Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 15 February 2014

RASMI, NI YANGA NA AL AHLY AFRIKA, NGASSA APIGA HAT TRICK TENA JANGWANI WAKIUA 5-2 MORONI


Mrisho Ngassa (kushoto) amefunga mabao matatu leo katika ushindi wa 5-2 wa Yanga dhidi wenyeji Komorozine mjini Moroni katika mchezo wa marudiano Raundi ya Awali Kombe la Shirikisho Afrika. Mabao mengine ya Yanga yamefungwa nna Hamisi Kiiza kulia na Simon Msuva na sasa timu hiyo ya Dar es Salaam inafuzu kwa ushindi wa jumla wa 12-2 baada ya awali kushinda 7-0, Ngassa akifunga hat trick pia na itamenyana na mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya Misri katika Raundi ya Kwanza mwezi ujao.

SIMBA SC imegawana pointi na wenyeji Mbeya City baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 Uwanja wa Sokoine Mbeya

Na Mahmoud Zubeiry, Mbeya
Matokeo hayo yanaifanya Mbeya itimize pointi 35 sawa na Yanga SC iliyo nafasi ya pili kwa wastani mzuri wa mabao wakati Simba inatimiza pointi 32 na inabaki nafasi ya nne.
Hadi mapumziko, tayari Mbeya City walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililofungwa na Deogratius Julius kwa penalti dakika ya 13, akimchambua vizuri kipa Mghana, Yaw Berko.

Wachezaji wa Mbeya City wakishangilia bao la kuongoza kabla ya Simba kusawazisha leo Uwanja wa Sokoine

HUYU NDIO SIMBA MWEUSI NA NI MWEUSI KUSHINDA WOTE DUNIANI CHEKI PICHA



Tuesday 11 February 2014

WANA SIMBA SC WAIPENDE TIMU YAO KATIKA WAKATI MGUMU PIA

BAADA ya kuambulia pointi moja katika mechi mbili za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba SC wanakwenda katika mchezo mwingine mgumu Jumamosi dhidi ya Mbeya City.
Walitoa sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakaenda kufungwa 1-0 na Mgambo JKT Uwanja wa Mkwakwani, Tanga- sasa wanakwenda Uwanja wa Sokoine kuifuata Mbeya City, nini matarajio?
Naamini hapa hata wana Simba vichwa vinawauma wanapoufikiria mchezo huo, ikizingatiwa Mbeya City ni moja ya timu bora katika Ligi Kuu msimu huu na za ushindani haswa, ambayo bado ipo kwenye mbio za ubingwa.

REAL YATINGA FAINALI KOMBE LA MFALME KWA MABAO YA RONALDO

REAL Madrid imefanikiwa kuingia Fainali ya Kombe la Mfalme baada ya usiku wa jana kuizamisha Atletico Madrid kwa mabao 2-0 katika nusu Fainali ya pili.
Shukrani kwake Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo aliyefunga kwa penalti mara mbili dakika ya saba na 16 na kufanya vigogo hao wa Hispania wasonge mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-0.
Real sasa inaweza kukutana na barcelona katika fainali ya michuano hiyo Aprili 19 mwaka huu.

We mkali: Sergio Ramos (kulia) akifurahia na Cristiano Ronaldo baada ya kufunga jana

SHAFF D ; NIONAVYO MIMI:TUNAHITAJI NIDHAMU YA JUU TUNAPOCHEZA SOKA NA WANAWAKE.


Na Oscar Oscar Jr
0789-784858
Mechi ya Mtibwa Sugar vs simba iliyopigwa kwenye uwanja wa Jamhuri pale Morogoro wiki moja iliyopita,ilimalizika kwa matokeo ya sare ya 1-1,Mussa Hassan Mgosi akiifungia Mtibwa sugar na Hamis Tambwe akiisawazishia timu yake ya Simba.Jonisia Rukyaa toka Bukoba ndo mdada aliyekuwa mwamuzi wa kati wa mchezo huo.

KALI ONGALA AACHWA AZAM FC SAFARI YA MSUMBIJI, KIKOSI CHAONDOKA KESHO KUPITIA AFRIKA KUSINI

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
KOCHA Msaidizi wa Azam FC, Kalimangonga Sam Daniel Ongala ‘Kali Ongala’ hatakuwamo kwenye msafara wa timu hiyo unaokwenda Msumbiji kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Raundi ya Awali Kombe la Shrikisho Afrika dhidi ya wenyeji Ferroviario de Beira mwishoni mwa wiki.
Menaja wa Azam FC, Jemadari Said ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, Kali raia wa Uingereza mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) aliyekulia Sinza mjini Dar es Salaam, atakosa safari hiyo kwa sababu pasipoti yake imeisha.

Pasipoti imemkwamisha; Kocha Msaidizi wa Azam FC, Kali Ongala kushoto akiwa na bosi wake Joseph Marius Omog

MBEYA CITY NA MTIBWA ZAINGIZA MILIONI 25.6 uwanja wa sokoine, mbeya




Sunday 9 February 2014

FULHAM YATOKA SARE NA MAN UNITED 2-2


Darren Bent alifunga bao dakika za mwisho mwisho na kumhakikishia kocha wao Rene Meulensteen matokeo muhimu wakati wa mechi kati ya Fulham na Manchester United iliyochezwa katika uwanja wa Old Trafford.