Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Tuesday 15 October 2013

SAMATTA, ULIMWENGU WAIPA MAZEMBE TAJI LA SUPER CUP DRC



TOUT Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) leo imetwaa taji la Super Cup la nchini humo baada ya kuifumua mabao 7-0 FC MK ya Kinshasa mjini Lubumbashi.
Mabingwa hao mara nne Afrika tayario walikuwa mbele kwa mabao mawili hadi mapumziko, yaliyofungwa na mshambuliaji Mtanzania, Thomas Ulimwengu dakika ya 21 na kiungo wa Ghana, Daniel Nii Adjei dakika ya 33.

Dakika tano baada ya kuanza kipindi cha pili, Gladson Awako wa Ghana pia alifunga la tatu kabla ya ndugu yake Richard Kissi Boateng kufunga la nne dakika ya 66.
Adjei akafunga bao lake la pili katika mchezo huo dakika ya 68 kabla ya Herve Ndonga kufunga la sita dakika tatu baadaye na Mtanzania mwingine, Mbwana Samatta akafunga la saba dakika ya mwisho.


Ushindi huo mnono unakuja siku chache kabla ya kucheza Nusu Fainali ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stade Malien ya Mali wiki ijayo, baada ya awali kushinda ugenini 2-1 katika mchezo wa kwanza. Chanzo: binzubeiry

No comments:

Post a Comment