Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Tuesday 25 March 2014

MAN CITY YAIPIGA MAN UNITED 3-0, ARSENAL YALAZIMISHWA SARE 2-2 NA SWANSEA

KLABU ya Manchester City imewaangusha wapinzani wao Manchester United kwa mabao 3-0 usiku huu katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford.
Mabao ya Man City usiku huu yamefungwa na mshambuliaji Edin Dzeko mawili dakika za kwanza na 26, pasi kutoka Samir Nasri na Yaya Toure dakika ya 90.

Kiboko yao; Edin Dzeko amefunga mabao mawili Manchester City ikiilaza 3-0 Man United usiku huu

BAYERN MUNICH YANYAKUA UBINGWA WA UJERUMANI


Na P.T
Timu ya Bayern Munich ya ujerumani imenyakua kombe la ligi kuu ya nchi hiyo baada ya kuifunga Hertha Berlin kwa jumla ya mabao 3-1 na kuifanya kuwa ni timu ya kwanza nchini humo kunyakua ubingwa huo ikiwa bado haijakamilisha mechi zake. Mpaka sasa timu hiyo ina mechi saba ambazo zimebaki ili kukamilisha mechi za ligi kuu nchini humo. Katika mchezo huo uliofanyika usiku wa kuamkia leo ni kuwa magoli ya Bayern yalifungwa na Toni Kroos dakika ya 6 katika kipindi cha kwanza,Mario Goetze dakika ya 14 naye Franck Ribery alihitimisha idadi ya magoli kwa Bayern baada ya kufunga goli la tatu dakika ya 79 ya mchezo na kuifanya Bayern kunyakua ubingwa huo