Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 4 January 2014

ARSENAL RAHA KWA KWENDA MBELE, MAN CITY MGUU NJE, NDANI FA

TIMU ya soka ya Arsenal imefuzu kutinga Raundi ya Nne ya Kombe la FA baada ya kuwafunga wapinzani wa London Kaskazini, Tottenham mabao 2-0 Uwanja wa Emirates.
Santi Cazorla alifuga bao la kwanza dakika ya 31 kabla ya Tomas Rosicky kufunga la pili 62.
Tottenham, ambayo ilionyesha kuimarika chini ya kocha mpya, Tim Sherwood, ilizidiwa katika safu ya kiungo na washambuliaji wake Emmanuel Adebayor na Roberto Soldado wakajikuta hawana madhara uwanjani.

Matawi ya juu: Kiungo wa Arsenal, Santi Cazorla akishangilia baada ya kufunga dhidi ya Tottenham
Katika mechi nyingine, Manchester City ikiwa pungufu ya mchezaji mmoja ililazimishwa kwenda kwenye mchezo wa marudiano baada ya bao la Scott Dann kuwapa sare ya 1-1 Blackburn Uwanja wa Ewood Park, kufuatia Alvaro Negredo kutangulia kufunga kipindi ca kwanza

TAKWIMU MBALI MBALI KWA MWAKA 2013 ZA LIGI 5 BORA ULAYA.

AZAM FC WALIVYOKATA TIKETI YA KWANZA YA ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI


Mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Herman Tchetche kulia akipiga mpira uliompita kipa wa Tusker FC ya Kenya, Samuel Odhiambo na kwenda nje sentimita chache kutoka langoni katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mapinduzi usiku wa leo Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam FC ilishinda 1-0 na kuwa timu ya kwanza kufuzu Robo Fainali ya michuano hiyo.


Kiungo wa Tusker, Michael Olonga akiwatoka wachezaji wa Azam

soma hii; LUIS SUAREZ NDIYE MWANASOKA ANAYEONGOZA KWA UBORA MPAKA SASA DUNIANI.


RANGI YA MWAKA 2014 NI ZAMBARAU



Mwaka 2013 umemalizika na tumeanza mwaka mpya wa 2014 tukiwa na matumaini mapya. Kama ilivyo ada kila mwaka huwa kuna rangi inayotawala ambayo kwa kawaida hutangazwa na Kampuni ya Pentone ya nchini Marekani.

WATATU WAOMBEWA ITC SHELISHELI

Shirikisho la Mpira wa Miguu la Shelisheli (SFF) limetuma Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) maombi ya Hati ya Uhamisho ya Kimataifa (ITC) kwa wachezaji watatu wa Tanzania.

SIMBA SC YASHIKWA NA KCC AMAAN, NGOMA DROO

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
SIMBA SC imegawana pointi na KCC ya Uganda baada ya sare ya bila kufungana katika mchezo wa Kundi B, Kombe la Mapinduzi usiku huu Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Kwa ujumla timu zote zilitoshana nguvu na maarifa kwa dakika zote 90 za mchezo huo, huku makipa wote, Ivo Mapunda wa Simba na Magoola Omar wa KCC wakistahili sifa kwa kuokoa michomo mingi ya hatari.
Mabeki wa KCC walimdhibiti vizuri winga machachari wa Simba SC, Ramadhani Yahya Singano ‘Messi’ leo, wakati pia beki Mkenya, Donald Mosoti Omwanwa aliiongoza vyema safu ya ulinzi ya Simba SC.

Kipa wa KCC, Magoola Omar akiruka juu kupangua mpira kichwani kwa mshambuliaji wa Simba, Betram Mombeki jioni hii Uwanja wa Amaan
Matokeo hayo yanazifanya Simba SC na KCC ziendelee kukabana kileleni, kila timu ikiwa na pointi nne baada ya kucheza mechi mbili.

WAAMUZI 11 WAPATA BEJI ZA FIFA


ISRAEL NKONGO,Mmmoja wa waamuzi waliopata beji ya FIFA.

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limewapatia beji waamuzi kumi wa Tanzania kwa mwaka 2014.
Waamuzi wa kati waliopata beji hiyo ni Ramadhan Ibada, Oden Mbaga, Israel Mujuni na Waziri Sheha.
Waamuzi wasaidizi ni Josephat Bulali, Ferdinand Chacha, Hamis Changwalu, John Kanyenye, Ali Kinduli, Erasmo Jesse na Samuel Mpenzu.

YANGA YAANZA KUJIFUA



Mkwasa (mwenye rangi za Bluu) akiongoza mazoezi leo asubuhi katika uwanja wa Bora Mabatini Kijitonyama.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara timu ya Young Africans leo imeeanza kujifua katika viwanja vya bora Mabatini Kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa.

Chelsea yapata hasara England

London, England. Chelsea imepata hasara ya Pauni 49.4 milioni kwa mwaka ulioisha Juni 2013.
Mapato ya Pauni 255.8 milioni ni rekodi kwa klabu hiyo lakini kutolewa katika hatua za makundi za Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita kuliwaathiri.

Thursday 2 January 2014

Alichokisema Zitto Kabwe kuhusiana na Kesi yake Mahakamani, tazama pia jibu alilotoa John Mnyika


Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe leo ameingia kwenye headline kuhusiana na kile alichokiwasilisha kwenye mahakama kuu juu ya kupinga kujadiliwa kwenye kikao cha kamati kuu ya Chadema,Kikao ambacho kilikuwa kikutane kesho.

Kikao hicho kilikuwa na hoja mbalimbali ikiwa ni pamoja na hoja inayomhusu Zitto,Millardayo.com imepiga exclusive interview na Zitto Kabwe mara baada ya kutoka kwenye viwanja vya mahakama hiki ndicho alichokizungumza juu ya shauri lake alilopeleka mahakamani.

‘Tumekwenda mahakamani kwa ajili ya jambo moja tu kutaka haki itendeke kwa sababu mahakaama ndiyo chombo cha juu kabisa kwenye nchi yetu cha kuweza kutenda haki mara baada ya kamati kuu ya chama changu kufanya maamuzi ya kunivua nafasi zangu ambayo niliandikiwa makosa 11′

MKWASA, PONDAMALI, KUINOA YANGA




Uongozi wa Young Africans SC umepata warithi wa nafasi tatu za benchi la ufundi (Charles Boniface Mkwasa, Juma Pondamali na Dr. Suphian Juma), huku wakiendelea na mchakato kumpata kocha mkuu ambaye atachukua nafasi ya mholanzi Ernie Brandts aliyesitishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2013.

HATIMAE TOM HUDDLESTONE ATIMIZA AHADI YA KUZINYOA NYWELE ZAKE.

Kiungo wa Hull City Tom Huddlestone ametimiza ahadi yake ya kunyoa nywele zake iwapo angefunga bao baada kukaa miaka miwili na nusu bila kufunga,kiungo huyo aliifungia timu yake bao moja kwenye mchezo ambao timu yake iliifunga Fulham mabao 6-0.





FRANK LAMPARD & BRANISLAV NJE MWEZI MMOJA!!



Nyota wa Chelsea Frank Lampard na
Branislav Ivanovic watakuwa nje kwa Mwezi
mmoja baada kuumia kwenye Mechi na
Liverpool ambayo walishinda 2-1 Uwanjani
Stamford Bridge hivi Juzi.

Wednesday 1 January 2014

LIONEL MESSI AUPANDA MLIMA KILIMANJARO.









WANACHAMA WAMTAKA RAGE KUACHA UBABE



MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage, ametakiwa kuacha ubabe na kujipima katika uongozi wake, ikiwa ni pamoja na kuitisha mkutano wa dharura badala ya kukejeli na kuonyesha umwamba. 

RAY AONA AIBU KUMBUSU LULU


STAA wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ amesema alipata wakati mgumu kumpanga mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwenye filamu yake ambayo walipaswa kucheza kama wapenzi kwa kuhofia kumbusu

YAYA TOURE AING'ARISHA MAN CITY ENGLAND Pia ARSENAL imeua 2.0

KLABU ya Manchester City imeanza vyema mwaka 2014 baada ya mabao ya kipindi cha pili ya Yaya Toure na Aleksandar Kolarov kuwapa ushindi wa 3-2 dhidi ya Swansea huo ukiwa ushindi wa tano mfululizo katika Ligi Kuu ya England.

DIEGO COSTA: RONALDO NDIO ANASTAHILI KUTWAA BALLON D'OR

Mshambuliaji wa Atletico Madrid Diego Costa amesema angependelea tuzo ya Ballon d'Or iende kwa Cristiano Ronaldo mwaka huu.

Ushindani wa tuzo hiyo mwaka huu ni mkubwa sana, huku mshambuliaji huyo wa Real Madrid na Ureno - ambaye alishinda tuzo hiyo mwaka 2008 - anaungana na mshindi wa mara 4 wa tuzo hiyo Lionel Messi na Frank Ribery.

Monday 30 December 2013

KANUNI YA 24, KUVURUGA MCHEZO

1. Wachezaji na viongozi wa timu itakayosababisha mchezo kuvurugika na hatimaye kuvunjwa, itapoteza mchezo huo hata kama ilikuwa inaongoza kwa magoli na timu pinzani itapewa ushindi wa pointi tatu na magoli matatu, iwapo timu pinzani inaongoza kwa magoli zaidi ya matatu, itabakia na idadi ya magoli hayo iliyokwishafunga.

BASI JIPYA LA AZAM FC "KAMA ULAYA"



Basi jipya la wachezaji wa klabu ya Azam FC ya Dar es Salaam, lililowasili nchini juzi likiwa tayari kusafirishwa visiwani Zanzibar ambako timu hiyo imekwenda kushiriki Kombe la Mapinduzi. Hili ni aina ya mabasi ambayo yanatumiwa na klabu za Ulaya kama Manchester United, Bayen Munich na Barcelona ambalo kwa Afrika Azam inaweza kuwa klabu ya kwanza kulimiliki.

MZUNGUKO WA PILI LIGI KUU NI VITA YA KUSAKA UBINGWA NA KUKWEPA RUNGU LA KUSHUKA DARAJA!!


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
NGWE ya lala salama ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014 unatarajia kuanza kushika kasi januari 25 mwakani.
Kwasasa timu zote 14 zinazoshiriki ligi hiyo zipo katika maandalizi ya vikosi vyao ili kufanya vizuri zaidi ya mzunguko wa kwanza.
Wataalamu wengi wa soka wanasema mzunguko wa pili kama ilivyo kawaida timu zinajigawa katika makundi matatu.

Sunday 29 December 2013

ROSE MUHANDO AWAKUNA WAKAZI WA TANGA UWANJA WA MKWAKWANI



Mwimbaji mahiri wa nyimbo za kiroho a.k.a Injili,na anaetamba na wimbo mpya wa Facebook,Rose Muhando akiwa sambamba na skwadi lake zima wakilishambulia jukwaa vilivyo jioni ya leo ndani ya uwanja wa Mkwakwani wakati wa muendelezo wa tamasha la Krisimasi lililofanyika leo Mkoani Tanga.Tamasha hilo ndio kwa mara ya kwanza linafanyika mkoani humo,limezindundiliwa jijini Dar siku ya Krisimasi ndani ya uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na watazamaji lukuki.Tamasha hilo baada ya kufanyika mkoani Tanga,kesho litafanyika jijini Arusha na baadae mkoani Dodoma likiwajumuisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za Injili.

Baada ya Jaguar kuonyesha hili gari jipya, Prezzo nae kalionyesha lake nje ndani


Unaambiwa wiki moja baada ya staa wa muziki Kenya (Jaguar) kuonyesha gari lake jipya aina ya Jaguar ambalo alionekana nalo alipokwenda kufanya show, zimetoka picha za nje ndani za gari analotembelea rapper CMB Prezzo wa Kenya ambae mara kadhaa waliingia kwenye headlines na Jaguar kwa malumbano mbalimbali ikiwemo kutambiana muziki, mali na uwezo wa kifedha.

NGASSA HATARINI KUKOSA KOMBE LA MAPINDUZI, TYPHOID YAMLAZA

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
MSHAMBULIAJI tegemeo wa Yanga SC, Mrisho Khalfan Ngassa anasumbuliwa na homa ya matumbo, typhoid ambayo inaweza kumfanya akose michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayotarajiwa kuanza wiki hii visiwani Zanzibar.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana, Ngassa alisema kwamba baada ya kuona hali yake si nzuri kiafya juzi alikwenda kupimwa na akakutwa na maradhi hayo.
“Nimepatiwa tiba na sasa hivi nipo katika dozi, nadhani nitahitaji angalau wiki mbili za kupumzika ili niwe sawa kabisa. Kwa ujumla nimekuwa nikijisikia vibaya kwa muda mrefu tu, ila nikawa nakula dawa za kutuliza maumivu,”alisema Ngassa.

Anaumwa typhoid; Mrisho Ngassa anahitaji kiasi cha wiki mbili kupumzika kutokana na kusumbuliwa na homa ya matumbo
Yanga SC wamepangwa Kundi C katika Kombe la Mapinduzi, michuano itakayoshirikisha timu 12, pamoja na mabingwa watetezi, Azam FC, Tusker ya Kenya na Unguja Combine.
Kundi kuna Mbeya City, Pemba Combine, Chuoni na URA kutoka Uganda wakati Kundi B lina timu za Simba SC, KMKM, AFC Leopards ya Kenya na KCC ya Uganda.

CHELSEA YAIKALISHA LIVERPOOL DARAJANI, SUAREZ AFANYIWA 'UNDAVA' KINOMA, SPURS NAYO YAUA 3-0



Shujaa; Samuel Eto'o akishangilia baada ya kufunga bao la ushindi, Chelsea ikiilaza Liverpool 2

KOCHA Mreno Jose Mourinho ametoka na furaha Uwanja wa Stamford Bridge jioni hii, baada ya timu yake, Chelsea kuilaza mabao 2-1 Liverpool katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Shukrani kwake mshambuliaji mkongwe, Samuel Eto'o aliyefunga bao la ushindi dakika ya 34 akimalizia pasi ya Oscar ndani ya sita.
Mabeki wa Chelsea walimchezea 'kindava' mshambuliaji Luis Suarez na akatoka uwanjani bila kufunga bao.

Liverpool ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya nne, mfungaji Skrtel, lakini Edin Hazard akasawazisha dakika ya 17.
Kwa ushindi huo, Chelsea inatimiza pointi 37 na kubaki nafasi ya tatu, wakati Liverpool inabaki na pointi zake 36.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo leo, Tottenham Hotspur imeifunga Stoke City mabao 3-0, wafungaji Soldado dakika ya 37, Dembele dakika ya 65 na Lennon dakika ya 69.



Ushindi raha; Lennon kulia akishangilia Adebayor baada ya kuifungia Spurs katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Stoke leo

TFF YASEMA: RAGE BADO MWENYEKITI HALALI SIMBA



Ismail Aden Rage ndiye Mwenyekiti halali wa Simba ambapo Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imemtaka kuitisha Mkutano Mkuu kwa mujibu wa taratibu za klabu ya Simba. (HM)
Kamati imebaini upungufu kadhaa wa kisheria kwenye uamuzi wa Kamati ya Utendaji ya Simba uliofanywa Novemba 18, 2013 kwa kumsimamisha Mwenyekiti wao. Upungufu huo ni pamoja na ukiukwaji wa Ibara ya 33 ya Katiba ya Simba juu uitishaji wa mkutano, ajenda ya kumsimamisha Mwenyekiti kuwasilishwa kwenye kikao kwa utaratibu wa mengineyo.

ARSENAL YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND nsa CHEALSE YA ICHAPA LIVERPOOL


Home » Unlabelled » ARSENAL YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND
MSHAMBULIAJI Olivier Giroud amemaliza ukame wa mabao katika mechi saba baada ya kuifungia Arsenal bao pekee la ushindi Uwanja wa St James' Park katika mchezo wa Ligi Kuu England.
Giroud alifunga bao hilo pekee dakika ya 65 akimtungua kipa Tim Krul kufuatia krosi maridadi ya Theo.
Kwa ushindi huo, Arsenal inarejea kileleni kwa kufikisha pointi 42 baada ya kucheza mechi 19, ikiishusha Manchester City hadi nafasi ya pili kwa pointi zake 41.

MAGOLIKIPA WA LIGI KUU YA VODACOM WAIFUNGA CLOUDS MEDIA MABAO 3-1.


Wachezaji wa timu ya Clouds Media Group wakifanya mazoezi mepesi kabla ya kuanza kwa mtanange wa kufunga mwaka dhidi ya timu ya magorikipa wanaocheza Ligi Kuu ya soka tanzania Bara.

Mbwiga akijifua.

Kocha mchezaji wa timu ya Clouds Media Group, Mbwiga Mbwiguke (kulia) akiwaongoza wachezaji wenzake katika mazoezi.