
BAO la dakika za lala salama la Robert Lewandowski limeipa ushindi wa 2-1 Borussia Dortmund dhidi ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Uwanja wa Emirates usiku huu.
Henrikh Mkhitaryan aliifungia bao la kuongoza Borussia Dortmund, lakini Olivier Giroud akasawazisha ikawa 1-1.

Lakini katika dakika 10 za mwisho, Arsenal ikatepeta na kumruhusu mshambuliaji Lewandowski kuwamaliza nyumbani.
Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Ramsey, Arteta, Wilshere, Ozil, Rosicky na Giroud.

Borussia Dortmund: Weidenfeller, Grosskreutz, Subotic, Hummels, Schmelzer, Bender, Sahin, Blaszczykowski, Mkhitaryan, Reus na Lewandowski.