Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 22 February 2014

MATOKEO YA LIGI KUU YA WINGEREZA LEO HAYA HAPA,Arsenal 4 Sunderland 1,MNCITY 1-0SOTCITY

JOHN TERRY AIBEBA CHELSEA ENGLAND

BAO la dakika ya mwisho kabisa la Nahodha aliyerejea John Terry limeipa Chelsea ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Everton jioni hii katika Ligi Kuu ya England.
Ilikuwa kama Jose Mourinho tayari amekwishapoteza pointi mbili katika mbio za ubingwa kutokana na timu hizo kuwa hazijafungana hadi Phil Jagielka alipomchezea rafu Ramires.
Frank Lampard akaenda kupiga mpira wa adhabu ambao uliguswa na Branislav Ivanovic na Terry akateleza kwenda kuusukumia nyavuni dhidi ya kipa Tim Howard.
Baada ya ushindi huo wa mbinde unaoifanya Chelsea itimize pointi 60 baada ya mechi 27 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, na The Blues watasafiri hadi Galatasaray kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Hatua ya 16 Bora Jumatano.


Mkombozi: Frank Lampard (kushoto) na John Terry ushirikiano wao umeipa bao la ushindi Chelsea

YANGA SC YAWATUMIA SALAMU NZITO AL AHLY, YAWAFUMUA WANAJESHI 7-0 LIGI KUU BARA DAR

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
YANGA SC imetoa onyo kwa wapinzani wao katika Ligi ya Mabingwa Afrika mwezi ujao, Al Ahly ya Misri baada ya kuifumua mabao 7-0 Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
Ushindi huo unaifanya Yanga SC irejee kileleni mwa Ligi Kuu baada ya kutimiza pointi 38, mbili zaidi ya Azam inayoangukia nafasi ya pili sasa, ambayo kesho itamenyana na Prisons ya Mbeya Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Wawili wabaya; Emmanuel Okwi kulia na Mrisho Ngassa wakishangilia baada ya bao la nne leo na chini Kavumbangu anapongezwa baada ya kufunga moja ya mabao yake



Hadi mapumziko, tayari Yanga SC walikuwa mbele kwa mabao 4-0 yaliyotiwa kimiani na Didier Kavumbangu, Simon Msuva, Emmanuel Okwi na Mrisho Ngassa.
Yanga SC leo ilibadilika mno kiuchezaji na kuonyesha soka ya kiwango cha juu, tofauti na soka yao iliyozoeleka ya bila mipango inayosababisha kupoteza nafasi nyingi.
Ngassa alicheza nafasi ya kiungo mchezeshaji mbele ya mkabaji Frank Domayo na kuiongoza vyema timu, hata kuwa chachu ya ushindi huo mnono.

MBEYA CITY 0 - 2 COASTAL UNION



Leo mambo yamekuwa magumu kwa Mbeya City baada ya kukubali kufungwa na Coastal Union ya jijini Tanga kwa goli 2 bila

FLAMINI ALIVYOMTWANGA NGUMI WILSHERE BAADA YA KUZINGUANA MAZOEZINI JANA...NI SIKU CHACHE TU BADAA YA KUMPA MAKAVU OZIL

KIUNGO Jack Wilshere ameposti picha inayomuonyesha akipigana na mchezaji mwenzake Mathieu Flamini baada ya mazoezi jana kwenye basi la timu.
Viungo hao wawili walipigwa picha wakionekana kutofautiana kwenye mazoezi ya timu hiyo saa 24 kabla ya Arsenal kuwakaribisha Black Cats katika mchezo wa Ligi Kuu.

Wote utani: Wilshere ameposti picha hii inayomuonyesha akipigana na Mfaransa huyo kwenye basi la timu
+6

Nipishe: Jack Wilshere amehusishwa na kutofautiana na mchezaji mwenzake Mathieu Flamini kwenye mazoezi ya Arsenal jana na Bacary Sagna anaonekana kwenda kusuluhisha

Utaniambia nini: Wilshere akiongea kwa ishara ya mikono na Flamini huku Sagna akimfuata kumtuliza

Tuesday 18 February 2014

SAKATA LA OKWI LAMPELEKA MFANYAKAZI WA TFF KWENYE KAMATI YA MAADILI KWA UDANGANYIFU,


WATANO WALALAMIKIWA KAMATI YA MAADILI
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewalalamikia wana familia watano wa mpira wa miguu kwa Kamati ya Maadili kuhusiana na udanganyifu katika mtihani wa utimamu wa mwili wa waamuzi na usajili wa mchezaji Emmanuel Okwi.

SHAFFIH,, NIONAVYO MIMI:HESHIMA YA WENGER ITARUDISHWA NA MATAJI.


Na Oscar Oscar Jr
0789-784858.
Haustahili kupata heshima kwenye mchezo wa soka kama hushindi mataji.Ufalme wa Pep Gaudiola Duniani haukuletwa na staili yake tu ya "Tiki-taka" bali mataji lukuki aliyoshinda akiwa na Barcelona.Jose Mourinho pamoja na kuhama hama timu lakini anapewa heshima kokote anakokwenda kwa sababu tu ya mataji aliyoshinda akiwa na klabu ya Porto,Chelsea,Inter Millan na Real Madrid.

MESSI AWAKALISHA MAN CITY ETIHAD, IBRAHIMOVIC AING'ARISHA PSG UGENINI

BARCELONA imejiwekea mazingira mazuri ya kupenya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Manchester City, Uwanja wa Etihad usiku huu katika mchezo wa kwanza, hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo.
Lionel Messi alifunga bao la kwanza dakika ya 54 kwa penalti ya utata, baada ya yeye mwenyewe kuangushwa nje kidogo ya eneo la hatari na Martin Demichelis, lakini refa akatenga tuta, kabla ya beki Dani Alves kufunga la pili dakika ya 90.

Mtu hatari; Messi akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza kwa penalti usiku huu Uwanja wa Etihad
Hilo linakuwa bao la kwanza kabisa Messi anafunga dhidi ya vigogo wa Ligi Kuu ya England tangu ameanza kukutana navyo akiwa na Barca mwaka 2006 na kumaliza ukame wa kucheza saa 12 nchini humo bila kufunga.

Monday 17 February 2014

Lulu akiri mahakamani kuwa mpenzi wa Kanumba

Dar es Salaam. Mwigizaji maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael Kimemeta, amekiri mahakamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na aliyekuwa mwigizaji mwenzake, Steven Kanumba na pia kuwa ugomvi na Kanumba siku ya tukio la kifo cha mwigizaji huyo, lakini akakana mashtaka ya kumuua bila kukusudia.
Lulu ambaye yuko nje kwa dhamana anakabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akidaiwa kumuua Kanumba bila kukusudia, kinyume cha Kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu (PC), April 7, 2012, nyumbani kwa marehemu Kanumba, Sinza Vatican.

Sunday 16 February 2014

ARSENAL YALIPA KISASI KWA LIVERPOOL, YAING'OA KOMBE LA FA 2-1

BAO la Alex Oxlade-Chamberlain na pasi ya bao vimetoa mchango mzuri jioni hii kwa Arsenal kutinga Raundi ya sita ya Kombe la FA baada ya kuifunga Liverpool mabao 2-1 Uwanja wa Emirates.
Kiungo huyo kinda wa England alifunga bao la kwanza dakika ya 16 akimalizia pasi ya Lukas Podolski, aliyefunga bao la pili dakika ya 47.
Refa Howard Webb aliwapa penalti Liverpool baada ya Podolski kumchezea faulo Luis Suarez, na Steven Gerrard akaenda kufunga dakika ya 59.
Pamoja na hayo, Webb alimezea penalti nyingine ya Liverpool baada ya Oxlade-Chamberlain kumuangusha Suarez kwenye eneo la hatari.
Liverpool ilitawala mchezo na kutengeneza nafasi nyingi za kusawazisha, lakini mwisho wa mchezo, Arsenal walifanikiwa kulipa kisasi cha kufungwa mabao 5-1 Uwanja wa Anfield katika Ligi Kuu.

Kitu hicho: Alex Oxlade-Chamberlain akifunga bao la kwanza

NI MUHIMU YANGA KUYAFAHAMU HAYA KABLA YA KUMCHEZESHA OKWI.

Stori iliyoongoza kwa vichwa vya habari za michezo mwishoni mwa juma lililopita ilikuwa inamuhusu mshambuliaji Emmanuel Okwi.
Kilichopelea gumzo la mchezaji huyo ilikuwa ni baada ya FIFA kuiandikia barua TFF na kuitaarifu ya kwamba mchakato wa uhamisho wa Okwi toka SC Villa kwenda Yanga ulikuwa hauna tatizo. Lakini pamoja na kutoa taarifa hiyo FIFA bado ilisema yenyewe haina mamlaka ya kumruhusu mchezaji kuichezea klabu yake hiyo mpya zaidi ya kuiagiza TFF kufuatilia wenyewe taratibu za uhamisho wa mchezaji huyo kama zipo sahihi.