Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 25 January 2014

Hii ndio headline mpya ya Jay Z na Beyonce.

Moja kati ya familia maarufu hivi sasa kwenye kiwanda cha burudani ni ya Mr and Mrs Carter ambao wote wawili wana-status kubwa kwenye muziki.

LIVERPOOL YAPETA KOMBE LA FA...SUAREZ LEO ALIKUWA MPISHI TUUUU!

MABAO ya Victor Moses na Daniel Sturridge yametosha kuiwezesha Liverpool kuifunga Bournemouth katika mechi ya Raundi ya Nne ya Kombe la FA jioni hii.
Wageni waliingia Uwanja Goldsands na kikosi cha nguvu na alikuwa ni Luis Suarez aliyetengeneza mabao yote yaliyoiwezesha Reds kuingia 16 Bora.

Back to business: Daniel Sturridge celebrates in front of the Liverpool fans after scoring their second

KIPRE TCHETCHE AITAKATISHA AZAM CHAMAZI, YANGA HAWANA RAHA KILELENI

RAHA KILELENI
Na Prince Akbar, Chamazi
BAO pekee la mshambuliaji wa Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche jioni ya leo limeipa ushindi wa 1-0 Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Isihaka Shirikisho wa Tanga, Tchetche alifunga bao hilo baada ya kupokea pasi nzuri ya Joseph Lubasha Kimwaga na akiwa katikati ya mabeki wa Mtbwa Sugar, akaumiliki mpira vyema na kufumua shuti kali lililotinga nyavuni.

Asante kwa pande; Kipre Tchetche kulia akipongezana na Joseph Kimwaga aliyempa pasi ya kuifungia Azam bao pekee leo

MBEYA CITY YAZIDI KULA SAHANI MOJA NA YANGA NA AZAM KILELENI

Na Princess Asia, Bukoba
MBEYA City imezidi kula sahani moja na Yanga SC na Azam FC kileleni, kufuatia ushindi wa 1-0 leo ugenini dhidi ya wenyeji Kagera Sugar, Uwanja wa Kaitaba, Bukoba katika mchezo wa kwanza wa duru la pili Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Shukrani kwake Swita Julius aliyefunga bao hilo pekee kwenye mchezo huo na sasa Mbeya City inatimiza pointi 30 sawa na Azam FC inayokaa nafasi ya pili tu kwa sababu ya wastani mzuri wa mabao, wakati Yanga ipo kileleni kwa pointi zake 31.

Mbeya City bado inakula sahani moja na Yanga na Azam

RAAASMIII, JUAN MATA NI MAN UNITED

KLABU ya Manchester United imetangaza kumsajili Juan Mata kutoka Chelsea kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 37.1.
Kiungo huyo wa Hispania alipokewa na kocha David Moyes Jumamosi, na Mata anatarajiwa kuanza kuitumikia Man United katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Cardiff Jumanne Uwanja wa Old Trafford.



Mpango mzima: Mata akisaini Manchester United kwa dau la rekodi, pauni Milioni 37.

YANGA YAANZA MZUNGUKO WA PILI KWA KUTOA KIPIGO - YAICHAPA ASHANTI 2-1


Raha ya ushindi.....Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao pili la timu hiyo dhidi ya Ashanti United.

Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao pili la timu hiyo dhidi ya Ashanti United, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga imeshinda 2-1. Kutoka kushoto ni Frank Domayo, Simon Msuva na David Luhende. Yanga imeshinda 2-1.

Friday 24 January 2014

MOYES ANAVYOHAHA DUNIA NZIMA KUIIMARISHA MAN UNITED...JANA ALIKUWA KWENYE MECHI YA BAYERN KUANGALIA WACHEZAJI

UNITED...JANA ALIKUWA KWENYE MECHI YA BAYERN KUANGALIA WACHEZAJI
KOCHA David Moyes alisindikizwa Uwanja wa Borussia Monchengladbach na wakala wa Toni Kroos jana usiku na inaaminika ilikuwa katika harakati za usajili.
Mshambuliaji wa Bayern Munich, Mario Mandzukic na kiungo wa Moenchengladbach, Patrick Herrmann inaaminika ndio wachezaji ambao kocha huyo wa Manchester United alikuwa anawafuatilia akiwa ameketi jukwaani Borussia Park kuangalia mchezo wa Bundesliga ambao wageni walishinda 2-0.
Lakini pamoja na hayo imevuma sana kwamba Kroos ndiye chaguo la kwanza la Moyes baada ya kuonekanana wakala wake, Sascha Breese kwenye mechi hiyo.

Mchapa kazi: Kocha wa Manchester United, David Moyes akiwa na wakala wa Toni Kroos kulia nchini Ujerumani

MANCHESTER UNITED WATHIBITISHA RASMI KUMSAJILI JUAN MATA

ARSENAL RAHA DUNIANI, YAWATANDIKA JAMAA 4-0 KOMBE LA FA HADI HURUMA!

ARSENAL imeilaza mabao 4-0 Coventry katika mchezo wa Raundi ya Nne Kombe la FA usiku wa jana Uwanja wa Emirates.
Lukas Podolski alifunga mabao mawili kabla ya Olivier Giroud na Santi Cazorla kuja kufunga meine.

Shujaa: Podolski akipiga ngumi hewani baada ya kufunga mabao mawili jana

HUU NDO UKWELI KUHUSU USAJILI WA OKWI

Thursday 23 January 2014

EZEKIEL KAMWAGA KATIBU MPYA SIMBA SC...ASHA MUHAJI OFISA HABARI


Bosi mpya; Ezekiel Kamwaga Katibu mpya wa Simba SC
MWENYEKITI wa Simba SC, Alhaj Ismail Rage anatarajiwa kumtaja Ezekiel Kamwaga kuwa Katibu mpya wa klabu hiyo, nafasi iliyoachwa wazi na Evodius Mtawala aliyejiuzulu baada ya kuteuliwa Shirikisho la SOka la SOka Tanzania (TFF).

COASTAL WAREJEA DAR 'WANUKIA' MARASHI YA MUSCAT
Home » Unlabelled » COASTAL WAREJEA DAR 'WANUKIA' MARASHI YA MUSCAT


Kipa Shaaban Kado akiwaongoza wachezaji wenzake wa Coastal Union kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jioni hii baada ya kuwasili kutoka Muscat, Oman walipoweka kambi ya wiki mbili kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara unaoanza keshokutwa.

CHELSEA YATHIBITISHA KUFIKIA MAKUBALIANO NA FC BASEL JUU YA UHAMISHO WA MOHAMED SALAH.



KUUMIA KWA FALCAO NI PIGO KWA COLOMBIA & KOMBE LA DUNIA.



Habari mbaya leo kwenye michezo ni kuhusu majeraha ya mshambuliaji Radamel Falcao aliyoyapata jana usiku kwenye mchezo kati ya timu yake ya Monaco dhidi ya timu ya ligi daraja la nne ya Chasselay kwenye kombe la Ufaransa.

Wednesday 22 January 2014

MESSI AWA BONGE LA MPISHI BARCA IKIITANDIKA 4-1 LEVANTE ILIYOTOKA NAYO SARE JUMAPILI

TIMU ya Barcelona imemaliza hasira zake za sare ya Jumapili na Levante kwa kuifumua timu hiyo mabao 4-1 usiku huu kwenye Robo Fainali ya kwanza ya Kombe la Mfalme Uwanja wa Ciutat de Valencia.
Mkali wa mabao wa Barca, Lionel Messi amecheza mechi ya 400 katika timu hiyo Katalunya usiku huu, ambazo ndani yake ameshinda mataji sita ya La Liga na matatu ya Ligi ya Mabingwa.
Messi alifanya kazi nzuri akitoa mchango kwa mabao yote manne, ikiwemo hat-trick ya Cristian Tello. Wenyeji walitangulia kupata bao lililofungwa na mchezaji wa zamani wa Liverpool, Nabil El Zhar.
Juanfran alijibabatiza mpira uliopigwa na Messi na akaudondoshea kwenye nyavu zake mwenyewe kuisawazishia Barca- kabla ya Tello kufunga mara tatu mfululizo kuipa ushindi mtamu timu yake.


Mpishi: Lionel Messi (kulia) akishangilia baada ya kumsetia Cristian Tello (katikati) kufunga hat trick katika ushindi wa Barcelona wa 4-1 dhidi ya Levante

KENNY MWAISABULA: 2010 NILIPEWA JUKUMU LA KUIBAKISHA LIGI KUU VILLA SQUARD IKASHINDIKANA,SASA NIMEPEWA JUKUMU KUIPANDISHA LIGI KUU.

Kocha wa mpira Kennedy Mwaisabula leo ametangazwa rasmi kuwa kocha wa timu ya Villa Squard ya Magomeni,timu hiyo inashiriki ligi daraja la kwanza.
''Ni kweli nimechaguliwa kuwa kocha wa Villa Squard hadi mwishoni mwa raundi yapili ya ligi daraja la kwanza, malengo yangu makubwa mara tu baada ya kupewa nafasi hii ni kuhakikisha timu hii kongwe inapanda ligi kuu mwakani''.
Hii leo Mwaisabula ameiongoza Villa kuifunga Ashanti mabao 2-1 kwenye mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye uwanja wa karume jijini Dar Es Salaam.
Je wajua ?

Hatimae CHELSEA WAKUBALI OFA YA £37M KUTOKA MAN UNITED KWA AJILI YA MATA - KUFANYIWA VIPIMO LEO


Ofa ya Manchester United ambayo inaaminika kuwa kiasi cha £37m, imekubaliwa na klabu ya Chelsea kwa ajili ya usajili kiungo wa kihispania Juan Mata.
Kiungo mwenye miaka 25 atafanyiwa vipimo vya afya leo Alhamisi kabla ya kukamilisha usajili wake wa kujiunga na mabingwa hao wa EPL.

Monday 20 January 2014

MALINZI AELEZEA MIKAKATI YAKE KWA LOWASSA


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema shirikisho lake limepanga malengo ya muda mfupi na mrefu ikiwa na sehemu ya mkakati wa kuendeleza na kuinua kiwango cha mchezo huo nchini.

RAIS KIKWETE AMUAPISHA JUMA NKAMIA NA WENZAKE KUANZA KAZI RASMI


Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Juma Nkamia, kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR

MANCHESTER CITY KUKIPIGA NA WEST HAM LEO.



Timu ya Manchester City leo itapambana na timu ya West Ham United katika uwanja wa Upton Parkkwenye mzunguko wa pili wa nusu fainali ya kombe la '' Capital One Cup''.

Sunday 19 January 2014

ETO'O AUA SHETANI DARAJANI...MAN UNITED YALALA 3-1 KWA CHELSEA

MCAMEROON Samuel Eto'o amelichangamsha Jiji la London leo baada ya kufunga mabao yote matatu katika ushindi wa 3-1 wa Chelsea dhidi ya Manchester United, Uwanja wa Stamford Bridge.
Eto'o alifunga mabao mawili kipindi cha kwanza dakika ya 17 na 45 na baadaye dakika ya nne tangu kuanza kipindi cha pili akakamilisha hattrick yake kabla ya kumpisha Fernando Torres dakika ya 79.
Javier Hernandez 'Chicharito' aliyetokea benchi dakika ya 56 kuchukua nafasi ya Ashley Young aliwafungia Mashetani Wekundu bao la kufutia machozi dakika ya 78.
Nemanja Vidic alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 90 na ushei na Man United ikaishiwa nguvu kabisa.
Ushindi huo, unaifanya The Blues ya Jose Mourinho ifikishe pointi 49 baada ya kucheza mechi 22, ikiwa katika nafasi ya tatu nyuma ya Manchester City pointi 50 na Arsenal pointi 51, wakati United ya David Moyes inabaki nafasi ya saba pointi 37.
Katika mchezo uliotangulia, Tittenham Hotspur imeifunga Swansea City mabao 3-1 nyumbani kwake. Mabao ya Spurs yalifungwa na Emmanuel Adebayor dakika ya 35 na 71 na Chico aliyejifunga dakika 53, wakati la wenyeji la kufutia machozi lilifungwa na Bony dakika ya 78.




Shujaa: Samuel Eto'o akishangilia raha aliyowaha Chelsea na huzuni aliyowaachia Manchester United Uwanja wa Stamford Bridge leo

MANJI AWAOMBA WADHAMINI WA KLABU HIYO KUANGALIA UPYA MKATABA WA AZAM TV,ASISITIZA KUTOTETEA NAFASI YAKE


Mwenyekiti wa Yanga Yusuf Manji amewaomba wadhamini wa klabu hiyo, kuangalia upya mkataba wa Azam TV, kwani kwake yeye binafsi anauona hauna manufaa kwa klabu yao ambayo inaingiza zaidi ya mil 300 katika mchezo mmoja akitolea mfano mchezo kati yao na Watani zao Simba.

BREAKING NEWS; BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI HILI HAPA,ASHA MIGIRO,NKAMIA NA SAADA WAULA,NCHIMBI,KAGASHEKI OUT, MAGUFULI APETA.

Dakika chache zilizo pita katibu kiongozi wa Serikali ya Tanzania kwa niaba ya raisi Kikwete ametangaa baraza jipya la mawaziri.
HAYA NI MABADILIKO MAPYA

Wizara ya katiba na sheria ni Dk. Asha Migiro huku aliekuwa naibu akiendelea.
Wizara ya makamo wa raisi nchi na Mungano mabadiliko ni kwa naibu amabae ni ALL MWALIMU