Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Tuesday 8 April 2014

ROONEY FITI KABISA, AWAPASHIA KIKAMILIFU BAYERN MUNICH LEO

MSHAMBULIAJI Wayne Rooney amerejesha matumaini ya Manchester United kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuanza mazoezi kwa ajili Robo Fainali ya pili dhidi ya mabingwa watetezi, Bayern Munich Uwanja wa Allianz Arena kesho.
Rooney alikosa mechi ya Ligi Kuu England United ikiifunga mabao 4-0 Newcastle mwishoni mwa wiki kutokana na maumivu ya mguu, lakini sasa kuna uwezekano kesho akacheza
Ryan Giggs pia alifanya mazoezi baada ya kukosa mechi dhidi ya Newcastle, lakini Marouane Fellaini, ambaye alitolewa nje Uwanja wa St James Park baada ya kuumia na Rafael hawakushiriki mazoezi leo.
Baada ya sare ya 1-1 nyumbani, United sasa wanatakiwa kushinda ugenini dhidi ya Bayern ili kutinga Nusu Fainali.

Mazoezi makali: Rooney akifanya mazoezi kuelekea mchezo wa marudiano na Bayern Munich



+12
Rooney alishiriki mazoezi kikamilifu



Rooney ameonekana kusahau kabisa kuhusu maumivu


Rooney ameonekana yuko fiti kwa ajili ya mchezo huo
Kocha wa Manchester United, David Moyes ameonekana kufurahia kurejea kwa Rooney

No comments:

Post a Comment