Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Monday 6 January 2014

PIGO ARSENAL NA ENGLAND, WALCOTT NJE MIEZI SITA...ATAKOSA HADI KOMBE LA DUNIA

TIMU ya taifa ya England na Arsenal zimepata pigo kubwa baada ya Theo Walcott kutakiwa kuwa nje kwa kipindi chote kilichobaki cha msimu pamoja na Kombe la Dunia, baada ya kuumia goti.
Winga huyo alitolewa nje Jumamosi katika mechi ya Kombe la FA Arsenal ikiifunga Tottenham baada ya kuumia na baada ya vipimo anatakiwa kuwa nje kwa mzi sita kwa sababu ya maumivu ya goti la mguu wa kushoto.
Habari hizo hakika ni pigo kubwa kwa kocha wa timu ya taifa ya England, Roy Hodgson kuelekea Fainali za Kombe la Dunia katikati ya mwaka huu nchini Brazil.


Maumivu: Theo Walcott anatakiwa kuwa nje kwa miezi sita baada ya kuumia goti la mguu wa kulia

Alivyoumia: Walcott (kushoto) alipata maumivu hapa wakati anapambana kugombea mpira na Danny Rose wa Spurs

Walcott (kushoto) sasa atakuwa nje kwa kipindi chote cha msimu kilichobaki na atakosekana pia kwenye kikosi cha England Kombe la Dunia

No comments:

Post a Comment