Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Tuesday 14 January 2014

ARSENAL KUTOA PAUNI MILIONI 37 KUMSAJILI 'NEW VAN PERSIE, NI KINDA HATARI LA UJERUMANI...WENGER UDENDA WAMWAGIKA

KLABU ya Arsenal ipo tayari kutoa Pauni Milioni 37 kumnunua kinda mwenye kipaj Mjerumani ambaye wanaamini atakuwa Robin van Persie mwingine.
Wanajiandaa kufika bei ya Julian Draxler, mwenye umri wa miaka 20, ambaye ametambulishwa kama mlengwa mkuu kwa Gunners katika usajili wa dirisha dogo baada ya kupita huku na kule kusaka vipaji.
Benchi la Ufundi la Arsene Wenger inaamini Draxler, ambaye anacheza kama kiungo mshambuliaji katika klabu ya Schalke, anaweza kucheza kama mshambuliaji pekee wa kati.
Arsenal inafikiri Draxler ni sawa na Van Persie na Thierry Henry ambao waliwasili klabu hiyo kama mawinga, lakini baadaye wakawa washambuliaji hatari.

Anakwenda London? Arsenal inatazamiwa kutoa Pauni Milioni 37 kumsajili nyota wa Schalke, Julian Draxler

No comments:

Post a Comment