Pages

ELIMU KWANZA.

ELIMU KWANZA.
FEDHA SIO KIPAUMBELE CHETU.

Saturday 8 March 2014

BARCELONA YAPIGWA NA KITUMU CHA KUSHUKA DARAJA LA LIGA

KLABU ya Barcelona leo imecheza sokambovu mno zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya kukutana na Manchester City katika mchezo wa marudiano wa Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya na kufungwa na bao 1-0 Real Valladolid iliyo hatarini kushuka.
Bao hilo pekee lililozaimisha Barca iliyoongozwa na nyota wake Lionel Messi leo, lilifungwa na Mtaliano Fausto Rossi dakika ya 17 Uwanja wa Manispaa mjini Valladolid.
Huo ni ushindi wa kwanza wa Valladolid tangu Januari ambao unaiinua hadi nafasi ya 17 kutoka ya 18 kwa kutimiza pointi 26 baada ya kucheza mechi 27, wakati Barcelona inabaki nafasi ya pili kwa pointi zake 63 baada ya kucheza mechi 27,moja zaidi dhidi ya vinara, Real Madrid wenye pointi 64.

Siku mbaya ofisini: Nyota wa Barcelona, Lionel Messi akiwa haamini macho yake baada ya kipigo cha Valladolid
Kiboko yao: Mfungaji wa bao pekee la Valladolid, Fausto Rossi akishangilia

No comments:

Post a Comment