Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 4 January 2014

AZAM FC WALIVYOKATA TIKETI YA KWANZA YA ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI


Mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Herman Tchetche kulia akipiga mpira uliompita kipa wa Tusker FC ya Kenya, Samuel Odhiambo na kwenda nje sentimita chache kutoka langoni katika mchezo wa Kundi C, Kombe la Mapinduzi usiku wa leo Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Azam FC ilishinda 1-0 na kuwa timu ya kwanza kufuzu Robo Fainali ya michuano hiyo.


Kiungo wa Tusker, Michael Olonga akiwatoka wachezaji wa Azam

Seif Abdallah wa Azam akimiliki mpira pembeni ya Martin Kiiza wa Tusker


Salum Abubakar 'Sure Boy' wa Azam Fc akipasua katikati ya Uwanja


Beki wa Tusker akijaribu kumpokonya mpira mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Tchetche


Mshambuliaji wa Azam FC, Brina Umony akijaribu kuumiliki vyema mpira mrefu aliotanguliziwa

Kiungo mkabaji wa Azam FC, Kipre Balou akiondosha mpira miguuni mwa mshambuliaji wa Tusker FC


Winga wa Azam FC, Joseph Kimwaga akimuacha chini beki wa Tusker FC


Kikosi cha Tusker FC leo


Kikosi cha Azam FC leo


Mashabiki jukwaa kuu wakiangalia burudani

No comments:

Post a Comment