Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Wednesday 23 April 2014

REAL HATARINI KUWAKOSA GARETH BALE NA RONALDO LEO DHIDI YA BAYERN, WOTE WAGONJWA

WINGA Gareth Bale yuko shakani kuichezaea Real Madrid katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich kutokana na kusumbuliwa nugonjwa wa mafua.
Nyota huyo wa Wales hajasafiri na wenzake kwa ajili ya mchezo wa kwanza leo Uwanja wa Sangtiago Bernabeu.
Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti pia anatilia shaka uzima wa Cristano Ronaldo. Nyota huyo wa Ureno anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya muda mfupi kabla ya mchezo wa leo.

Shaka tupu: Gareth Bale anasumbuliwa na mafua kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Bayern Munich

Pigo: Madrid inaweza kumkosa Bale na Cristiano Ronaldo leo
Ikiwa Bale ataukosa mchezo wa leo, litakuwa pigo kwa Ancelotti, ambaye alimwagia sifa nyingi winga huyo katika Mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea mchezo wa leo.
Bale anang'ara kwa sasa, baada ya kufunga bao la ushindi katika fainali ya Copa del Rey dhidi ya Barcelona wiki iliyopita na kocha wake akasema mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 86 kutoka Tottenham atakuwsa mkali zaidi msimu ujao Hispania ambao utakuwa wa pili kwake Real.
"Gareth ni mtoto mkali,"alisema Ancelotti. "Anavutia kwa kujiamini kiasi cha kutosha hususan kutokana na bao alilofunga dhidi ya Barcelona katika fainali,"alisema.

No comments:

Post a Comment