Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Monday 23 December 2013

Hatima ya Rage kujulikana leo

NA MWANANCHI
Dar es Salaam. Hatma ya Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage itajulikana leo wakati kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) chini ya mwenyekiti wake Jamal Malinzi atakapokutana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kikao hicho mbali na kumjadili Rage pia kitapitia ajenda mbalimbali ikiwemo uundwaji wa vyombo vya haki Kamati ya Nidhamu, Kamati ya Maadili na Kamati ya Uchaguzi.
Kamati hizo zinaundwa upya baada ya zile za awali zilizoundwa na Rais aliyemaliza muda wake Leodegar Tenga kuvunjwa na Rais Malinzi mara alipotangazwa kuwa mshindi.


Tayari Malinzi ameshaunda kamati ndogondogo na kamati hizi atakazotangaza leo ndiyo kamati za mwisho katika ngazi za uamuzi.


Mbali na kamati hizo, kikao hicho pia kitatoa tamko la mwisho kuhusu Rage ambaye alikaidi agizo la kamati hiyo ya utendaji iliyotoa Novemba 23 kwa kumtaka aitishe mkutano wa dharura wa wanachama ndani ya siku 14 ili kujadili matatizo yanayoendelea ndani ya klabu hiyo ikiwa ni pamoja na kufanya marekebisho ya katiba.

Hata hivyo, Rage alikaidi agizo hilo kwa kile alichoeleza kuwa katiba ya Simba haisemi hivyo na hamlazimishi kuitisha mkutano huo, pia tayari Rage ameweka msimamo wake kuwa anasubiri tamko hilo la TFF ili atangaze tarehe rasmi ya kuanza mchakato wa uchaguzi.


Wakati huohuo, TFF imetangaza kesho ndiyo siku ya mwisho ya kuweka pingamizi kwa usajili wa dirisha dogo kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza.
Klabu za Kagera Sugar, Mtibwa Sugar na Coastal Union ndizo timu pekee kati ya 14 za Ligi Kuu hiyo ambazo hazikuwasilisha maombi ya usajili katika dirisha dogo.


Ashanti United imeweka rekodi ya kusajili wachezaji 15 katika usajili wake wa sasa.

No comments:

Post a Comment