Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 8 February 2014

LIVERPOOL YAICHANACHANA ARSENAL...AIBU TUPU ni 5-1

LIVERPOOL imewaadhiri Arsenal waliokuwa wanasifiwa wana ukuta mgumu, kwa kuwafumua mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jioni hii Uwanja wa Anfiled.
Mabao ya Liverpool leo yamefungwa na Skrtel dakika ya kwanza na 10, Sterling dakika ya 15 na 52 na Sturridge dakika ya 20.
Bao la kufutia machozi la Arsenal lilifungwa na Arteta dakika ya 69 kwa penalti. Ushindi huo, unaifanya Arsenal ibaki na pointi zake 55 katika nafasi ya pili baada ya kuchea mechi 25, wakati Liverpool imefikisha pointi 50 baada ya mechi 25 pia, ingawa inaendelea kubaki nafasi ya nne.

Furaha tupu: Wachezaji wa Liverpool wakishangilia ushindi wao mnono dhidi ya Arsenal leo


Huruma: Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere akiwa haamini macho yake juu ya kilichowakuta leo

Mmoja wa wafadhili maarufu wa Simba SC na mwanachama wa klabu hiyo ya Dae es Salaama,ambaye pia ni shabiki wa Liverpool, Muslsah Ruwah alikuwepo Anfield leo

No comments:

Post a Comment