake ya ‘Pombe yangu’ iliyokaa kwa wiki zaidi ya 30 kwenye Clouds FM Top 20 ikiwa ni single iliyomuingizia zaidi ya milioni 130 kutokana na showz, staa kutoka Manzese Madee ametoa single yake mpya siku kadhaa zilizopita inaitwa ‘tema mate tumchape’ ft Raymond.

fumanizi,MKE, MUME WA MTU WANASWA GESTI SAA 7 USIKU

HABARI NA MTANDAO WA GLOBAL PUBLISHER.
Stori: Mwandishi Wetu
ILE Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers imeshuhudia mume wa mtu aliyejitambulisha kwa jina la Emmanuel Benedict na mke wa mtu aitwaye Rehema ambao wamenaswa laivu wakifanya ‘mambo’ gesti.

Live: Mume wa mtu, Emmanuel Benedict na mke wa mtu aitwaye Rehema baada ya kunaswa gesti saa 7 usiku.

Wawili hao walinaswa hivi karibuni kwenye gesti ambayo pia ina baa iitwayo Blue Roze maeneo ya Buguruni-Sokoni jijini Dar wakijiachia kwa raha zao.

Habari zilizopenyezwa katika timu yetu ni kwamba, baa hiyo hutumia vibaya leseni yake ya biashara kwa kugeuza gesti hiyo danguro ambapo machangu hufanya biashara ya kuuza miili yao katika eneo hilo.

Aibu: Emmanuel na Rehema wakiwa na aibu wakati wakijiandaa kutoka chumbani.

Ilielezwa kuwa baa hiyo huwahifadhi machangudoa ndani yake huku biashara ya ngono ikifanyika mchana kweupe na usiku kucha bila kushtukiwa.

Ligi kuu bara leo,YANGA YAIKARIBISHA RHINO DAR LEO, SIMBA KAZI IPO MKWAKWANI MBELE YA COASTAL



HABARI NA SHAFII BLOGU
YANGA na Simba kwa pamoja leo zinashuka katika viwanja viwili tofauti kupambana na Rhino Rangers na Coastal Union katika muendelezo wa Ligi Kuu ya Bara.
Yanga ambayo ni mabingwa watetezi wenyewe watakuwa jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa, kuvaana na Rhino ya Tabora inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JW).
Kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro amesema vijana wake wamefuta makosa na sasa wapo tayari kuikabiri Rhino Rangers leo.
“Kikosi kipo sawa kupambana na Rhino hapo kesho (leo), kama ni makosa tumeshayafanyia kazi na nadhani tutafanya vizuri zaidi katika mchezo huu na kilichobaki sasa ni muda kufika tuweze kuingia uwanjani,” anasema Minziro.

ALEX FERGUSON AMPONDA DAVID BECKHAM

Aliyekuwa meneja wa klabu ya Manchester United ya Uingereza Sir Alex Ferguson amesema David Beckham alilazimika kuondoka katika klabu hiyo kutokana na tabia yake ya kujiona ni mkubwa kuliko meneja wake.

Katika kitabu kipya kuhusu historia ya maisha yake Ferguson amesema enzi za uongozi wake walitofautiana na Beckham
kutokana na kumkosoa kuhusiana na kiwango chake katika matokeo ya ligi ya FA 2003.


Mchezaji huyo alionekana kuwa na msimamo unaoonyesha kujiona mkubwa na kutokubali maelekezo .

Furguson amesema kuwa tabia ya Beckham ilionekana kubadilika tangia alipomuoa mwanamuziki maarufu wa miondoko ya pop Victoria kutoka kundi la Spice Girls

JANA HIYO,LEWANDOWSKI AITEKETEZA ARSENAL, CHELSEA YAUA LIGI YA MABINGWA, BARCA NA AC MILAN 1-1



BAO la dakika za lala salama la Robert Lewandowski limeipa ushindi wa 2-1 Borussia Dortmund dhidi ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Uwanja wa Emirates usiku huu.

Henrikh Mkhitaryan aliifungia bao la kuongoza Borussia Dortmund, lakini Olivier Giroud akasawazisha ikawa 1-1.



Lakini katika dakika 10 za mwisho, Arsenal ikatepeta na kumruhusu mshambuliaji Lewandowski kuwamaliza nyumbani.

Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Ramsey, Arteta, Wilshere, Ozil, Rosicky na Giroud.



Borussia Dortmund: Weidenfeller, Grosskreutz, Subotic, Hummels, Schmelzer, Bender, Sahin, Blaszczykowski, Mkhitaryan, Reus na Lewandowski.

Monday 21 October 2013

Huyu ndio Baba mzazi wa Madee, na hii ndio kazi ameifanya kwa miaka


Baba mzazi wa Madee Ally Selengia ambae ana zaidi ya 50 sasa hivi lakini bado anaonekana kijana na hata mambo yake mengine ni ya ujana ujana, anayo mpaka a.k.a ya ‘Mwakitoki hoi’ ambayo Madee amekua akisikika akimrusha kwenye nyimbo zake.

Ni mzazi ambae kazi yake kwa zaidi ya miaka 20 ni kuendesha Taxi jijini Dar es salaam kama unavyomuona kwenye picha akiwa na Taxi anayoimiliki, ni biashara ambayo ndio imemuwezesha kuwasomesha kina Madee na kuilea familia kwa miaka yote.

Anasema kwa miaka kadhaa hata mpaka sasa hivi, nyumbani kwake analea baadhi ya Wasanii ambao ni marafiki zake Madee, kwa sababu wanafanya muziki na Madee imebidi akubali hali halisi ya maisha ya mwanae ambapo toka miaka hiyo amewalea watu kama kina MB Dogg yani kama watoto wake, chakula kinapikwa pamoja wanakula na kulala kama familia.

Baba Madee anasema yeye ndio alikua mtu wa kwanza kumkataza Madee kufanya muziki miaka hiyo kwa sababu hakuona faida yake ila kwa sasa ameiona na mpaka amemruhusu mdogo wake Madee wa mwisho kufanya muziki pia mwingine kuwa producer wa video.

WEMA SEPETU KWENYE INSTAGRAM KINACHOMHUSU DIAMOND



Wema Sepetu mwenyewe anajua kwamba watu wengi wanafikiri yeye anawaza kuwa na Diamond hivi sasa, lakini ametoa majibu ya hayo mawazo kwenye hii picha. Maana ya hii picha ni kwamba watu wengi wanafikiri kwamba muda wote Diamond yupo kwenye kichwa cha Wema, lakini yeye mwenyewe anasema kwamba muda wote anafikiria pesa.

JULIO: YANGA KAMA TYSON, WANA NGUVU DAKIKA 25 TU


Ama kweli sare ya mabao 3-3 ya mchezo wa Ligi Kuu ya Bara ulizokutanisha Simba na Yanga imezua mambo, Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’ amesema kikosi cha Yanga kinamudu kucheza vizuri na kwa kasi ndani ya dakika 25, na kwenda mbele inaweza kufungwa idadi yoyote ya mabao.

Katika mchezo huo uliochezwa Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga ilitangulia kufunga mabao 3-0 ndani ya dakika 45 za kwanza, lakini Simba ilirudi kipindi cha pili na kuweza kusawazisha mabao hayo na kumaliza mechi kwa sare ya mabao 3-3.

CANNAVARO, MORRIS WATEMWA TAIFA-KOMBE LA CHALLENJI



KIKOSI cha wachezaji 30 cha timu ya taifa ya Zanzibar kimetangazwa na kocha mkuu wa timu hiyo Salum Bahusi bila ya jina la nahodha wa Yanga, Nadir Haroub Cannavaro na Aggrey Morris wa Azam FC.
Kwa mujibu wa habari kutoka Zanzibar, kikosi hicho ambacho kinatarajiwa kushiriki Kombe la Chalenji kuanzia Novemba 27 mwaka huu jijini Nairobi Kenya, Kocha wa Zanzibar Heroes, Bausi amesema kikosi hicho kitaingia kambini Oktoba 27 mwaka huu na keshokutwa jumatano wachezaji wote walioitwa kikosini watafanyiwa vipimo.

BARCELONA WATUA ITALIA KUIKABILI AC MILAN LIGI YA MABINGWA



KIKOSI cha Barcelona kimewasili mjini Milan leo kwa maandalizi ya mchezo wa Kundi H wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya AC Milan wachezaji wake wakiwa wamependeza kwa mavazi yao ya nadhifu.
Barcelona itameyana na wenyeji wao hao, Milan kwenye Uwanja wa San Siro Jumanne usiku, lakini nyota kama Neymar, Alex Song na Dani Alves walionekana kupendeza zaidi baada ya kutua Italia.

Wakiwa wamepigilia shati kali, suti za nguvu na miwani ya jua, watatu hao walifunika mbaya kiasi cha kuonekana kama nyota wa filamu wakati kikosi cha timu ya Katalunya kinatua mjini humo.

ONAMASHABIKI WALIOZIMIA JANA KWENYE MATCH YA SIMBA NA YANGA,wengi ni wa Yanga yupo pia shabiki "MAMA YANGA"


Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross) limesema watu 21 walianguka na kupoteza fahamu wakati wa mechi ya watani Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Watu walikuwa wakianguka mfululizo kila Yanga ilipofunga bao, likianza bao la Mrisho Ngassa. Baadaye mawili yaliyofungwa na Hamis Kiiza.

MAMA YANGA

BLOGU YA TABASAMU LEO NA MAHABA LEO KUBORESHWA

OSCAR SAMBA,MKURUGENZI WA KAMPUNI YA HAKI-LEO
MKURUGENZI WAKAMPUNI YA HAKI-LEO, OSCAR SAMBA AMEHAIDI KUZIPBORESHA BLOGU ZAKE ZOTE ZIKIWEMO BLOGU MBILI WASHIRIKA AMBAZO NI TABASAMU LEO NA MAHABALEO.

NDG OSCA AMEYASEMA HAYO MAPEMA LEO MCHANA WAKIKATI AKIZUNGUMZA NA MWANDISHI WETU OFISINI KWAKE MAENEO YA KWA MORROMBO MKOANI ARUSHA.

IMEBAINIKA YA KWAMBA UBORESHAKI HUWO UTAHUSISHA UANDISHI WA MAKALA MOTO MOTO ZA KIMAPENZI,MICHEZO NA BURRUDANI YAANI KULINGANA NA SERA ZA BLOGU HUSIKA.

NDG. OSCAR AMEWATAKA WADAU NA WAPENZI WA BLOGU HIZI KUKAA MKAO WA MAPOKEZI YA HABARRI NZURI NA SAHIHI AMBAZO ZITALENGA KUWAHABARISHA,KUWACHANGAMSHA KUWAFURAHISHA NA PIA KUSOGEZA MBELE GURRUDUMU LA MAENDELLEO KWA KUTA MAARIFA NA UJUZI WA KIMAISHA.

IKUMBWUKWE YA KUWA HAKI-LEO PIA INAMILIKI BLOGU NYINGINEZO IKIWEMI HAKI LEO,MAKALA LEO NA MWAKASEGEBIBILIA.
www.tabasamuleo.blogspot.com

makala,MJUWE ZENA MOHAMMED YUSSUPH AKA “SHILOLE”


KUKUA kwa tasnia ya filamu Tanzania kunakwenda sambamba na kuibuka kwa vipaji vipya vya waigizaji mahiri na wenye mvuto kila kukikcha.


Mmoja kati ya Zena Mohamed Yussuf maarufu kama ‘Shilole’ ambaye tangu ajikite katika tasnia hiyo ameweza kuonyesha uwezo na kiwango cha hali ya juu licha ya kuwa amecheza filamu nne ambazo zimeshatoka mpaka sasa .

Kwa wanaofuatilia filamu hizo watakumbuka jinsi alivyofanya kweli katika ‘Fair Desecion’ akicheza na Ray, Johari na wengineo,ikifuatiwa ‘Crazy Of Love’ aliyocheza na Basupa, David Mjata na wengineo, ‘Pigo’ aliyocheza na Cloud na Aunty Ezekieli kabla ya kuibukia katika ‘Bed Rest’ akicheza na Ray, Thea, Johari na Mainda.


Hivi karibuni msani huyo ataonekana katika filamu mpya iliyosheheni nyota kibao katika nyanja mbalimbali nchini ‘Cut Off’ ambayo ipo katika matayarisho ya mwisho mwisho kabla ya kuingia sokoni.