Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Wednesday 5 February 2014

PICHA KAMILI SIMBA NA MTIBWA JAMHURI, HANS POPPE NA MAESTRO KAMA 'WAMEPIGWA SHOTI'


Vita ya mabeki; Beki wa kushoto wa Simba SC, Issa Rashid 'Baba Ubaya' akigombera mpira na beki wa kulia wa Mtibwa Sugar, Hassan Ramadhani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya jana Uwanja wa Jamhuri, Morogoro ambao ulimalizika kwa sare ya 1-1.


Rmadhani Singano 'Messi' wa Simba SC akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Mtibwa Sugar, Hassan Ramadhani

Messi na Hassan


Messi akipambana kuwatoka mabeki wa Mtibwa Sugar

Mshambuliaji wa Simba SC, Ali Badru akiwatoka mabeki wa Mtibwa Sugar


Kocha wa Mtibwa Sugar, Meck Mexime aliyeipa mgongo kamera akimtuliza Nahodha wake, Shaaban Nditi baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kwenye mchezo huo


Beki wa Mtibwa Sugar, Juma Mpakala kushoto akipambana na mshambuliaji wa Simba SC, Ali Badru


Haroun Chanongo wa Simba SC kulia akigombea mpira na Jamal Mnyate wa Mtibwa Sugar


Mshambuliaji wa Simba SC, Amisi Tambwe akimtoka beki wa Mtibwa Sugar, Salvatory Ntebe, huku Messi akiwa tayari kutoa msaada


Kiungo wa Simba SC, Jonas Mkude akimtoka kiungo wa Mtibwa Shaaban Kisiga


Mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Juma Luizio akipasua katikati ya wachezaji wa Simba SC, Haroun Chanongo kulia na Jonas Mkude kushoto


11 walioanza Mtibwa Sugar leo


11 wa Simba SC walioanza leo


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera kulia akiwasalimi wachezaji wa Simba SC kabla ya mechi. Hapa amepeana mikono na beki Joseph Owino. Katikati ni Messi na kushoto Donald Mosoti


Wakubwa; Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe kulia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili na Ibrahim Masoud 'Maestro' wakifuatilia mchezo huo

No comments:

Post a Comment