Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 5 October 2013

HI HAPA RATIBA YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAMOSI



14:45 Manchester City na Everton
17:00 Cardiff City na Newcastle United
17:00 Fulham na Stoke City
17:00 Hull City na Aston Villa
17:00 Liverpool na Crystal Palace
19:30 Sunderland na Manchester United

HATIMAYE MECHI ZA LIGI KUU KUONYESHWA TBC 1

Azam Media Limited imefanikiwa kukamilisha utaratibu wa ushirikiano na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) utakaowawezesha mashabiki wa kandanda kote nchini kunufaika kwa kuona michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom kila mwishoni mwa juma hadi kukamilika kwa nusu ya msimu wa 2013/14 kupitia TBC1 kwa hisani ya AzamTV.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi (Kamati ya Ligi) wameeleza kuunga mkono utaratibu huu makini.

“Baada ya kupata haki za matangazo ya luninga ya Ligi Kuu ya Vodacom, moja ya shabaha zetu kuu imekuwa ni kuhakikisha kuwa tunafanikiwa kurusha matangazo yanayokidhi viwango vya kimataifa kwa ubora. Ili kufanikisha shabaha hiyo tumewekeza vilivyo katika teknolojia ya kisasa ya vifaa vya matangazo ya nje (Outside Broadcasting) na katika mafunzo kwa watumiaji wa vifaa hivyo. Ninayo furaha kusema kuwa matayarisho yamekwenda vema kiasi kwamba tumejikuta tuko tayari kurusha matangazo ya kiwango cha juu kabla hata ya kuzinduliwa kwa huduma kamili za AzamTV”, alisema Rhys Torrington, Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited.

ADAM NDITI:CHELSEA






Chelsea

Born on 18 September 1994 in Zanzibar, Tanzania, Adam arrived at Chelsea as an Under-13 and can play either left-back or left-wing. It was the more defensive of those roles he filled as the FA Youth Cup was captured in 2012. He was joint-highest youth league appearance maker and played four games for the reserves in 2011/12, his first full-time season which led to a professional contract.

As a schoolboy he amassed 27 youth team appearances, and featured regularly during the 2011 FA Youth Cup run to the semi-final.

Friday 4 October 2013

Kocha wa Timu ya Taifa ya Uingereza Hodgson asema tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia 2014 ipo mikononi mwao



Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Uingereza Roy Hodgson

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Uingereza Roy Hodgson ametamka wazi anauhakika kikosi chake kitafanikiwa kukata tiketi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

Hodgson amesisitiza Uingereza ina nafasi ya kufuzu kwa ajili ya Kombe la Dunia mwaka 2014 iwapo itashinda michezo yake miwili ya kusaka tiketi ya kufuzu kwa fainali hizo zitakazofanyika nchini Brazil.

Kocha huyo wa Timu ya Taifa ya Uingereza amesema kwa sasa amekuwa akiangalia kwa karibu mno michezo yao miwili ya kufuzu Kombe la Dunia itayopigwa baada ya juma moja ili kusaka tiketi hiyo muhimu.

Timu ya Taifa ya Uingereza inatarajiwa kucheza michezo miwili katika ya Montenegro na Poland iliyopangwa kufanyika tarehe 11 na 15 na iwapo itashinda michezo hiyo miwili itakuwa imejipatia tiketi hiyo muhimu.

Nahodha wa Manchester United Nemanja Vidic ataka wachezaji kurejea kwenye kiwango chao ili kupata matokeo mazuri


Nahodha wa Mabingwa Watetezi Nchini Uingereza Klabu ya Manchester United Nemanja Vidic
Nahodha wa Klabu wa Manchester United Nemanja Vidic ametoa wito kwa wachezaji wenzake kuhakikisha wanarejea kwenye hali yao ya kawaida ili waweze kufanya vizuri kwenye mchezo Ligi Kuu dhidi ya Sunderland na kusahau matokeo mabaya waliyopitia. Vidic amesema hatua ya wachezaji kurudi kwenye hali yao ya kawaida itasaidia kupunguza shinikizo linalomkabili Kocha Mkuu David Moyes aliyeshuhudia vichapo viwili mfululizo kwenye Ligi Kuu nchini Uingereza.
Manchester United inashika nafasi ya kumi na mbili kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza baada ya kufungwa na Manchester City kabla ya kupata kichapo cha nyumbani mbele ya West Bromwich Albion.

Thursday 3 October 2013

WEMA DIAMOND WARUDIANA.

Stori: Waandishi Wetu
WACHUMBA wa zamani, Wema Sepetu na Nasibu Abdul ‘Diamond’ ndiyo habari ya mjini kwa sasa, kwamba wawili hao wamerudiana tena kwa kasi kupita ile ya mwanzo,
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Habari zinasema wawili hao walikutana Dubai hivi karibuni  kabla Diamond hajaenda Malaysia na Wema akiwa njiani kuelekea Hong Kong, China ambapo walikula bata kwa sana.
Ikazidi kuelezwa kuwa wameamua kuwa kwenye uhusiano wa siri na lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha mpenzi wa sasa wa msanii huyo wa Bongo Fleva, Penniel Mungilwa ‘Penny’ hajui kitu chochote.

DIAMOND ​AKABIDHI IPAD KWA MSHINDI WA NGOLOLO




Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul "Diamond Platinumz"akimkabidhi Ipad yenye thamani ya shilingi Milioni Tsh 1.2 mshindi wa dansi ya Ngololo Bw.Faudhu Kiobya kupitia ukurasa wa kijamii wa instragram wa Vodacom Tanzania,mara baada ya kumalizika droo ya tatu ya shindano la miito ya simu.Washindi 35 kila mmoja amejishindia Sh 50,000.Anaeshuhudia katikati ni Meneja wa huduma za ziada wa Vodacom Bw.Mathew Kampambe, Chanzo Matina Nkurlu

UJENZI WASIMAMA UWANJA WA KOMBE LA DUNIA

130611205613_sp_itaquerao_reuters_304x171_reuters_nocredit_682c9.jpg
Kazi ya ujenzi katika Uwanja utakaochezewa mechi za kombe la dunia la soka mwaka 2014 nchini Brazil zimesimamishwa baada ya jaji wa mahakama kusema kuna wasiwasi kuhusu usalama.
Uwanja huo wa Arena da Baixada katika jiji la Curitiba ulipangiwa kuchezwa mechi nne za kombe la dunia. Ukarabati wa uwanja huo ulikwishacheleweshwa kwa kipindi kadhaa.

Blatter aendelea kupata upinzani juu ya mpango wake wa kusogeza mashindano ya Kombe la Dunia majira ya joto nchini Qatar



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA Sepp Blatter ameendelea kukumbana na upinzani mkali juu ya pendekezo lake la kutaka kuhamisha mashindano ya Kombe la Dunia ya mwaka 2022 yaliyopangwa kufanyika nchini Qatar wakati wa majira ya baridi. Blatter amependekeza mashindano ya Kombe la Dunia yaliyopangwa kufanyika nchini Qatar kusogeza kutoka majira ya joto hadi yale ya baridi kutokana na wakati huwa joto kuwa kali mno na huenda likawathiri wachezaji.www.tabasamuleo.blogspot.com

Timu ya Taifa ya Misri yaendelea kushusha kichapo kwa Uganda kwenye michezo yake miwili ya kirafiki



Beki wa Timu ya taifa ya Uganda akikabiliana na mshambuliaji wa Misri kwenye mchezo wa kirafiki
Timu ya Taifa ya Uganda imeendelea kuwa vibonde vya kudumu mbele ya Misri baada ya kukabali kichapo cha pili kwenye michezo miwili ya kirafiki iliyofanyika katika kipindi cha siku tatu.
Pharaohs waliendeleza ubabe mbele ya Cranes baada ya kuwachakaza kwa jumla ya magoli 3-0 katika mchezo wa pili wa kirafiki wa kujiandaa na hatua ya mtoano dhidi ya Ghana kusaka tiketi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia.

Rafael Nadal akaribia kushika nafasi ya kwanza kwa Ubora wa Tennis Duniani upande wa Wanaume


Mchezaji Tennis nambari mbili kwa ubora Duniani Rafael Nadal


Mchezaji wa Tennis ambaye ni raia wa Hispania Rafael Nadal huenda akareja kwenye nafasi yakwanza katika orodha ya Wachezaji Bora Wanaume wa mcheo huo baada ya kufanikiwa kutinga hatua ya Robo Fainali ya mashindano ya China Open.
Nadal anayeorodheshwa katika nafasi ya pili kwa ubora wa Tennis upande wa wanaume ametinga kwenye Robo Fainali ya China Open kufuatia kumchakaza bila huruma Philipp Kohlschreiber baada ya kumfunga kwa seti mbili kwa bila.

HISTORIA NA WASIFU WA MISS READS TANZANIA 2013 Hapines Watimanywa

ALIPOFANYA MAHOJIANO NA GAZETI LA MWANASPORTI




Hapines Watimanywa


WAKATI mshindi wa jumla wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka 2011 wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa) Shomari Kapombe akizaliwa mwaka 1994, katika kijiji cha Kishozi, Kagera alizaliwa mtoto wa kike ambaye hakudhaniwa iwapo siku moja angefika mbali kimtazamo, kiakili, kifikra na katika masuala ya ulimbwende.

DAKTARI WA SIMBA ATHIBITISHA KUPONA KWA HENRY NA CHOLO



Henry Joseph

DAKTARI wa Simba, Yassin Gembe amemkabidhi Kocha wa Simba, Abdallah Kibadeni wachezaji wawili kiungo, Henry Joseph na nahodha Nassor Said ‘Cholo’.
Henry mchezaji tegemeo wa kikosi hicho alishindwa kucheza mechi mbili zilizopita kutokana na kusumbuliwa na majeruhi ya mguu pamoja na mkongwe mwenzake, Nassor Said ‘Cholo’ naye amepona ingawa hali ya Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ ndiyo bado haijatengemaa.

MPAMBANO WA MASUMBWI KUFANYIKA PANANDI PANANDI ILALA OKTOBA 26




MPAMBANO mwingine wa masumbwi kufanyika katika ukumbi wa panandi panandi Oktoba 26 mpambano huo wa mchezo wa masumbwi utakaokuwa chini ya uratibu wa Kinyogoli Fondition utawakutanisha mabondia mbalimbali wenye majina na wanaotamba kwa sasa katika anga za masumbwi nchini.
Akizungumzia mchezo huo kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini kutoka kambi ya ilala Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa mpambano huo utawakutanisha bondia Yakubu Maganga atakae zichapa na Ubwa Salumu katika uzito wa kilo 75 huku Seif Ali akipambana na Hassani Labanda

PATA MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA WA ULAYA:





CSKA Moskva 3 - 2 Viktoria Plzeň

Shakhtar Donetsk 1 - 1 Manchester United

Bayer Leverkusen 2 - 1 Real Sociedad

Juventus 2 - 2 Galatasaray

Real Madrid 4 - 0 København

PSG 3 - 0 Benfica

Anderlecht 0 - 3 Olympiakos Piraeus

Manchester City 1 - 3 Bayern München www.tabasamuleo.blogspot.com

Wednesday 2 October 2013

Ferguson akanusha madai ya kwamba anataka kurejea kuifunza Timu hiyo


Kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson akiwasalimia mashabiki

Kocha wa zamani wa Klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson amekanusa taarifa zilizokuwa zimezagaa ya kwamba yupo mbioni kurejea tena kwenye kazi yake ya kuongoza Timu hiyo kutokana na kushuhudia matokeo mabaya kwa klabu yake ya zamani. Ferguson amesema hana mpango wala nia ya kurejea tena kuwa Kocha kwani anaamini kazi yake ameshaifanya ipasavyo na sasa ataendelea kufamnya shughuli nyingine nje ya kuwa mkufunzi.

Kocha huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 71 amesema hawezi akarejea tena nyuma eti kwa sababu Manchester United inashika nafasi ya kumi na mbili kwenye msimamo wa ligi kwani anaamini ipo kwenye mikono salama.

David Moyes atetea uamuzi wake wa kubadili wachezaji kwenye kikosi cha kwanza cha Manchester United


Kocha Mkuu wa Manchester United David Moyes akifanya mkutano wa waandishi wa habari

Kocha Mkuu wa Klabu ya Manchester United David Moyes amejitetea na kusema kwa sasa anaendelea kusaka Kikosi cha kwanza kauli aliyoitoa baada ya kukosolewa vikali na Kocha wa Shakhtar Donetsk Mircea Lucescu aliyesema hakuna sababu ya kubadili wachezaji kila siku. Moyes ambaye amekuwa akipata matokeo mabovu kwenye michezo ya Ligi Kuu nchini Uingereza amejikuta akikosolewa vikali kutokana na tabia yake ya kubadili wachezaji wa kikosi cha kwanza kitu ambacho kinatajwa kuwa chanzo cha matokeo mabaya.

Real Madrid kukosa huduma ya Mshambuliaji wake Gareth Bale kwenye mchezo dhidi ya FC Copenhagen kutokana na majeraha


Timu ya Madaktari wa Real Madrid wakitoa huduma ya matibabu kwa Mshambuliaji Gareth Bale

Kikosi cha Real Madrid kinatarajiwa kukosa kwa mara nyingine huduma na Mshambuliaji wake ghali zaidi duniani Gareth Bale anayekabiliwa na majeraha ya nyamaza za paja na hivyo hatakuwepo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya FC Copenhagen.

Kocha Mkuu wa Nigeria Stephen Keshi asisitiza kuendelea na mkakati wake wa kujenga kikosi imara


Nigerian Head Coach Stephen Keshi
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Nigeria Stephen Keshi akiwa kibaruani
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Nigeria Stephen Keshi ameweka wazi yupo kwenye harakati za kuendelea kuijenga Timu hiyo na hadi kufika sasa bado hajapata Kikosi ambacho anakihitaji.

UWANJA A TAIFA SII SALAMA.







Na Mwandishi Wetu
PAMOJA na tukio kubwa na la hatari la kutisha lililotokea katika nchi jirani ya Kenya, imebainika hakuna tahadhari yoyote iliyochukuliwa katika sehemu za mikusanyiko mikubwa ya watu kama vile Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

ONA UFUSIKA WA WEMA NA AUNT EZEKILEL CHINA.


Na Mwandishi Wetu
LICHA ya mwaka jana kuita vyombo vya habari na kujisafisha baada ya kukaa nusu utupu jukwaani, mastaa wawili wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel wamefanya uchafu wakiwa Hong Kong, China.
Video ya aibu ya wawili hao ilivuja mitandaoni mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwaonesha ‘wakidendeka’ na kufanyiana vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili ya Kitanzania.

Tuesday 1 October 2013

PATA MATOKEO YA CHAPION LEAGUE

FIESTA NI MAJANGA,WALA SIO SEHEMU YA BURUDANI


MAJANGA HAYA! NINGELIKUWA WAZIRI WA VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO...



Basi, Siku ya kwanza tu ya kuingia ofisini ningetoa tamko la kupiga marufuku fiesta zote isipokuwa kwenye misimu ya likizo za wanafunzi. Na kwa masharti, kuwa fiesta kwa watoto chini ya miaka 18 zianze alasiri na kumalizika saa kumi na mbili jioni. Fiesta za usiku iwe ni kwa watu wazima tu.

Tuwe wakweli kwa jamii yetu na Nchi Yetu. Wanaosema ' Twenzetu tukawinde' wanapotosha umma. Ni sawa na kusema pia ' Twenzetu tukawindwe'. Wahenga walinena; mwinda huindwa. Hapo pichani imeandikwa, kuwa bia laki 2 kuwindwa. Ni majanga. Hapa kuna ' wawindaji haramu' wenye kuwaaminisha wenye kuwindwa kuwa wao ndio wawindaji www.tabasamuleo.blogspot.com

IRENE UWOYA ajiuzulu muve BONGO, asema HATA IGIZA TENA

"ww.tabasamuleo.blogspot.com NIMEAMUA KUACHA MAMBO YA MOVIE NA KUWAACHIA WENGINE"

Msanii maarufu wa bongo movie Irene Uwoya ameaacha rasmi kuigiza bongo movie na kuamua kundelea na shughuli zake nyingine kama TV SHOWS.


Kupitia website ya DSTV Irene Uwoya alifunguka na kusema “Nimeamua kuacha mambo ya movie na kuwaachia wengine, haya maamuzi nimeyafanya kama miezi sita iliyopita… Mara ya mwisho kuigiza ni zaidi ya miezi sita iliyopita pia.”
Movie alizocheza mpaka sasa zinafika 40 lakini za kwake ni nne tu na amekiri kwamba kuacha kwake kuigiza hakuta mshushia kipato chake cha siku zote ambapo kwa movie moja ya kwake mwenyewe alikua anaiuza mpaka kwa milioni 35.
source DSTV

Monday 30 September 2013

YANGA YA CHANJA MBUGA SASA KUJENGA UWANJA WA KISAASA MAPEMA.


UJENZI WA UWANJA WA YANGA: TAARIFA KUHUSU MAENDELEO YA MRADI WA UJENZI


LEO tungependa kupitia kwenu kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi wetu wa Uwanja wa kisasa wa mpira katika Jiji la Jangwani kama itakavyojulikana

Mara ya mwisho tuliongea ama kuonana ilikuwa mwezi wa tatu wakati Ndugu zetu wa BCEG walipokabizi Concept design ama Usanifu wa awali na kuanzia sasa tutakuwa tunatoa taarifa za mara kwa mara kuhusu mradi huu. Wahenga walisema UKICHA KUSEMA HUTATENDA JAMBO lakini pia KUKAA KIMYA SANA kunajenga hisia mbaya na kutoa nafasi ya upotoshwaji wa habari.www.hakileo.blogspot.com

NI MOTO ULAYA LEO;ARSENAL, CHELSEA, BARCA, DORTMUND, NAPOLI, AC MILAN…!!!




RAHA NI ARSENAL v NAPOLI, STEAU v CHELSEA, PORTO v ATLETICO, CELTIC v BARCA!

MECHI za Pili za Makundi E hadi H zipo Dimbani leo huku Chelsea wakiwa Ugenini wakisaka ushindi wao wa kwanza baada ya kutandikwa katika Mechi yao ya kwanza, Arsenal wapo Emirates na mtanange mkali sana na Napoli huku Vigogo Barcelona, bila ya Supastaa Lionel Messi, wakiwa Ugenini Uwanja wa Celtic Park ambako Msimu uliopita walinyukwa.(P.T)

RATIBA:

[Saa za Bongo]

Jumanne 1 Oktoba 2013

[Saa 1 Usiku]
www.hakileo.blogspot.com

Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers ajivunia Suarez na Sturridge.



Washambuliaji wa Klabu ya Liverpool Daniel Sturridge na Luis Suarez wakishangilia moja kati ya magoli matatu waliyoshinda dhidi ya Sunderland
Na Nurdin Selemani Ramadhani

Kocha Mkuu wa Liverpool Brendan Rodgers ameibuka na kusifu timu yake ndiyo yenye safu hatari zaidi ya ushambuliaji na hili limekuja kutokana na ushindi alioupata kwenye mchezo dhidi ya Sunderland huku washambuliaji wake wawili wakifunga magoli yao matatu.www.tabasamuleo.blogspot.com

Barcelona kukosa huduma ya Lionel Messi


kwa kipindi cha majuma matatu baada ya kuumia nyama za paja





Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi akishangilia moja ya magoli aliyofunga dhidi ya Ajax

Klabu ya Barcelona ya nchini Hispania inatarajiwa kukosa huduma ya Mshambuliaji wake wa Kimataifa wa Argentina na Mchezaji Bora wa Dunia Lionel Messi kwa kipindi cha majuma matatu kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyama za paja.

Maumivu ya Messi aliyapata kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Almeria ambapo Barcelona walifanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0 na hivyo kuendelea kujiwekea mazingira mazuri ya kutetea Ubingwa wao msimu huu.www.tabasamuleo.blogspot.com

WENGER AWAKOROMEA WACHEZAJI WAKE.




Kocha Mkuu wa Arsenal Arsene Wenger akizungumza na wanahabari na kutoa onyo kwa wachezaji wake kabla ya mchezo dhidi ya Napoli
Na Nurdin Selemani Ramadhani

Kocha Mkuu wa Vinara wa Ligi Kuu nchini Uingereza Arsenal, Arsene Wenger ametoa onyo kwa wachezaji wake kuwa makini kwenye mchezo wao wa siku ya jumanne wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya watakapovaana na Napoli kutoka nchini Italia. Wenger amewataka wachezaji wake kuwa na tahadhari kwa ajili ya mchezo huo kutokana na kiwango cha Napoli kuwa kizuri na iwapo hawatakuwa makini basi huenda wakapoteza mchezo huo utakaopigwa nyumbani kwao huko kwenye Dimba la Emirates.www.tabasamuleo.blogspot.com

Roberto Mancini huenda akapewa kibarua cha kuinoa Galatasaray iwapo atakubaliana na Uongozi kwenye mazungumzo yanayoendelea






Kocha wa zamani wa Manchester City Roberto Mancini akiwajibika wakati akiwa na Klabu hiyo
Klabu ya Galatasaray ya nchini Uturuki ipo kwenye mazungumzo na Kocha wa zamani wa Manchester City Roberto Mancini kwa lengo la kumpa kibarua cha kukinoa kikosi chao kutokana na Klabu hiyo kumtimua Kocha wake.
Klabu ya Galatasaray imethibitisha kuanza mazungumzo na Mancini aliyetimuliwa nchini Uingereza baada ya kushindwa kutwaa taji lolote msimu uliopita wa Ligi Kuu na kuambulia kumaliza nafasi ya pili.www.tabasamuleo.blogspot.com

www.tabasamuleo.blogspot.comRais wa Klabu ya Galatasaray Unal Aysal pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Lutfi Aribogan wamekutana na Mancini kwa mazungumzo kuangalia iwapo wataafikiana ili aweze kuanza kazi ya kuifundisha timu hiyo.

Galatasaray wamelazimika kuanza kibarua cha kusaka kocha mwingine baada ya kumtimua Fatih Terim juma lililopita ikiwa ni siku chache baada ya kupata kipigo cha mbwa mwizi kutoka kwa Real madrid kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.

Mancini huenda akachukua nafasi ya Terim aliyefukuzwa baada ya kushindwa kufikia makubaliano na Uongozi wa Galatasaray juu ya kuongeza mkataba wa kuendelea kuifundisha Klabu hiyo.

Terim alikuwa ni mtu mwenye ushawishi mkubwa ndani ya Klabu ya Galatasaray na amefanikiwa kuipa mataji sita miongoni mwa makombe kumi na kenda ambayo timu hiyo imeshinda kwenye historia yake.

Kocha huyo wa Galatasaray anatimuliwa kipindi hiki timu hiyo ikiwa kwenye nafasi ya kumi kwenye msimamo ikiwa imecheza michezo mitano wakiwa pointi nane nyuma ya vinara wa msimu huu na mahasimu wao Fenerbache.

Mancini iwapo atatangazwa kuchukua nafasi ya Terim atakuwa na kibarua cha kuhakikisha Galatasaray inaendeleza ubabae wake kwenye ligi ya nyumbani sanjari na mashindano ya Kombe la Ulaya kwa ngazi za Klabu.

ONA JINSI Megan Young Miss Philippines alivyoibuka mshindi wa Miss World 2013


Miss kutoka Philippines Megan Young ndio amevishwa taji la Miss World 2013 iliyofanyika usiku wa jumamosi, Bali Nusa Dua Convention Center Indonesia.

"I promise to be the best Miss World ever," Alisema Miss Megan baada ya kuvishwa taji hilo na miss world 2012, Wenxia Yu.

MISS UTALII KUTANGAZA KUPATIKANA NYATI WA AJABU NGORONGORO


Nyati mweupe nayepatikana Ngorongoro (HM)

Miss Utalii Tanzania 2013, Hadija Said Mswaga, amesema kuwa kupatikana kwa nyati mweupe wa ajabu na pekee duniani katika hifadhi ya Ngorongoro, imekuwa ni chachu na kichocheo cha pekee kwake katika mpango mkakati wake wa kuitangaza Hifadhi ya Ngorongoro kitaifa na kimataifa, ambapo kwa kuanzia ameamua kuanza kampeni hiyo kupitia mashindano ya dunia anayokwenda kushiriki ya Miss Tourism World 2013, ambayo mwaka huu yanafanyikia nchini Equatorial Guinea Octoba 12, 2013.www.tabasamuleo.blogspot.com

MAAJABU,WATOTO WAFUNGA NDOA.

Wanandoa Mary Chinjendi (15) na Amos Sailowa (17).
Na Imelda Mtema
HAKUNA lugha inayofaa kutumika katika habari hii zaidi ya kusema hii ni kali ya mwaka! Katika hali ya kushangaza, watoto Mary Chinjendi (15) na Amos Sailowa (17), wazaliwa wa Kijiji cha Vilundilo Mbandee, Mkoa wa Dodoma, wamefunga ndoa huku wazazi wa pande zote mbili wakisherehekea harusi, Ijumaa Wikienda lina mkasa wote.www.tabasamuleo.blogspot.com

makala SIMBA SC 2-0 JKT: SIMBA SC NI WAZITO SANA, JAPO WANASHINDA



Na Baraka Mbolembole Mabadiliko yakumtoa nje kiungo Amri Kiemba na kumuingiza uwanjani chipukizi RamadhaniSingano, awali yalionekana kama yangeipa wakati mgumu zaidi timu ya Simba mchezoni. Ila kocha Abdallah ‘King’ Kibadeni aliendelea kuwaamini kundi la wachezaji wake vijana alionao kikosini na kupata pointi nyingine tatu muhimu na kujitanua katika kilele cha msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.

Azam TV kuonyesha mechi zote za Ligi kuu Bara Ikiwemo zile za Yanga



Mtaalamu wa mitambo ya kurusha mpira mojakwamoja wa kituo cha televisheni cha Azam TV akiwajibika uwanjani
KITUO cha Televisheni cha Azam kimeahidi kuonyesha mechi za Yanga zitakazochezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na zile za ugenini kwa sababu mkataba unawaruhusu.
www.tabasamuleo.blogspot.com

ONAJINSI FRANSIC MIYEYUSHO ALIVYOMTWANGA SADIK MOMBA




Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Miyeyusho wakati wa mpambano wao usiokuwa wa ubingwa uliofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa Friends Coner Manzese.www.hakileo.blogspot.com