Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Wednesday 23 October 2013

JANA HIYO,LEWANDOWSKI AITEKETEZA ARSENAL, CHELSEA YAUA LIGI YA MABINGWA, BARCA NA AC MILAN 1-1



BAO la dakika za lala salama la Robert Lewandowski limeipa ushindi wa 2-1 Borussia Dortmund dhidi ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Uwanja wa Emirates usiku huu.

Henrikh Mkhitaryan aliifungia bao la kuongoza Borussia Dortmund, lakini Olivier Giroud akasawazisha ikawa 1-1.



Lakini katika dakika 10 za mwisho, Arsenal ikatepeta na kumruhusu mshambuliaji Lewandowski kuwamaliza nyumbani.

Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Ramsey, Arteta, Wilshere, Ozil, Rosicky na Giroud.



Borussia Dortmund: Weidenfeller, Grosskreutz, Subotic, Hummels, Schmelzer, Bender, Sahin, Blaszczykowski, Mkhitaryan, Reus na Lewandowski.



Katika mchezo mwingine, Chelsea imeshinda ugenini mabao 3-0 dhidi ya Schalke yaUjerumani, mabao ya Fernando Torres mawili na Eden Hazard moja.



P.T








Nayo AC Milan imelazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Barcelona katika mechi ya Ligi ya Mabingwa usiku huu Uwanja wa San Siro.



Robinho alitangulia kuwafungia wenyeji bao dakika ya tisa, pasi ya Mbrazil mwenzake, Kaka- lakini Lionel Messi akaisawazishia Barca dakika ya 24 kwa pasi ya Iniesta.
Mechi nyingine, Steaua Bucuresti imetoka 1 - 1 na
Basel, Olympique Marseille imefungwa 2-1 na Napoli, Porto imelala 1-0 mbele ya Zenit, Austria Wien imefungwa 3-0 na Atletico Madrid na Celtic imeshinda 2 - 1 dhidi ya Ajax.

No comments:

Post a Comment